Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Hos. 5:15-6:6

Bwana asema: Katika taabu yao watanitafuta kwa bidii:

Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tuataishi mbele zake. Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyeshayo nchi.

Ee Efraimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni kama wingu la asubuhi na kama umande utowekao mapema. Kwa sababu hiyo nimewakata-kata kwa vinya vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa change na hukumu yangu itatokea kama mwanga. Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 51:1-2, 16-19 (K) Hos. 6:6

(K) Ninavyotaka ni fadhili, si sadaka.

Ee Mungu, unirehemu,

Sawasawa na fadhili zako.

Kiasi cha wingi wa rehema zako,

Uyafute makosa yangu.

Unioshe kabisa na uovu wangu,

Unitakase dhambi zangu. (K)

Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,

Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.

Dhabihu za MUngu ni roho iliyovunjika;

Moyo uliovunjika na kupondeka,

Ee Mungu, hutaudharau. (K)

Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,

Uzijenge kuta za Yerusalemu.

Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,

Na sadaka za kuteketezwa, na kafara. (K)

SHANGILIO

Eze. 18:3

Tupilieni mbali nanyi makosa yenu yote mliyoyakosa yote, asema Bwana, jifanyieni moy mpya na roho mpya.

INJILI

Lk. 18:9-14

Yesu aliwaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyangโ€™anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mpato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Anna Mahiga Guest Sep 26, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Henry Sokoine Guest Nov 19, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Faith Kariuki Guest Jul 2, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Jul 7, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Janet Wambura Guest Oct 17, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthui Guest Sep 22, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Charles Mboje Guest Jun 25, 2020
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Frank Sokoine Guest May 19, 2020
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest May 3, 2020
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ David Kawawa Guest May 2, 2020
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Janet Sumari Guest Apr 17, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Mariam Hassan Guest Feb 16, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nekesa Guest Jan 27, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Joyce Aoko Guest Nov 24, 2019
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Peter Mugendi Guest Nov 14, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Moses Kipkemboi Guest Nov 10, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Alice Wanjiru Guest Sep 7, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Peter Otieno Guest Sep 3, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Alice Mwikali Guest Aug 25, 2019
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Jul 10, 2019
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Majaliwa Guest Mar 27, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Janet Sumari Guest Mar 14, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Feb 9, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Patrick Kidata Guest Jan 26, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ James Malima Guest Jan 15, 2019
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ David Chacha Guest Jan 5, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Robert Ndunguru Guest Jan 4, 2019
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Paul Kamau Guest Jan 3, 2019
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Grace Minja Guest Oct 9, 2018
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Charles Mrope Guest Oct 2, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Janet Mbithe Guest Jun 13, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest Jun 2, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Mar 31, 2018
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Dec 7, 2017
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Ann Wambui Guest Feb 11, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Ruth Wanjiku Guest Jan 17, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Joseph Mallya Guest Dec 9, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Oct 30, 2016
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Oct 7, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Agnes Lowassa Guest Oct 2, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Michael Onyango Guest Sep 5, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Anna Mchome Guest Jun 9, 2016
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Jun 4, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Apr 26, 2016
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Agnes Njeri Guest Feb 22, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Mercy Atieno Guest Jan 10, 2016
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Daniel Obura Guest Dec 11, 2015
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthoni Guest Nov 9, 2015
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Violet Mumo Guest Nov 1, 2015
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mahiga Guest Apr 12, 2015
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About