Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA,Β JUMAPILI, AGOSTI 27, 2023: JUMA LA 21 LA MWAKA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO I

Isa. 22:19-23

Bwana, Bwana wa majeshi, asema hivi: Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo. Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia; nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nvumba ya Yuda. Na ufunguo wa nvumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga. Nami nitamkaza kanta msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu

WIMBO WA KATIKATIΒ 

Zab. 138: 1-3, 6, 9 (K) 9

(K) Ee Bwana, fadhili zako ni za milele,Β 
Usiziache kazi za mikono yako.

Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,

Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu. (K)

Nitalishukuru jina lako,

Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwa maana umeikuza ahadi yako,
Kuliko jina lako lote.
Siku ile niliyokuita ulinitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. (K)

Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu,Β 

Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.
Ee Bwana, fadhili zako ni za milele;
Usiziache kazi za mikono yako. (K)

SOMO 2Β 

Rum 11: 33-36

Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake? Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena? Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu

SHANGILIO

Mt 11: 25

Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi,Β 
kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye
hekima na akili. ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya

INJILIΒ 

Ml 16:13-20

Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipo, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena Yohane Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaa- mbia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia. Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikufunulia hili, bali Baba vangu aliye mbinguni. Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. Ndipo alipowakataza sana wanafunziΒ wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo

Β 

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Kevin Maina Guest Jun 2, 2024
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Grace Mligo Guest Feb 22, 2024
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Dec 19, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ James Malima Guest Aug 18, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Jul 17, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Grace Mligo Guest Jan 21, 2023
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Dec 17, 2022
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Jul 2, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ David Kawawa Guest May 22, 2022
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Dec 1, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Mar 8, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Feb 1, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jan 7, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jan 1, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest Dec 23, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Nov 27, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Nov 1, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Aug 15, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest May 13, 2020
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Apr 30, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Jane Malecela Guest Apr 17, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ George Mallya Guest Feb 4, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Jan 12, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Jan 12, 2020
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ John Malisa Guest Dec 28, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Nov 13, 2019
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Nov 2, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Feb 24, 2019
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ George Wanjala Guest Feb 7, 2019
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Dec 2, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Aug 28, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest Jul 28, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Mar 14, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Nov 7, 2017
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Oct 8, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Sep 17, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Jun 29, 2017
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Apr 16, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Feb 19, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Feb 18, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jan 11, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Victor Mwalimu Guest May 31, 2016
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Mar 2, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Feb 11, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Dec 11, 2015
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ David Kawawa Guest Dec 1, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Nov 8, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Apr 25, 2015
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Apr 14, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Apr 4, 2015
Mwamini katika mpango wake.

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About