Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Yer. 20 : 10-13

Nimesikia mashutumu ya watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki; huenda akahahadaika; nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake. Lakini Bwana yu pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawakutenda kwa akili, wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe. Lakini Ee Bwana wa majeshi, wewe wawajaribu wenye haki, waona viuno na mioyo. nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu.

Mwimbieni Bwana; msifuni Bwana;Β 
Kwa maana ameiponya roho ya mhitajiΒ 
Katika mikono ya watu watendao maovu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 69 : 7-9, 13,16, 32-34 (K) 13

(K) Kwa wingi wa fadhili zako unijibu.

Kwa ajili yako nimestahimili laumu,
Fedheha imenifunika uso wangu.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
Maana wivu wa nyumba yako umenila,
Na laumu yao wanaokulaumu zimenipata. (K)

Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana,Β 
Wakati ukupendezao; Ee Mungu,
Kwa wingi wa fadhili zako unijibu,
Katika kweli ya wokovu wako.
Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema,
Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. (K)

Walioonewa watakapoona watafurahi;
Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yetu ihuishwe.
Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji,
Wala hawadharau wafunga wake.
Mbingu na nchi zimsifu
Bahari na vyote viendavyo ndani yake. (K)

SOMO 2

Rum. 5:12-15

Kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia uli mwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi; maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria; walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, alive mfano wake yeye atakayekuja. Lakini karama ile haikuwa kama lile kosa; kwa maana ikiwa kwa kukosa kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema yake mwanadamu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale wengi.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

SHANG1LIO

Mdo. 16:14

Aleluya, aleluya,
Fungua mioyo yetu, ee Bwana,Β 
Ili tuyatunze maneno ya Mwanao.
Aleluya.

INJILI

Mt. 10:26-33

Yesu aliwaambia mitume wake: Msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana. Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba. Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum, Je! mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu; lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope basi; bora nyinyi kuliko mashomoro wengi. Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Apr 14, 2024
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Feb 2, 2024
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Jan 22, 2024
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Peter Otieno Guest Jan 5, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Nov 23, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Sep 23, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Sep 12, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Sep 5, 2023
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Grace Mligo Guest Aug 31, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Jul 5, 2023
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest May 17, 2023
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Apr 24, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Oct 31, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Aug 14, 2022
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Jul 28, 2022
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Jun 14, 2022
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Apr 19, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Dec 18, 2021
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Oct 19, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Jun 29, 2021
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest Jun 14, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest May 21, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Jan 31, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Dec 1, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Oct 12, 2020
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Jun 24, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Feb 20, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Feb 9, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Dec 21, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Martin Otieno Guest Nov 21, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Jul 31, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Sep 11, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Jun 7, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Victor Mwalimu Guest May 17, 2018
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Mar 20, 2018
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ James Malima Guest Aug 27, 2017
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Apr 24, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Jan 26, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Nov 27, 2016
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Lydia Mzindakaya Guest Aug 14, 2016
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Jul 12, 2016
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Jun 6, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest May 28, 2016
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest May 20, 2016
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Apr 13, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ George Wanjala Guest Apr 7, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Mar 7, 2016
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Oct 31, 2015
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Jul 19, 2015
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Jun 9, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About