SOMO 1
Kut. 24:3-8
Musa aliwambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote; watu wote wakajibu kwa sauti moja, wakasema, Maneno yote aliyoyanena Bwana tutayatenda. Basi Musa akayaandika maneno yote ya Bwana, akaondoka asubuhi na mapema, akajenga madhabahu chini ya mlima, na nguzo kumi na mbili, kwa hesabu ya kabila kumi na mbili za Israeli, akapeleka vijana wa wana wa Israeli, waliotoa sadaka za kuteketezwa, wakamchinjia Bwana sadaka za amani za ng’ombe. Musa akatwaa nusu ya ile damu, akaitia katika mabakuli; na nusu ya ile damu akainyunyiza juu ya madhabahu. Kisha akakitwaa kitabu cha agano akakisoma masikioni mwa watu; wakasema, Hayo yote aliyoyanena Bwana tutayatenda, nasi tutatii. Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 50:1-2, 5-6, 14-15 (K) 14 (K)
Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru. Mungu, Mungu Bwana, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hata machweo yake. Tokea Sayuni,, ukamilifu wa uzuri, Mungu amemulika. (K)
Nikusanyieni wacha Mungu wangu, Waliofanya agano nami kwa dhabihu. Na mbingu zitatangaza haki yake, Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu. (K)
Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako. Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza. (K)
SHANGILIO
Zab. 8:15
Aleluya, aleluya,
Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao, hulisikia neno la Mungu na kulishika.
Aleluya.
INJILI
Mt. 13:24 – 30
Yesu aliwatolea makutano mfano akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala akaja adui yake akapanda magugu katikati ya agano, akaenda zake. Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu? Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye? Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo. Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.
Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.
Edwin Ndambuki (Guest) on February 12, 2024
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Lucy Wangui (Guest) on January 29, 2024
Neema na amani iwe nawe.
Margaret Mahiga (Guest) on January 2, 2024
Endelea kuwa na imani!
Betty Akinyi (Guest) on December 5, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
James Malima (Guest) on December 4, 2023
Mungu akubariki!
Hellen Nduta (Guest) on September 17, 2023
Mwamini katika mpango wake.
Miriam Mchome (Guest) on July 24, 2023
Rehema zake hudumu milele
Jackson Makori (Guest) on June 24, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Andrew Mchome (Guest) on January 22, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Peter Mugendi (Guest) on January 20, 2023
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Lydia Mahiga (Guest) on January 7, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
George Tenga (Guest) on November 19, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Grace Majaliwa (Guest) on August 30, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Janet Sumaye (Guest) on August 5, 2022
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
John Mushi (Guest) on May 18, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Nancy Akumu (Guest) on February 20, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Josephine Nekesa (Guest) on February 19, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
Simon Kiprono (Guest) on January 28, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
Jackson Makori (Guest) on January 3, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
Miriam Mchome (Guest) on December 25, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
Ruth Wanjiku (Guest) on August 27, 2021
Baraka kwako na familia yako.
George Ndungu (Guest) on December 4, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Andrew Odhiambo (Guest) on September 6, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Vincent Mwangangi (Guest) on July 5, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rose Lowassa (Guest) on May 11, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Esther Cheruiyot (Guest) on January 15, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rose Mwinuka (Guest) on January 10, 2020
Dumu katika Bwana.
Esther Nyambura (Guest) on June 23, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Moses Kipkemboi (Guest) on June 15, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Andrew Mchome (Guest) on June 11, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
James Malima (Guest) on June 9, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Monica Lissu (Guest) on May 7, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
George Ndungu (Guest) on January 28, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Grace Mushi (Guest) on October 26, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
Samson Mahiga (Guest) on October 15, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Joseph Kiwanga (Guest) on September 9, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Dorothy Nkya (Guest) on June 19, 2018
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Ann Awino (Guest) on December 11, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Charles Mrope (Guest) on December 5, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
John Kamande (Guest) on June 23, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Betty Akinyi (Guest) on February 18, 2017
Nakuombea 🙏
Lydia Wanyama (Guest) on August 15, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
Philip Nyaga (Guest) on July 16, 2016
Sifa kwa Bwana!
Anthony Kariuki (Guest) on April 11, 2016
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Raphael Okoth (Guest) on March 1, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Victor Kamau (Guest) on December 14, 2015
Rehema hushinda hukumu
Diana Mallya (Guest) on December 2, 2015
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Elizabeth Malima (Guest) on September 4, 2015
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Thomas Mwakalindile (Guest) on June 8, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Andrew Mchome (Guest) on April 9, 2015
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia