Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, MARCHI 31, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Hek. 2:1, 12-22

Wasiomsadikia Mungu walisema hivi, huku wakimfikiri yasiyo kweli, Zaidi ya hayo na tumwotee mtu wa haki, maana hatuna haja naye, naye yu kinyume cha matendo yetu; atukaripia ya kama tumeiasi torati, na kutushitaki ya kama tumekosa adabu. Asema ya kwamba anamjua Mungu, na kujiita mtumishi wa Bwana. Ametuwia magombezi ya fikira zetu. Hata kumtazama twaona ni kugumu; maan amaisha yake si sawasawa na masiha ya wengine, na mwenendo wake ni wa kigeni. Tuanhesabiwa naye kuwa kama madini hafifu; anajitenga na njia zetu kama na uchafu. Wenye haki asema kuwa mwisho wao ni heri; hujivuna ya kwamba Mungu ndiye baba yake.

Haya na tuone kama maneno yake ni kweli; tufanye kujaribu yatakayompata wakati wa mwisho wake; mradi mwenye haki akiwa ni mwana wa Mungu, Yeye atamtegemeza na kumwokoa mikononi mwa adui zake. Na tumhakikishe kwa jeuri na maumivu, ili tujifunze upole wake na kuithibitisha saburi yake akidhulumiwa. Hata tumhukumu auawe mauti ya aibu, maana ataangaliwa sawasawa na maneno yake.

Ndivyo walivyosemezana, wakakosea kabisa. Kwa maana uovu wao uliwapofusha; hawakuzijua siri za Mungu; wala hawakuutarajia mshahara wa utakatifu, wala kudhani ya kwamba iko thawabu kwao wenye roho zisizo na hatia.

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 34:16-20, 22 (K) 18

(K) Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo.

Uso wa Bwan ani juu ya watenda mabaya,

Aliondoe kumbukumbu lao duniani.

Walilia, naye Bwan akasikia,

Akawaponya na taabu zao zoe. (K)

Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,

Na waliopondeka roho huwaokoa.

Mateso ya mwenye haki ni mengi,

Lakini Bwana humponya nayo yote. (K)

Huihifadhi mifupa yake yote,

Haukuvunjika hata mmoja.

Bwana huzikombo a nafsi za watumishi wake,

Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao. (K)

SHANGILIO

Lk. 8:15

Heri wale walishikao neno la Mungu katika moyo wao mwema na mnyofu, na wazaao matunda katika uvumilivu.

INJILI

Yn. 7:1-2, 25-30

Baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuw awakitafuta kumwua.

Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu. Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye laipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.

Basi baadhi ya watu wa yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue? Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu tuna jua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo? Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.

Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi. Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.

Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Moses Kipkemboi Guest May 13, 2024
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Feb 17, 2024
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mzindakaya Guest Dec 1, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Joseph Njoroge Guest May 13, 2023
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Stephen Mushi Guest Mar 13, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Feb 8, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ John Malisa Guest Dec 29, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Brian Karanja Guest Nov 12, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest Nov 9, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ John Kamande Guest Sep 23, 2022
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ David Sokoine Guest Aug 8, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Francis Mrope Guest May 19, 2022
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Jan 30, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Stephen Malecela Guest Jul 10, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Apr 20, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Thomas Mtaki Guest Apr 14, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Peter Mbise Guest Mar 8, 2021
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kitine Guest Jan 29, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Janet Sumari Guest Jan 10, 2021
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Ruth Wanjiku Guest Sep 27, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Isaac Kiptoo Guest Aug 13, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mahiga Guest Aug 12, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Samson Tibaijuka Guest Mar 4, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest Feb 3, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Anna Kibwana Guest Jan 12, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mutheu Guest Nov 3, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Agnes Sumaye Guest Oct 11, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Jackson Makori Guest Oct 3, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Stephen Malecela Guest Sep 27, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kiwanga Guest Mar 12, 2019
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Monica Lissu Guest Dec 2, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Mariam Kawawa Guest Oct 14, 2018
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Mwakalindile Guest Sep 28, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Sep 10, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Jacob Kiplangat Guest Jun 9, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Frank Sokoine Guest May 16, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest Jun 27, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Ruth Wanjiku Guest Apr 2, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Alex Nakitare Guest Mar 11, 2017
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest Feb 9, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest Jan 9, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Anna Malela Guest Dec 13, 2016
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ David Sokoine Guest Nov 20, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mutheu Guest Sep 27, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Mwakalindile Guest Sep 11, 2016
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrema Guest Sep 9, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Monica Nyalandu Guest Jun 20, 2016
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest Sep 26, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Jul 9, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Jun 16, 2015
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About