Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, MARCHI 31, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Hek. 2:1, 12-22

Wasiomsadikia Mungu walisema hivi, huku wakimfikiri yasiyo kweli, Zaidi ya hayo na tumwotee mtu wa haki, maana hatuna haja naye, naye yu kinyume cha matendo yetu; atukaripia ya kama tumeiasi torati, na kutushitaki ya kama tumekosa adabu. Asema ya kwamba anamjua Mungu, na kujiita mtumishi wa Bwana. Ametuwia magombezi ya fikira zetu. Hata kumtazama twaona ni kugumu; maan amaisha yake si sawasawa na masiha ya wengine, na mwenendo wake ni wa kigeni. Tuanhesabiwa naye kuwa kama madini hafifu; anajitenga na njia zetu kama na uchafu. Wenye haki asema kuwa mwisho wao ni heri; hujivuna ya kwamba Mungu ndiye baba yake.

Haya na tuone kama maneno yake ni kweli; tufanye kujaribu yatakayompata wakati wa mwisho wake; mradi mwenye haki akiwa ni mwana wa Mungu, Yeye atamtegemeza na kumwokoa mikononi mwa adui zake. Na tumhakikishe kwa jeuri na maumivu, ili tujifunze upole wake na kuithibitisha saburi yake akidhulumiwa. Hata tumhukumu auawe mauti ya aibu, maana ataangaliwa sawasawa na maneno yake.

Ndivyo walivyosemezana, wakakosea kabisa. Kwa maana uovu wao uliwapofusha; hawakuzijua siri za Mungu; wala hawakuutarajia mshahara wa utakatifu, wala kudhani ya kwamba iko thawabu kwao wenye roho zisizo na hatia.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 34:16-20, 22 (K) 18

(K) Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo.

Uso wa Bwan ani juu ya watenda mabaya,

Aliondoe kumbukumbu lao duniani.

Walilia, naye Bwan akasikia,

Akawaponya na taabu zao zoe. (K)

Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,

Na waliopondeka roho huwaokoa.

Mateso ya mwenye haki ni mengi,

Lakini Bwana humponya nayo yote. (K)

Huihifadhi mifupa yake yote,

Haukuvunjika hata mmoja.

Bwana huzikombo a nafsi za watumishi wake,

Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao. (K)

SHANGILIO

Lk. 8:15

Heri wale walishikao neno la Mungu katika moyo wao mwema na mnyofu, na wazaao matunda katika uvumilivu.

INJILI

Yn. 7:1-2, 25-30

Baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuw awakitafuta kumwua.

Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu. Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye laipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.

Basi baadhi ya watu wa yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue? Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu tuna jua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo? Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.

Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi. Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.

Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest May 13, 2024
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Feb 17, 2024
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Lydia Mzindakaya Guest Dec 1, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest May 13, 2023
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Stephen Mushi Guest Mar 13, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ George Ndungu Guest Feb 8, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ John Malisa Guest Dec 29, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Brian Karanja Guest Nov 12, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Martin Otieno Guest Nov 9, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ John Kamande Guest Sep 23, 2022
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Aug 8, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest May 19, 2022
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Jan 30, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Jul 10, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Apr 20, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Apr 14, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Mar 8, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Jan 29, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jan 10, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Sep 27, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Aug 13, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Aug 12, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Mar 4, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Sharon Kibiru Guest Feb 3, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Jan 12, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Nov 3, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Oct 11, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Oct 3, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Sep 27, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest Mar 12, 2019
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest Dec 2, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Oct 14, 2018
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Sep 28, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Sep 10, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Jun 9, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest May 16, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Jun 27, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Apr 2, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Mar 11, 2017
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ John Lissu Guest Feb 9, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Jan 9, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Dec 13, 2016
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Nov 20, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Sep 27, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Sep 11, 2016
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Sep 9, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Jun 20, 2016
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Sep 26, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Jul 9, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Jun 16, 2015
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About