Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, APRILI 5, 2022: JUMANNE JUMA LA 5 LA KWARESIMA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Hes. 21:4-9

Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu; ili kuizunguka nchi ya Edomu watu wakafa moyo kwa sababu ya ile njia. Watu wakamnung’unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.

Bwana akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa. Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung’unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa Bwana, atuondolee nyoka hawa. Basi, Musa akawaombea watu. Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo, ataishi. Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 102:1-2, 15-20 (K) 1

(K) Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, kilio changu kikufikie.

Ee Bwana, usikie kuomba kwangu,

Kilio change kikufikie,

Usinifiche uso wako siku ya shida yangu,

Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi. (K)

Kisha mataifa wataliogopa jina la Bwana,

Na wafalme wote wa dunia utukufu wako;

Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni,

Atakapoonekana katika utukufu wake,

Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa,

Asiyadharau maombi yao. (K)

Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo,

Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.

Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu,

Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,

Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa,

Na kuwafungua walioandikiwa kufa. (K)

SHANGILIO

Yn. 8:12

Β 

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema Bwana, yeye anifuataye, atakuwa na nuru ya uzima.

INJILI

Β 

Yn. 8:21-30

Β 

Yesu aliwaambia Mafarisayo: Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi mtakufa katika dhambi yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja.

Basi, Wayahudi wakasema, Je! Atajiua! Kwa kuwa asema, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja?

Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu. Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.

Basi wakamwambia, U nani wewe? Yesu akawaambia, Hasa neno lilo hilo ninalowaambia. Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu; lakini yeye aliyenipeleka ni kweli, nami niliyoyasikia kwake ndiyo ninenayo katika ulimwengu.

Wala hawakutambua ya kuwa anawatajia Baba. Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo. Naye aliyenipeleka yu pamoja nami; hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.

Naye alipokuwa akisema hayo, wengi walimwamwini.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Michael Onyango Guest Jul 17, 2024
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Apr 16, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Jan 20, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Nov 23, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Jul 29, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Jul 26, 2023
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Jul 9, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest May 7, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Feb 5, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Nov 20, 2022
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Oct 21, 2022
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Sep 28, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Aug 22, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Jul 5, 2022
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Apr 8, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Dec 10, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Nov 11, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Aug 2, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jul 6, 2021
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ John Lissu Guest Jun 19, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest May 29, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest May 4, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Apr 19, 2021
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Apr 1, 2021
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest Nov 28, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Sep 4, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest May 8, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest Apr 7, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Sep 8, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Jul 19, 2019
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Diana Mumbua Guest May 28, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ David Kawawa Guest Apr 29, 2019
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Mar 26, 2019
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Jan 24, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ John Mushi Guest Dec 12, 2018
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Jul 19, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest May 11, 2018
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Apr 6, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Apr 3, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Feb 14, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Feb 5, 2017
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Nov 7, 2016
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Oct 30, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Jul 12, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest May 8, 2016
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest May 2, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Peter Mwambui Guest Dec 11, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Dec 8, 2015
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Oct 21, 2015
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Apr 21, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About