Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2022: IJUMAA, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2022
IJUMAA, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SHEREHE YA KUPASHWA HABARI YA KUZALIWA BWANA

Β 

SOMO 1

Isa. 7:10 – 14
Bwana alisema na Ahazi akinena, Jitakie ishara ya Bwana, Mungu wako; itake katika mahali palipo chini sana, au katika mahali palipo juu sana. Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka, wala sitamjaribu Bwana. Naye akasema, Sikilizeni sana, enyi nyumba ya Daudi; Je! Ni neno dogo kwenu kuwachosha wanadamu, hata mkataka kumchosha Mungu wangu pia? Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, Bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 40:6 – 10 (K) 7 , 8

(K) Tazama, nimekuja, Ee Bwana, kuyafanya mapenzi yako.

Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua,
Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Ndipo niliposema, Tazama nimekuja. (K)

Katika gombo la chuo nimeandikiwa
Kuyafanya mapenzi yako,
Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;
Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. (K)

Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa,
Sikuizuia midomo yangu; Ee Bwana, unajua. (K)

Sikusitiri haki yako moyoni mwangu;
Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Sikuficha fadhili zako wala kweli yako
Katika kusanyiko kubwa. (K)

SOMO 2

Ebr. 10:4 – 10
Haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari; Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo; Ndipo niliposema, Tazama nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) niyafanye mapenzi yako, Mungu.
Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati), ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili. Katika mapenzi hayo tumepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.

Neno la Bwana…
Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO

Yn. 1:14

Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, nasi tukaona utukufu wake.

INJILI

Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema. Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye ju, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu. Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa; kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Jun 23, 2024
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest May 28, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest May 27, 2024
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Grace Mligo Guest Feb 20, 2024
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Oct 18, 2023
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Oct 17, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Aug 15, 2023
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Aug 5, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Agnes Lowassa Guest May 20, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Apr 11, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Aug 11, 2022
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Jan 20, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Jan 3, 2022
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Oct 30, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ John Kamande Guest Apr 22, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Grace Wairimu Guest Apr 12, 2021
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Apr 7, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest Feb 26, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jan 7, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Dec 30, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Aug 30, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Apr 29, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Mar 31, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Jane Muthui Guest Feb 17, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ David Nyerere Guest Feb 5, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Oct 30, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Sep 24, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest May 8, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ John Mushi Guest Feb 20, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Nov 3, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Oct 18, 2018
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest May 17, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest Apr 30, 2018
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Jan 28, 2018
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Jan 16, 2018
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Nov 13, 2017
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Jun 8, 2017
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Jun 7, 2017
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Mar 27, 2017
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Jan 6, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Dec 29, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Nov 14, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ David Musyoka Guest May 28, 2016
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Mar 22, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Feb 19, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Dec 13, 2015
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Nov 30, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Oct 5, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Sep 24, 2015
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Jul 9, 2015
Rehema zake hudumu milele

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About