Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, MACHI 22, 2022: JUMATANO, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1 - Kumb. 4:1, 5-9

Musa aliwaambia makutano: Ee Israeli, zisikilizeni amri na hukumu niwafundishazo, ili mmzitende; mpate kuishi na kuingia na kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wa baba zenu.Angalieni nimewafundisha amri na hukumu, vile vile kama Bwana, Mungu wangu, alivyoniamuru, ili mzitende katika nchi mwmingiayo ili kuimiliki. Zishikeni basi,5 mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia⁡ amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili. Kwa maana liko taifa gani kubwa, lililo na Mungu aliye karibu nao, kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo? Tena liko taifa gani kubwa, lililo na amri na hukumu zenye haki kama torati hii yote, ninayoiweka mbele yenu leo.

Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI - Zab. 147:12-13, 15-16, 19-20 (K) 12(K)

Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;

Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,Amewabariki wanao ndani yako. (K)

Huipeleka amri yake juu ya nchi,Neno lake lapiga mbio sana.

Ndiye atoaye theluji kama sufu,Huimwaga barafu yake kama majivu. (K)

Humhubiri Yakobo neno lake,Na Israeli amri zake na hukumu zake.

Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,Wala hukumu zake hawakuzijua. (K)

SHANGILIO

Mbegu neno la Mungu, mpanzi lakini ni Kristu; Yeyote ampataye, ataishi milele.

INJILI - Mt. 5:17-19

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Msidhani kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme mbinguni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Feb 6, 2024
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Nov 26, 2023
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Francis Njeru Guest Nov 23, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Oct 13, 2023
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest Dec 24, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Elijah Mutua Guest Jul 7, 2022
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest May 14, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Apr 5, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Jul 20, 2021
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Jul 11, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Jun 29, 2021
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Jun 24, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Jun 12, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Apr 8, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Feb 21, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ John Mushi Guest Feb 6, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Jan 20, 2021
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Dec 17, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Dec 8, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Aug 10, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Jun 25, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest May 25, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Apr 16, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Feb 7, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Jan 31, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ John Malisa Guest Jan 10, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Dec 25, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Dec 24, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Oct 21, 2019
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Jun 18, 2019
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Apr 10, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Oct 3, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Sep 18, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Aug 5, 2018
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ George Ndungu Guest Jun 14, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest May 9, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest May 5, 2018
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Dec 11, 2017
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Peter Mwambui Guest Dec 3, 2017
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Nov 24, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Nov 3, 2017
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Sep 28, 2017
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ George Wanjala Guest Aug 16, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Feb 28, 2017
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest May 21, 2016
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Feb 9, 2016
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Nov 29, 2015
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Aug 24, 2015
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Jul 17, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Jun 18, 2015
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About