Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, DOMINIKA YA 5 YA KWARESIMA, MWAKA C

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1: Isa. 43:16-21

Bwana asema hivi, yeye afanyaye njia katika bahari, na mahali pa kupita katika maji yenye nguvu; atoaye gari na farasi, jeshi la askari na uwezo; wamelala, hawataondoka; wametoweka, wamezimwa mfano wa utambi. Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani. Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani. Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni; kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu, wateule wangu; watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.

WIMBO WA KATIKATI: Zab. 126, (K) 3

(K) Bwana alitutendea mambo makuu, tulikuwa tukifurahi.

Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni,

Tulikuwa kama waotao ndoto.

Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko.

Na ulimi wetu kelele za furaha. (K)

Ndipo waliposema katika mataifa,

Bwana amewatendea mambo makuu.

Bwana alitutendea mambo makuu,

Tulikuwa tukifurahi. (K)

Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa,

Kama vijito vya Kusini.

Wapandao kwa machozi,

Watavuna kwa kelele za furaha. (K)

Ingawa mtu anakwenda zake akilia,

Azichukuapo mbegu za kupanda.

Hakika atarudi kwa kelele za furaha,

Aichukuapo miganda yake. (K)

SOMO 2: Flp. 3:8-14

Nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo; tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa Imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa Imani; ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake; ili nipate kwa njia yoyote kuifikia kiyama ya wafu. Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.

SHANGILIO: Yoe. 2:12, 13

Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, kwa maana ni mwenye neema na huruma.

INJILI: Yn. 8:1-11

Yesu akaenda mpaka mlima wa Mizeituni. Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha.

Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati. Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini. Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje? Nao wakasema neno hili wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki.

Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.

Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia? Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Joyce Nkya Guest May 18, 2024
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Joseph Njoroge Guest Sep 28, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Francis Mtangi Guest Sep 20, 2023
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Victor Malima Guest Jul 24, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest Jun 24, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Peter Tibaijuka Guest May 7, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Apr 15, 2023
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Feb 14, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Joyce Aoko Guest Jan 27, 2023
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Chris Okello Guest Oct 13, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Isaac Kiptoo Guest May 28, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest Mar 22, 2022
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mushi Guest Oct 27, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Irene Akoth Guest Aug 11, 2021
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Patrick Kidata Guest Feb 21, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Charles Wafula Guest Dec 15, 2020
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Raphael Okoth Guest Dec 11, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Ruth Wanjiku Guest Nov 30, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ David Ochieng Guest Nov 5, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Anna Mahiga Guest Sep 24, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Mariam Hassan Guest Jul 28, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Irene Makena Guest Jul 9, 2020
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Grace Njuguna Guest Apr 18, 2020
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Edward Lowassa Guest Feb 28, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Mary Sokoine Guest Feb 24, 2020
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Mwakalindile Guest Feb 22, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ George Tenga Guest Jan 5, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest Oct 11, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Victor Kamau Guest Aug 1, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kiwanga Guest Jun 15, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Anna Mahiga Guest Apr 25, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Apr 17, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Grace Njuguna Guest Mar 28, 2018
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Janet Wambura Guest Mar 24, 2018
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest Jan 23, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Francis Njeru Guest Jan 23, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Dec 28, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Nov 8, 2016
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Jul 20, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Peter Mugendi Guest Jul 10, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Mary Kendi Guest May 26, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Victor Kimario Guest May 26, 2016
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Thomas Mtaki Guest Mar 14, 2016
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kawawa Guest Jan 30, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Kevin Maina Guest Jan 18, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Carol Nyakio Guest Nov 27, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Oct 19, 2015
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Kenneth Murithi Guest Oct 11, 2015
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Charles Wafula Guest Sep 25, 2015
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Samson Tibaijuka Guest Aug 21, 2015
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About