Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, MACHI 21, 2022: JUMATATU , JUMA LA 3 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

2 Fal. 5:1-15

Naamani, jemadari wa jeshi la mfalme wa Shamu, alikuwa mtu mkubwa mbele ya bwana wake, na mwenye kuheshimiwa, kwa sababu kwa mkono wake Bwana alikuwa amewapa Washami kushinda; tena likuwa mtu hodari wa vita; lakini alikuwa mwenye ukoma. Na Washami walikuwa wametoka vikosi vikosi, wakachukua mfungwa mmoja kijana mwanamke kutoka nchi ya Israeli; naye akamhudumia mkewe Naamani. Akamwambia bibi yake, Laiti bwana wangu angekuwa pamoja na yule nabii aliyeko Samaria! Maana angemponya ukoma wake. Mtu mmoja akaingia, akamwambia bwana wake, akasema, Yule kijana mwanamke aliyetoka nchi ya Israeli asema hivi na hivi. Mfalme wa Sahmu akasema, Haya! Basi, mimi nitampelekea mfalame wa Israeli waraka. Basi akaenda zake, akachukua mikononi mwake talanta kumi za fedha, na vipande vya dhahabu elfu sita, na mavazi kumi.

Akampelekea mfalme wa Israeli waraka ule, kusema, Waraka huu utakapokuwasilia, tazama, nimemtuma mtumishi wangu Naamni kwako, ili upate kumponya ukoma wake. Ikawa, mfalme wa Israeli alipousoma waraka, alirarua mavazi yake, akasema, Je! Mimi ni Mungu, niue na kuhuisha, hata mtu huyu akanipelekea mtu nimponye ukoma wake? Fahamuni, basi, nakusihini, mwone ya kuwa mtu huyu anataka kugombana nami.

Ikawa, Elisha, yule mtu wa Mungu, aliposikia kwamba mfalme wa Israeli ameyararua mavazi yake, ndipo akatuma mtu kwa mfalme, akisema, Mbona umeyararua mavazi yako? Na aje sana kwangu mimi, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.

Basi Naamani akaja na farasi wake na magari yake, akasimama mlangoni pa nyumba ya Elisha. Naye Elisha akampelekea mjumbe, akisema. Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itakurudia nawe utakuwa safi. Lakini Naaman akakasirika, akaondoka, akasema, Tazama, nalidhania, Bila shaka atatoka kwangu, na kusimama, na kuomba kwa jina la Bwana, Mungu wake, na kupitisha mkono wake mahali penye ugonjwa, na kuniponya mimi mwenye ukoma Je! Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko maji yote ya Israeli? Je! Siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? Akageuka, akaondoka kwa hasira.

Watumishi wake wakamkaribia, wakamwambia, wakisema, Baba yangu, kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? Je! Si zaidi basi, akikuambia, Jioshe, uwe safi? Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; naye nyama ya wmili wak eikarudi ikawa kama nyam aya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi.

Akamrudia yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake; akasema, Sasa tazama, najua ya kwamba hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli, basi nakuomba upokee mbaraka kwa mtumwa wako.

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 42:1-2, 43:3-4 (K) 42:3

(K) Nafsi yangu inamwonea kiu Mungu, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu.

Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji.

Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu. (K)

Nafsi yangu inamwonea kiu Mungu, Mungu aliye hai,

Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu? (K)

Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze,

Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu

Na hata maskani yako. (K)

Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu,

Kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu. (K)

SHANGILIO

Yn. 8:12

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema Bwana, Yeye anifuataye, atakuwa na nuru ya uzima.

INJILI

Lk. 4:24-30

Yesu alifika Nazareti akawaambia makutano hekaluni: Amin, nawaambia ya kuwa, Hakuna nabii mwenye kukubaliwa katika nchi yake mwenyewe. Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima; wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni. Tena, palikuwa na weny eukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha, wala hapana aliyetakazwa ila Naamani, mtu wa Shamu.

Wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo. Wakaondoka wakamtoa nje ya mji, wakampeleka mpaka ukingo wa kilima ambacho mji wao umejengwa juu yake, wapate kumtupa chini; lakini yeye alipiita katikati yao, akaenda zake.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest May 29, 2024
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Edward Chepkoech Guest May 28, 2024
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Patrick Mutua Guest May 23, 2024
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrema Guest Apr 21, 2024
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Dec 22, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Grace Majaliwa Guest Dec 14, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Anna Kibwana Guest Sep 5, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Henry Mollel Guest Jul 28, 2023
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Jun 30, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Victor Malima Guest Mar 26, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Nkya Guest Nov 29, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Edward Lowassa Guest Oct 22, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ David Sokoine Guest Oct 11, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Mwakalindile Guest May 29, 2022
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ James Malima Guest Apr 11, 2022
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Victor Mwalimu Guest Dec 17, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Aug 15, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nekesa Guest Jun 13, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Philip Nyaga Guest Mar 17, 2021
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Feb 16, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Joyce Aoko Guest Nov 12, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Joseph Njoroge Guest Oct 19, 2020
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Rose Kiwanga Guest Aug 16, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Mary Kendi Guest Aug 5, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kikwete Guest Jul 9, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kawawa Guest Jul 6, 2020
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Apr 6, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Edith Cherotich Guest Apr 3, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Mar 30, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Tabitha Okumu Guest Mar 9, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Samuel Were Guest Jan 16, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Mary Kendi Guest Aug 20, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Victor Malima Guest May 4, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Anna Malela Guest Apr 29, 2019
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Raphael Okoth Guest Nov 3, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Ruth Kibona Guest Jun 12, 2018
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Rose Kiwanga Guest Apr 28, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Anthony Kariuki Guest Mar 22, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Alex Nyamweya Guest Nov 24, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Edwin Ndambuki Guest Apr 22, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Patrick Akech Guest Dec 19, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mzindakaya Guest Nov 20, 2016
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Alex Nyamweya Guest Jun 16, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest May 13, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kawawa Guest Mar 23, 2016
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Hellen Nduta Guest Feb 17, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Anna Mahiga Guest Jan 19, 2016
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest Dec 6, 2015
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Mary Njeri Guest Nov 4, 2015
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Joyce Mussa Guest Sep 24, 2015
Sifa kwa Bwana!

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About