Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, JUNI 11, 2023: SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Kum. 8:2-3;14-16

Musa aliwaambia makutano: Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu, kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 147:12-15,19-20 (K) 12

(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.

Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;

Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.

Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,

Amewabariki wanao ndani yako. (K)

Ndiye afanyaye amani mipakani mwako,

Akushibishaye kwa unono wa ngano.

Huipeleka amri yake juu ya nchi,

Neno lake lapiga mbio sana. (K)

Humhubiri Yakobo neno lake,

Na Israeli amri zake na hukumu zake.

Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,

Wala hukumu zake hawakuzijua.

aleluya. (K)

SOMO 2

1Kor. 10:16-17

Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

SHANG1LIO

Yn. 6:51

Aleluya, aleluya,

Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; asema Bwana; mtu akila chakula hiki, ataishi milele.

Aleluya.

INJILI

Yn. 6:51-58

Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule? Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Jun 24, 2024
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Sarah Achieng Guest Jun 5, 2024
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Victor Kamau Guest Feb 27, 2024
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mushi Guest Feb 24, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kangethe Guest Jan 26, 2024
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ John Mushi Guest Oct 2, 2023
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ David Ochieng Guest May 21, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Ruth Wanjiku Guest Apr 4, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Janet Sumaye Guest Feb 10, 2023
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Violet Mumo Guest Jan 31, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Masanja Guest Dec 8, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Aug 17, 2022
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Jan 10, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Grace Mligo Guest Jan 6, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Alice Mwikali Guest Dec 10, 2021
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ George Tenga Guest Sep 17, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Faith Kariuki Guest May 20, 2021
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Robert Okello Guest Mar 27, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Odhiambo Guest Mar 24, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Henry Mollel Guest Feb 20, 2021
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Feb 2, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Charles Wafula Guest Jul 8, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Irene Akoth Guest Jun 25, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Vincent Mwangangi Guest Mar 12, 2020
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kawawa Guest Feb 23, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Jan 23, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Richard Mulwa Guest Jan 14, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Anna Sumari Guest Jun 25, 2019
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest Jan 6, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Moses Kipkemboi Guest Dec 28, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Joseph Mallya Guest Dec 26, 2018
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Mercy Atieno Guest Sep 4, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ John Kamande Guest Jul 15, 2018
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Peter Otieno Guest Jul 5, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Victor Malima Guest Jul 4, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Lucy Kimotho Guest Oct 13, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Monica Lissu Guest Aug 5, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Ruth Kibona Guest Jul 17, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrema Guest May 25, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Sarah Karani Guest Feb 25, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest Feb 20, 2017
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Brian Karanja Guest Feb 14, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Paul Ndomba Guest Feb 4, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Carol Nyakio Guest Aug 28, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Peter Tibaijuka Guest Apr 9, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Sarah Mbise Guest Mar 9, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Raphael Okoth Guest Feb 4, 2016
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Diana Mumbua Guest Sep 23, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kawawa Guest Aug 10, 2015
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Hellen Nduta Guest Jun 13, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About