Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2022: JUMATANO JUMA LA 3 LA KWARESIMA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2022: JUMATANO JUMA LA 3 LA KWARESI

SOMO 1 - Kumb. 4:1, 5-9

Musa aliwaambia makutano: Ee Israeli, zisikilizeni amri na hukumu niwafundishazo, ili mmzitende; mpate kuishi na kuingia na kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wa baba zenu.
Angalieni nimewafundisha amri na hukumu, vile vile kama Bwana, Mungu wangu, alivyoniamuru, ili mzitende katika nchi mwmingiayo ili kuimiliki. Zishikeni basi, mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili. Kwa maana liko taifa gani kubwa, lililo na Mungu aliye karibu nao, kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo? Tena liko taifa gani kubwa, lililo na amri na hukumu zenye haki kama torati hii yote, ninayoiweka mbele yenu leo.
Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI - Zab. 147:12-13, 15-16, 19-20 (K) 12

(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.

Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)

Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana.
Ndiye atoaye theluji kama sufu,
Huimwaga barafu yake kama majivu. (K)

Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua. (K)

SHANGILIO

Mbegu neno la Mungu, mpanzi lakini ni Kristu; Yeyote ampataye, ataishi milele.

INJILI - Mt. 5:17-19

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Msidhani kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme mbinguni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Jun 23, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Apr 23, 2024
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Apr 23, 2024
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Jun 12, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Lydia Mzindakaya Guest Jun 8, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ John Lissu Guest Feb 10, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Jan 30, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Jan 6, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Dec 20, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Oct 27, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Francis Mtangi Guest Jun 26, 2022
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Jun 23, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Jun 2, 2022
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Feb 19, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Dec 30, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Diana Mumbua Guest Sep 19, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Sep 7, 2021
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Aug 25, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Violet Mumo Guest Apr 5, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Janet Sumaye Guest Feb 2, 2020
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Jan 5, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Oct 2, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Sep 27, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Aug 12, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Jul 25, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Jul 2, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Feb 20, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Dec 28, 2018
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Jun 18, 2018
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Janet Wambura Guest Mar 20, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Mar 10, 2018
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Mar 6, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Oct 2, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Sep 3, 2017
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Jun 24, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Mar 17, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Jan 19, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Aug 25, 2016
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Jul 6, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Jun 27, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest May 6, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Apr 24, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Apr 23, 2016
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Apr 12, 2016
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Feb 6, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Jan 22, 2016
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Dec 22, 2015
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ James Malima Guest Dec 11, 2015
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Nov 3, 2015
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ James Mduma Guest Apr 27, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About