Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/mobile/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁
AckyShine

MASOMO YA MISA, JUMAPILI, JULAI 2, 2023: DOMINIKA LA 13 LA MWAKA

Featured Image

MWANZO

Zab. 47:2

Enyi watu wote, pigeni makofi, mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe.

SOMO 1 

2 Fal 4:8-11,14-16

Ilikuwa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; nave akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula.

Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu w’a Mungu. Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.

Ikawa siku moja akafikia huko, akaingia katika chumba kile akalala. Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee. Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni. Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI 

Zab. 89 : 1-2, 15-18 (K) 1(K)

Fadhili za Bwana nitaziimba milele. Fadhili za Bwana nitaziimba milele; Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako. Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)

Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, Ee Bwana, kuenenda katika nuru ya uso wako. Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)

Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe, Na kwa radhi yako pern be yetu itatukuka.

Maana ngao yetu ina Bwana,Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. (K)

SOMO 2 

Rum. 6:3-4,8-11

Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katikawafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO 

Mt. 11:25

Aleluya, aleluya, 
Nakushukuru, Baba, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. 
Aleluya.


INJILI 

Mt. 10:37-42


Yesu aliwafundisha mitume wake hivi: Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.

Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeave nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki.

Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia. haitampotea kamwe thawabu yake.

Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Robert Ndunguru (Guest) on July 17, 2024

Nguvu hutoka kwa Bwana

Andrew Mahiga (Guest) on May 9, 2024

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

David Sokoine (Guest) on May 8, 2024

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Betty Kimaro (Guest) on April 19, 2024

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

John Kamande (Guest) on April 6, 2024

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Nancy Kabura (Guest) on March 24, 2024

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Rose Waithera (Guest) on March 22, 2024

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Michael Onyango (Guest) on January 28, 2024

Rehema zake hudumu milele

Edward Chepkoech (Guest) on December 17, 2023

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Monica Lissu (Guest) on October 20, 2023

Katika imani, yote yanawezekana

Tabitha Okumu (Guest) on December 12, 2022

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

John Lissu (Guest) on October 12, 2022

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

John Malisa (Guest) on April 2, 2022

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Josephine Nekesa (Guest) on March 19, 2022

Nakuombea 🙏

Andrew Odhiambo (Guest) on March 16, 2022

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Victor Kimario (Guest) on February 24, 2022

Neema ya Mungu inatosha kwako

Bernard Oduor (Guest) on September 24, 2021

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Elizabeth Mrope (Guest) on March 1, 2021

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

John Mwangi (Guest) on January 27, 2021

Dumu katika Bwana.

Benjamin Masanja (Guest) on January 12, 2021

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Joseph Njoroge (Guest) on October 9, 2020

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Joseph Njoroge (Guest) on April 6, 2020

Mwamini Bwana; anajua njia

Alex Nakitare (Guest) on October 8, 2019

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Miriam Mchome (Guest) on September 16, 2019

Rehema hushinda hukumu

Alice Mrema (Guest) on September 14, 2019

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Charles Mboje (Guest) on June 20, 2019

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Thomas Mwakalindile (Guest) on May 5, 2019

Imani inaweza kusogeza milima

Josephine Nduta (Guest) on March 21, 2019

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Nancy Komba (Guest) on January 23, 2019

Sifa kwa Bwana!

Peter Mugendi (Guest) on December 21, 2018

Endelea kuwa na imani!

Alice Wanjiru (Guest) on May 31, 2018

Mungu ni mwema, wakati wote!

Sarah Mbise (Guest) on December 12, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Joyce Nkya (Guest) on November 11, 2017

Baraka kwako na familia yako.

Chris Okello (Guest) on October 22, 2017

Tumaini ni nanga ya roho

Jackson Makori (Guest) on October 16, 2017

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Daniel Obura (Guest) on July 9, 2017

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Francis Mrope (Guest) on June 18, 2017

Neema na amani iwe nawe.

George Tenga (Guest) on May 31, 2017

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Alice Mwikali (Guest) on February 20, 2017

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Monica Nyalandu (Guest) on February 11, 2017

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

John Malisa (Guest) on December 9, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Ruth Mtangi (Guest) on December 7, 2016

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Janet Wambura (Guest) on December 4, 2016

Mungu akubariki!

Grace Njuguna (Guest) on October 16, 2016

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Sarah Karani (Guest) on September 26, 2016

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

John Kamande (Guest) on May 28, 2016

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Joy Wacera (Guest) on April 23, 2016

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

George Tenga (Guest) on February 9, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Joy Wacera (Guest) on August 22, 2015

Mwamini katika mpango wake.

Moses Kipkemboi (Guest) on May 13, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Related Posts

MASOMO YA MISA, DOMINIKA YA 5 YA KWARESIMA, MWAKA C

MASOMO YA MISA, DOMINIKA YA 5 YA KWARESIMA, MWAKA C

SOMO 1: Isa. 43:16-21

Bwana asema hivi, yeye afanyaye njia katika bahari, na mahali pa ku... Read More

MASOMO YA MISA, JUNI 11, 2023: SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU

MASOMO YA MISA, JUNI 11, 2023: SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU

SOMO 1

MWANZO:

SOMO 1

2 Fal.... Read More

MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1

Hos. 5... Read More

MASOMO YA MISA, MEI, 28, 2023: SHEREHE YA PENTEKOSTE

MASOMO YA MISA, MEI, 28, 2023: SHEREHE YA PENTEKOSTE

SOMO 1

SOMO 1