MWANZO
Zab. 47:2
SOMO 1
2 Fal 4:8-11,14-16
Ilikuwa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; nave akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula.
Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu w’a Mungu. Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.
Ikawa siku moja akafikia huko, akaingia katika chumba kile akalala. Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee. Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni. Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 89 : 1-2, 15-18 (K) 1(K)
Fadhili za Bwana nitaziimba milele. Fadhili za Bwana nitaziimba milele; Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako. Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)
Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, Ee Bwana, kuenenda katika nuru ya uso wako. Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)
Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe, Na kwa radhi yako pern be yetu itatukuka.
Maana ngao yetu ina Bwana,Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. (K)
SOMO 2
Rum. 6:3-4,8-11
Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katikawafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.
Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Mt. 11:25
Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya.
INJILI
Mt. 10:37-42
Yesu aliwafundisha mitume wake hivi: Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.
Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeave nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki.
Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia. haitampotea kamwe thawabu yake.
Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo
Robert Ndunguru (Guest) on July 17, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
Andrew Mahiga (Guest) on May 9, 2024
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
David Sokoine (Guest) on May 8, 2024
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Betty Kimaro (Guest) on April 19, 2024
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
John Kamande (Guest) on April 6, 2024
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Nancy Kabura (Guest) on March 24, 2024
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rose Waithera (Guest) on March 22, 2024
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Michael Onyango (Guest) on January 28, 2024
Rehema zake hudumu milele
Edward Chepkoech (Guest) on December 17, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Monica Lissu (Guest) on October 20, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
Tabitha Okumu (Guest) on December 12, 2022
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
John Lissu (Guest) on October 12, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
John Malisa (Guest) on April 2, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Josephine Nekesa (Guest) on March 19, 2022
Nakuombea 🙏
Andrew Odhiambo (Guest) on March 16, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Victor Kimario (Guest) on February 24, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
Bernard Oduor (Guest) on September 24, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Elizabeth Mrope (Guest) on March 1, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
John Mwangi (Guest) on January 27, 2021
Dumu katika Bwana.
Benjamin Masanja (Guest) on January 12, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Joseph Njoroge (Guest) on October 9, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Joseph Njoroge (Guest) on April 6, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
Alex Nakitare (Guest) on October 8, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Miriam Mchome (Guest) on September 16, 2019
Rehema hushinda hukumu
Alice Mrema (Guest) on September 14, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Charles Mboje (Guest) on June 20, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Thomas Mwakalindile (Guest) on May 5, 2019
Imani inaweza kusogeza milima
Josephine Nduta (Guest) on March 21, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Nancy Komba (Guest) on January 23, 2019
Sifa kwa Bwana!
Peter Mugendi (Guest) on December 21, 2018
Endelea kuwa na imani!
Alice Wanjiru (Guest) on May 31, 2018
Mungu ni mwema, wakati wote!
Sarah Mbise (Guest) on December 12, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Joyce Nkya (Guest) on November 11, 2017
Baraka kwako na familia yako.
Chris Okello (Guest) on October 22, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
Jackson Makori (Guest) on October 16, 2017
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Daniel Obura (Guest) on July 9, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Francis Mrope (Guest) on June 18, 2017
Neema na amani iwe nawe.
George Tenga (Guest) on May 31, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Alice Mwikali (Guest) on February 20, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Monica Nyalandu (Guest) on February 11, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
John Malisa (Guest) on December 9, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Ruth Mtangi (Guest) on December 7, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Janet Wambura (Guest) on December 4, 2016
Mungu akubariki!
Grace Njuguna (Guest) on October 16, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Sarah Karani (Guest) on September 26, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
John Kamande (Guest) on May 28, 2016
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Joy Wacera (Guest) on April 23, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
George Tenga (Guest) on February 9, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Joy Wacera (Guest) on August 22, 2015
Mwamini katika mpango wake.
Moses Kipkemboi (Guest) on May 13, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi