Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, MEI 24, 2023: JUMATANO YA 7 YA PASAKA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Mdo 20 : 28-38

Paulo aliwaambia wakuu wa kanisa ya Efeso: Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe. Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwamwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi; tena katika ninyi wenyewe watainuka watu, wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao. Kwa hiyo kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi. Basi, sasa nawaweka katika mikono ya Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliotakaswa. Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu. Ninyi wenyewe mnajua ya kuwa mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami. Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea. Alipokwisha kunena haya akapiga magoti, akaomba pamoja nao wote. Wakalia sana wote, wakamwangukia Paulo shingoni, wakambusu-busu, wakihuzunika zaidi kwa sababu ya neno lile alilosema, ya kwamba hawatamwona uso tena. Wakamsindikiza hata merikebuni.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 68:28-29, 32-35 (K) 32

(K) Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu.
Au: Aleluya.

Ee Mungu, uziamuru nguvu zako;
Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu
Wafalme watakuletea hedaya. (K)

Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,
Msifuni Bwana kwa nyimbo.
Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele;
Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
Mhesabieni Mungu nguvu; (K)

Enzi yake i juu ya Israeli;
Na nguvu zake zi mawinguni.
Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako.
Ndiye Mungu wa Israeli;
Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo.
Na ahimidiwe Mungu. (K)

SHANGILIO

Yn. 14 : 26

Aleluya, aleluya,
Roho Mtakatifu atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Aleluya.

INJILI

Yn. 17:11-19

Siku ile, Yesu alisali akisema: Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.

Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao. Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.

Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu. Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu. Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni. Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristu.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest May 24, 2024
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ James Mduma Guest May 16, 2024
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Nov 30, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Nov 29, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Nov 18, 2023
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ John Lissu Guest Oct 24, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Jul 19, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest May 15, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest May 2, 2023
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Diana Mumbua Guest Apr 23, 2023
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Apr 18, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Dec 6, 2022
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Dec 3, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Jun 9, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Jun 1, 2022
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest May 12, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Nov 26, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Nov 12, 2021
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ John Mushi Guest Jun 11, 2021
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Apr 28, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Mar 18, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ David Chacha Guest Jun 30, 2020
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Chris Okello Guest May 24, 2020
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest May 10, 2020
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Apr 4, 2020
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Nov 11, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Sep 12, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Sep 9, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Jul 7, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Jun 16, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Feb 18, 2019
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Dec 26, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Dec 20, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Dec 8, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Nov 9, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Jan 16, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jan 14, 2018
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Jan 5, 2018
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Nov 1, 2017
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Apr 20, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Mar 11, 2017
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ John Lissu Guest Oct 31, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ John Malisa Guest Sep 28, 2016
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Aug 17, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Mar 28, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Mar 20, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Peter Mwambui Guest Dec 23, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Sep 14, 2015
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Jul 3, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest May 26, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About