Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

JUMAPILI YA 19 YA MWAKA A: MASOMO YA MISA AGOSTI 13, 2023

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Somo la Kwanza

1Fal 19:9, 11-13

Eliya alifika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia. Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunjavunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi: na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.

Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi vake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango.

NENO LA BWANA.......

Wimbo wa Katikati

Zab 85:8-13

Nisikie atakavyosema Mungu Bwana,
Maana atawambia watu wake amani.
Hakika wokovu wake u karibu na wamchao,
Utukufu ukae katika nchi yetu.

(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.

Fadhili na kweli zimekutana,
Haki na amani zimebusiana.
Kweli imechipuka katika nchi,
Haki imechungulia kutoka mbinguni.

(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.

Naam, Bwana atatoa kilicho chema,
Na nchi yetu itatoa mazao yake.
Haki itakwenda mbelc zake,
Nayo itazifanya hatua zake kuwa njia.

(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.

Somo la Pili

Rum 9:1-5

Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu, ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.

Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili; ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake; ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili.

Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.

NENO LA BWANA.....

Shangilio

Lk 19:38

Aleluya, aleluya,
Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana;
Aleluya.

Somo la Injili

Mt 14:22-33

Yesu aliwalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng'ambe. wakati yeye alipokuwa akiwaaga makutano. Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.

Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho. Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea. akienda kwa miguu juu ya bahari.

Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli, wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu akanena, akawaambia, Jipeni movo; ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo.

Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe akisema, Bwana, niokoe.

Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? Nao walipopanda chomboni, upepo ulikoma. Nao waliokuwamo ndani ya chombo wakamsujudia wakisema, Hakika wewe ni Mwana wa Mungu.

NENO LA BWANA..........

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jun 9, 2024
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest May 25, 2024
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest May 22, 2024
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest May 15, 2024
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Dec 15, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Oct 20, 2023
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ James Kimani Guest Oct 18, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Oct 4, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Sep 21, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Jul 24, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Samuel Were Guest May 26, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Feb 27, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Dec 14, 2022
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Oct 13, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Aug 24, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Feb 3, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Dec 16, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Nov 2, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest Jun 13, 2021
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Josephine Nduta Guest Apr 8, 2021
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Jan 12, 2021
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Jul 18, 2020
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Dec 8, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ George Mallya Guest Aug 22, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Jul 16, 2019
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Jun 18, 2019
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest May 14, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Jan 6, 2019
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ John Kamande Guest Dec 28, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ John Lissu Guest Sep 13, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Jun 5, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Francis Mtangi Guest Apr 17, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Apr 9, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Dec 2, 2017
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Oct 6, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Sep 15, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Aug 12, 2017
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Aug 8, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest May 17, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ John Kamande Guest Apr 15, 2017
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Mar 8, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Oct 23, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Martin Otieno Guest Sep 26, 2016
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest Aug 17, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ David Nyerere Guest May 15, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest Apr 6, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Jan 9, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Nov 21, 2015
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Janet Wambura Guest Oct 28, 2015
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Sep 25, 2015
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About