Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

MASOMO YA MISA, DOMINIKA YA 4 YA KWARESIMA, MARCHI 27, 2022

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1: Yos. 5:9a, 10-12

Bwana akamwambia Yoshua, Siku hii ya leo nimeivingirisha hiyo aibu ya Misri iondoke juu yenu.

Basi wana wa Israeli wakapanga hema zao huko Gilgali; nao wakala sikukuu ya pasaka siku ya kumi ya nne ya mwezi, jioni, katika nchi tambarare za Yeriko. Nao wakala katika mazao ya nchi siku ya pili ya kuiandama hiyo sikukuu ya pasaka, mikate isiyotiwa chachu, na bisi, siku iyo hiyo.

Ndipo ile mana ikakoma siku ya pili yake, baada ya wao kuyala hayo mazao ya nchi; na hao wana wa Israeli hawakuwa na mana tena; lakini wakala katika viliwa vya nchi ya Kanaani mwaka huo.

WIMBO WA KATIKATI: Zab. 34:1-6 (K) 8

(K) Onjeni muone ya kuwa Bwana yu mwema.

Nitamhimidi Bwana kila wakati,

Sifa zake kinywani mwangu daima.

Katika Bwana nafsi yangu itajisifu,

Wanyenyekevu wasikie wakafurahi. (K)

Mtukuzeni Bwana pamoja nami,

Na tuliadhimishe jina lake pamoja.

Nalimtafuta Bwana akanijibu,

Akaniponya na hofu zangu zote. (K)

Wakamwelekea macho wakatiwa nuru,

Wala nyuso zao hazitaona haya.

Maskini huyu aliita, Bwana akasikia,

Akamwokoa na taabu zake zote. (K)

SOMO 2: 2 Kor. 5:17-21

Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya. Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho; yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho. Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu. Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.

SHANGILIO: Lk. 15:18

Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.

INJILI: Lk. 15:1-3, 11-32

Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize. Mafarisayo na waandishi wakanung’unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao. Akawaambia mfano huu, akisema.

Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake. Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.

Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. Akaondoka, akaenda kwa babaye.

Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; mleteeni ndama yule aliyenona mkamchinje nje; nasi tule na kufurahi; kw akuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.

Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo. Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini? Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. Akakasirika, akakataa kuingia ndani.

Basi babaye alitoka nje, akamsihi. Akamjibu baba yake, akasema. Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wowote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu; lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.

Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami siku zote, na vyote nilivyo navyo ni vyako. Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.

Neno la Bwana...sifa kwako Ee Kristo

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Joy Wacera Guest Jul 8, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Esther Nyambura Guest Apr 23, 2024
Sifa kwa Bwana!
👥 Elizabeth Mrope Guest Apr 23, 2024
Mwamini katika mpango wake.
👥 Hellen Nduta Guest Feb 9, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Kevin Maina Guest Jun 16, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Ruth Wanjiku Guest Feb 4, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Brian Karanja Guest Jan 28, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 David Sokoine Guest Jul 24, 2022
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Elizabeth Mtei Guest Jun 25, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Thomas Mwakalindile Guest May 6, 2022
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Diana Mallya Guest Oct 29, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Violet Mumo Guest Jul 30, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Samson Mahiga Guest Jul 24, 2021
Baraka kwako na familia yako.
👥 Monica Adhiambo Guest Jul 11, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 James Mduma Guest Jun 20, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 David Musyoka Guest Jun 16, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 John Malisa Guest May 27, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Dorothy Mwakalindile Guest Jan 14, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Anthony Kariuki Guest Jan 3, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Rose Lowassa Guest Nov 6, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Charles Mboje Guest Sep 6, 2020
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Peter Mwambui Guest May 8, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Francis Mrope Guest Apr 17, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Nancy Komba Guest Feb 15, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Robert Ndunguru Guest Dec 19, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Peter Mwambui Guest Sep 23, 2019
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Patrick Kidata Guest Sep 8, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Sarah Karani Guest Aug 14, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 David Chacha Guest May 20, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Victor Mwalimu Guest Feb 2, 2019
Mungu akubariki!
👥 Mary Kendi Guest Jan 20, 2019
Dumu katika Bwana.
👥 Grace Majaliwa Guest Dec 12, 2018
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 David Sokoine Guest Nov 28, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Victor Mwalimu Guest Nov 23, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Benjamin Kibicho Guest Apr 24, 2018
Rehema zake hudumu milele
👥 David Chacha Guest Feb 17, 2018
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Grace Majaliwa Guest Jul 31, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Monica Adhiambo Guest Jul 13, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Sarah Achieng Guest Feb 13, 2017
Endelea kuwa na imani!
👥 Janet Wambura Guest Feb 9, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Andrew Mchome Guest Feb 2, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 David Ochieng Guest Sep 15, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 James Kawawa Guest Jul 23, 2016
Neema na amani iwe nawe.
👥 Lydia Mutheu Guest Jul 16, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Alex Nyamweya Guest Jun 15, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Robert Okello Guest Jan 12, 2016
Nakuombea 🙏
👥 Margaret Anyango Guest Nov 11, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Faith Kariuki Guest Sep 30, 2015
Rehema hushinda hukumu
👥 George Mallya Guest Apr 19, 2015
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Irene Makena Guest Apr 17, 2015
Tumaini ni nanga ya roho

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About