Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, MACHI 18, 2022: IJUMAA, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Mwa. 37:3-4, 12-13, 17-28

ย 

Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote, maana ni mwana wa uzee wake, akamfanyia kanzu ndefu. Ndugu zake wakaona ya kuwa baba yao anampenda kuliko ndugu zake wote, wakamchukia, na hawakuweza kusema naye kwa amani.

Ndugu zake wakaenda kuchunga kondoo za baba yao huko Shekemu. Israeli akamwambia Yusufu, Je! Ndugu zako hawachungi kondoo katika Shekemu? Njoo, nikutume kwao.

Basi Yusufu akawafuata ndugu zake akawakuta huko Dothani. Wakamwona toka mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shuri juu yake ili wamwue. Wakasemezana wao kwa wao, Tazama, yule bwana wa ndoto anakuja. Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake. Reubeni akasikia akamwokoa katika mikono yao, akasema, Tusimwue. Reubeni akawaambia, Msimwage damu; mtupeni katika birika iliyopo nyikani, wala msimguse; ili apate kumwokoa katika mikono yao, akamrudishe kwa baba yake. Ikawa Yusufu alipofika kwa ndugu zake, wakamvua Yusufu kanzu yake, kanzu ile ndefu aliyoivaa, wakamtwaa wakamtupa katika birika; na hiyo birika ilikuwa tupu, hamna maji. Nao wakakaa kitako kula chakula.

Wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na zeri na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri. Yuda akawaambia ndugu zake, Kwafaa nini kumwua ndugu yetu, na kuificha damu yake? haya, na tumwuze kwa hawa Waishmaeli, wala mikono yenu isimdhuru, maana yeye ni ndugu yetu, na damu yetu. Ndugu zake wakakubali.

Wakapita wafanyabiashara Wamidiani; basi wakamtoa Yusufu, wakampandisha kumtoa katika birika wakamwuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande vya fedha ishirini; nao wakamchukua Yusufu mpaka Misri.

ย 

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

ย 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 105:16-21 (K) 5

ย 

(K) Zikumbukeni ajabu zake Bwana alizozifanya.

ย 

Akaiita njaa iijilie nchi,

Akakiharibu chakula chote walichokitegemea.

Alimpeleka mtu mbele yao,

Yusufu utumwani. (K)

ย 

Walimwumiza miguu yake kwa pingu,

Akatiwa katika minyororo ya chuma.

Hata wakati wa kuwadia neno lake,

Ahadi ya Bwana ilimjaribu. (K)

ย 

Mfalme alituma watu akamfungua,

Mkuu wa watu akamwachia.

Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake,

Na mwenye amri juu ya mali zake zote. (K)

ย 

SHANGILIO

Yn. 3:16

ย 

Jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee; Kila mtu amwaminiye huwa na uzima wa milele.

ย 

INJILI

Mt. 21:33-43; 45-46

ย 

Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee wa watu, Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu mwenye nyumba, naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri. Wakati wa matunda ulipokuwa karibu, akawatuma watumwa wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake. Wale wakulima wakawakamata watumwa wake, huyu wakampiga, na huyu wakamwua, na huyu wakampiga kwa mawe. Akawatuma tena watumwa wengine wengi kuliko wa kwanza, wakawatenda vile vile.

Mwishowe akamtuma mwanawe kwao, akisema, Watamstahi mwanangu. Lakini wale wakulima walipomwona yule mwana, wakasemezana wao kwa wao, Huyu ni mrithi; haya na tumwue, tuutwae urithi wake. Wakamkamata, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi atakapokuja yule bwana wa shamba la mizabibu, atawatendaje wale wakulima? Wakamwambia, Ataangamiza vibaya wale wabaya; na shamba la mizabibu atawapangisha wakulima wengine, watakaomlipa matunda kwa wakati wake.

Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; neno hili limetoka kwa Bwana, nalo ni ajabu machoni petu? Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa, linguine lenye kuzaa matunda yake.

Wakuu wa makuhani na Mafarisayo, waliposikia mifano yake, walitambua ya kuwa anawanenea wao. Nao walipotafuta kumkamata waliogopa makutano, kwa maana wao walimwona kuwa nabii.

ย 

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

ย 

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Irene Makena Guest Jan 19, 2024
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kikwete Guest Dec 30, 2023
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Sep 22, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Thomas Mtaki Guest Sep 12, 2023
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Carol Nyakio Guest Jul 24, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ James Kawawa Guest Jul 9, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Mary Njeri Guest Jun 24, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Mary Sokoine Guest May 25, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Stephen Malecela Guest May 25, 2023
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest May 14, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Mwakalindile Guest May 10, 2023
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Francis Mtangi Guest May 1, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Dec 3, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Grace Minja Guest Aug 28, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Nora Lowassa Guest Aug 12, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Simon Kiprono Guest Jul 7, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Jun 14, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Jackson Makori Guest Apr 2, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Edith Cherotich Guest Sep 28, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Mary Kendi Guest Sep 20, 2020
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kiwanga Guest Sep 3, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Janet Wambura Guest Apr 19, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Richard Mulwa Guest Mar 26, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Grace Mligo Guest Feb 29, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Jackson Makori Guest Oct 3, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Agnes Sumaye Guest Oct 3, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Jun 29, 2019
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Apr 29, 2019
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Anthony Kariuki Guest Apr 12, 2019
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Thomas Mtaki Guest Dec 7, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Alice Mrema Guest Aug 3, 2018
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Anna Mahiga Guest Jul 20, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ James Kimani Guest Jun 1, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Peter Tibaijuka Guest Jun 1, 2018
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Edward Chepkoech Guest Jan 3, 2018
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Janet Mwikali Guest Aug 13, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Edwin Ndambuki Guest Feb 4, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mahiga Guest Nov 8, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Betty Kimaro Guest Sep 8, 2016
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Kevin Maina Guest Jun 17, 2016
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Grace Njuguna Guest Apr 17, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ John Mwangi Guest Feb 13, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Victor Kamau Guest Feb 1, 2016
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Janet Wambura Guest Nov 23, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Oct 10, 2015
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Betty Kimaro Guest Sep 16, 2015
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Sarah Achieng Guest Aug 28, 2015
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Sarah Karani Guest Aug 24, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Peter Tibaijuka Guest Aug 24, 2015
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Edward Chepkoech Guest Jul 1, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About