Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

MASOMO YA MISA, MACHI 28, 2022: JUMATATU: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Isa. 65:17-21

 

Bwana asema: Tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.

Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza. Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa. Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.

 

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 30:1, 3-5, 10-12 (K) 1

 

(K) Nitakutukuza, ee Bwana, kwa maana umeniinua.

 

Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua,

Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.

Umeniinua nafsi yangu,

Ee Bwana, kutoka kuzimu.

Umenihuisha na kunitoa

Miongoni mwao washukao shimoni. (K)

 

Mwimbieni Bwana zaburi,

Enyi watauwa wake.

Na kufanya shukrani.

Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.

Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo,

Katika radhi yake mna uhai.

Huenda kilio huja kukaa usiku,

Lakini asubuhi huwa furaha. (K)

 

Ee Bwana, usikie, unirehemu,

Bwana, uwe msaidizi wangu.

Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;

Ulinivua gunia, ukanivika furaha.

Ee Bwana, mungu wangu,

Nitakushukuru milele. (K)

 

SHANGILIO

Eze. 33:11

 

Sikufurahii kufa kwake mtu mwovu, asema Bwana, bali aiache njia yake mbaya, akaishi.

 

INJILI

Yn. 4:43-54

 

Baada ya siku mbili hizo Yesu aliondoka huko, akaenda Galilaya. Kwa maana Yesu mwenyewe alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe. Basi alipofika Galilaya, Wagalilaya walimpokea; kwa kuwa wameyaona mambo yote aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu; maana hao nao waliiendea sikukuu.

Basi alifika tena Kana ya Galilaya, hapo alipoyafanya yale maji kuwa divai. Na palikuwa na diwani mmoja ambaye mwanawe hawezi huko Kapernaumu. Huyo aliposikia ya kwamba Yesu amekuja kutoka Uyahudi mpaka Galilaya, alimwendea, akamsihi ashuke na kumponya mwanawe; kwa maana alikuwa kufani. Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa? Yule diwani akamwambia, Bwana, ushuke asijakufa mtoto wangu. Yesu akamwambia, Enenda; mwanao yu hai. Mtu yule akalisadiki lile neno aliloambiwa na Yesu, naye akashika njia. Hata alipokuwa akishuka, watumwa wake walimlaki, wakisema ya kwamba mtoto wake yu hai. Basi akawauliza habari ya saa alipoanza kuwa hajambo; nao wakamwambia, jana, saa saba, homa ilimwacha. Basi babaye akafahamu ya kuwa ni saa ile ile alipoambiwa na Yesu, Mwanao yu hai. Akaamini yeye na wote wa nyumbani mwake.

Hiyo ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu, alipokuwa ametoka Uyahudi kufika Galilaya.

 

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Edward Chepkoech Guest May 23, 2024
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Janet Mwikali Guest Apr 18, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Betty Akinyi Guest Oct 8, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 David Kawawa Guest Sep 9, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Mary Mrope Guest Jun 5, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Francis Mrope Guest May 17, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Grace Njuguna Guest May 8, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Lucy Mushi Guest Nov 30, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Benjamin Masanja Guest Aug 3, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Diana Mallya Guest Jul 18, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 David Chacha Guest May 10, 2022
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Charles Wafula Guest Mar 17, 2022
Mungu akubariki!
👥 Simon Kiprono Guest Mar 6, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
👥 David Kawawa Guest Mar 6, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Richard Mulwa Guest Feb 16, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Rose Kiwanga Guest Aug 26, 2021
Nakuombea 🙏
👥 Lydia Wanyama Guest Oct 27, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Sharon Kibiru Guest Jun 24, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Kenneth Murithi Guest Jun 7, 2020
Rehema zake hudumu milele
👥 Jane Malecela Guest May 9, 2020
Baraka kwako na familia yako.
👥 Edwin Ndambuki Guest Jan 31, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Charles Mrope Guest Oct 26, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Faith Kariuki Guest Aug 31, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Nora Kidata Guest Mar 13, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Isaac Kiptoo Guest Feb 9, 2019
Endelea kuwa na imani!
👥 Lydia Wanyama Guest Nov 13, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Stephen Amollo Guest Oct 5, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Kenneth Murithi Guest Aug 28, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 James Kimani Guest Aug 10, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Andrew Mchome Guest Jul 15, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 John Mushi Guest Jun 27, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Alice Jebet Guest Apr 16, 2018
Mwamini katika mpango wake.
👥 David Sokoine Guest Mar 9, 2018
Dumu katika Bwana.
👥 James Kawawa Guest Feb 11, 2018
Rehema hushinda hukumu
👥 David Nyerere Guest Jan 4, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Raphael Okoth Guest Dec 26, 2017
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Alex Nyamweya Guest Oct 12, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 George Tenga Guest Jun 6, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Jacob Kiplangat Guest May 18, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Mary Njeri Guest Apr 17, 2017
Neema na amani iwe nawe.
👥 Josephine Nekesa Guest Jan 1, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Charles Mchome Guest May 29, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Paul Ndomba Guest Apr 11, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Jacob Kiplangat Guest Feb 17, 2016
Sifa kwa Bwana!
👥 Joyce Mussa Guest Dec 31, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Paul Kamau Guest Dec 1, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Ann Awino Guest Nov 6, 2015
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Stephen Kangethe Guest Sep 30, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Alex Nyamweya Guest Sep 15, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Joy Wacera Guest Jun 16, 2015
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About