Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Maswali na Majibu kuhusu Karama

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Je, karama ni zile za kushangaza tu?
Hapana, karama si zile za kushangaza tu, tena zile muhimu zaidi si hizo, bali zile zinazojenga zaidi Kanisa, kama zile za uongozi:
“Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha” (1Kor 12:28).
“Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema tuliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia, kwa bidii; mwenye kurehemu, kwa furaha” (Rom 12:6-8).

Karama nyingine muhimu zinatuwezesha kufanya nini?
Karama nyingine muhimu zinatuwezesha kuishi kwa useja kama Yesu na Paulo, au kwa ndoa:
“Nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi. Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane; ni heri wakae kama mimi nilivyo” (1Kor 7:7-8).
“Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa” (Math 19:11).
Tunavyoona katika historia ya watawa, mara nyingi karama ya useja inaendana na nyingine katika maisha ya sala, ya kijumuia na ya kitume. Hivyo Filipo “alikuwa na binti wanne, mabikira, waliokuwa wakitabiri” (Mdo 21:9).

Karama zinagawiwa vipi?
Karama zinagawiwa na Roho Mtakatifu jinsi anavyotaka, si kwa sifa au faida ya binafsi, bali kwa ustawi wa taifa la Mungu.
“Kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye… Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza? Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?… Kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa… Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani” (1Kor 12:11,29-30; 14:12,33). Kwa ajili hiyo mitume walipambanua na kuratibu karama katika ibada na katika maisha ya jumuia zisije zikavuruga Kanisa.

Karama za kushangaza zina hatari gani?
Karama za kushangaza zina hatari mbalimbali, hasa zikitiwa maanani mno. Hapo ni rahisi zilete majivuno, kijicho na mafarakano.
“Ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je, si watu wa tabia ya mwili ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?… Mmekwisha kushiba, mmekwisha kupata utajiri, mmemiliki pasipo sisi. Naam, laiti mngemiliki… Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke” (1Kor 3:3; 4:8; 10:12).
Katika mambo yasiyothibitika ni rahisi kudanganyika kuwa yametoka kwa Mungu, kumbe sivyo. Kisha kudanganyika ni vigumu kuachana nayo hata yakiwa na madhara kwa mhusika au kwa Kanisa.
“Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani” (1Yoh 4:1).

Tunda la kuongozwa na Roho Mtakatifu ni lipi?
Tunda la kuongozwa na Roho Mtakatifu ni umoja wa Kanisa unaotokana na ustawi wa upendo na vipaji ndani ya waamini.
“Wote walijaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja” (Mdo 4:31-32).
“Tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria” (Gal 5:22-23).
“Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. Maana hapo palipo wivu na ugomvi, ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi; tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki” (Yak 3:14-17).
Madhehebu yanapozidi kufarakana ni lazima tujiulize kama kweli ni kazi ya Roho Mtakatifu.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Elijah Mutua Guest Jun 12, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Anna Kibwana Guest Mar 16, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Nora Lowassa Guest Mar 6, 2024
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Paul Ndomba Guest Sep 5, 2023
Baraka kwako na familia yako.
👥 Stephen Amollo Guest Apr 23, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Patrick Akech Guest Mar 1, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Moses Kipkemboi Guest Nov 11, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Nicholas Wanjohi Guest Jul 1, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Catherine Mkumbo Guest Jun 22, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Betty Cheruiyot Guest Mar 27, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 George Wanjala Guest Nov 25, 2021
Mwamini katika mpango wake.
👥 David Ochieng Guest Apr 21, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Joyce Mussa Guest Apr 4, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Joseph Kiwanga Guest Jan 23, 2021
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Elijah Mutua Guest Jan 20, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Irene Akoth Guest Aug 7, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Stephen Malecela Guest May 3, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Dorothy Nkya Guest Apr 10, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Joseph Mallya Guest Dec 18, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Joseph Mallya Guest Dec 16, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 David Musyoka Guest Aug 9, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Frank Sokoine Guest Aug 7, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 James Kawawa Guest Jul 6, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Edward Chepkoech Guest Jun 29, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Lydia Mzindakaya Guest Jun 17, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 David Ochieng Guest Jan 29, 2019
Endelea kuwa na imani!
👥 Alex Nyamweya Guest Dec 31, 2018
Neema na amani iwe nawe.
👥 Violet Mumo Guest Aug 26, 2018
Mungu akubariki!
👥 Rose Amukowa Guest Jun 4, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Sarah Mbise Guest Apr 15, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Joseph Kitine Guest Apr 11, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Alice Jebet Guest Apr 10, 2018
Nakuombea 🙏
👥 Jane Malecela Guest Feb 16, 2018
Rehema hushinda hukumu
👥 Stephen Mushi Guest Nov 4, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Patrick Akech Guest Aug 8, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Nancy Kawawa Guest Aug 5, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Isaac Kiptoo Guest Apr 14, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Samson Tibaijuka Guest Mar 25, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Elizabeth Mrope Guest Nov 28, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Nancy Kawawa Guest Nov 14, 2016
Dumu katika Bwana.
👥 Faith Kariuki Guest Apr 25, 2016
Sifa kwa Bwana!
👥 George Wanjala Guest Apr 1, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 John Lissu Guest Feb 14, 2016
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Henry Mollel Guest Jan 14, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Victor Malima Guest Nov 18, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Ruth Kibona Guest Nov 6, 2015
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Betty Kimaro Guest Jul 3, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Frank Sokoine Guest Jun 8, 2015
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Catherine Naliaka Guest May 16, 2015
Rehema zake hudumu milele
👥 Janet Wambura Guest Apr 21, 2015
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About