Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Mambo ya Msingi kufahamu kuhusu Ndoa ya Kikatoliki

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Daraja na ndoa ni tofauti na sakramenti nyingine kwa sababu gani?
Daraja na ndoa ni tofauti na sakramenti nyingine kwa sababu hazilengi hasa faida ya mtu anayezipokea, bali huduma zake kwa ajili ya Kanisa na jamii. Daraja inatia uwezo wa Kristo kwa ustawi wa Kanisa, Bibi arusi wake. Ndoa inatia upendo wake mwaminifu kwa ustawi wa familia, kanisa dogo la nyumbani.
“Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe” (Mdo 20:28).
“Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake popote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa” (Ef 5:29-32).

Kadiri ya mpango wa Muumba, ndoa halisi ina sifa ngapi?
Kadiri ya mpango wa Muumba, ndoa halisi ina sifa tatu: umoja, uimara na utayari wa kuzaa.
“Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, ‘Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja?’ Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe” (Math 19:4-6).
“Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, ‘Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha’” (Mwa 1:28).
Mitara, uzinifu, talaka, ushoga na kukataa uzazi ni kinyume cha mpango huo.

Yesu aliweka sakramenti ya ndoa kwa sababu gani?
Yesu aliweka sakramenti ya ndoa kwa sababu ya umuhimu wa familia kwa ustawi wa mume na mke, watoto, jamii na ufalme wa Mungu, na kwa sababu ya uzito wa majukumu yanayohusika.
“Siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwepo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake” (Yoh 2:1-2), akaleta divai bora ya ndoa sakramenti badala ya ndoa ya kimaumbile.
Hivyo ametuandalia neema tuweze kushinda “ugumu wa mioyo” (Math 19:8) unaohatarisha daima uzuri wa mpango wa Mungu kuhusu upendo mwaminifu katika ndoa. “Mungu aliona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana” (Mwa 1:31).

Ndoa ya Wakristo ni sakramenti ya nani?
Ndoa ya Wakristo ni sakramenti ya Yesu na Kanisa lake.
“Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi arusi, mke wa Mwanakondoo” (Ufu 21:9).
Wakiwa na ndoa halisi, mume na mke waliobatizwa ni ishara wazi ya hao wanaarusi wawili wasioonekana.
“Kama vile Kanisa limtiivyo Kristo, vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake” (Ef 5:24-25).
Ndiyo sababu Mkatoliki hawezi kufunga ndoa bila ya kuhusisha Kanisa na kufuata taratibu zake.

Ni zipi Sakramenti za Huduma ya ushirika na utume?
Ni Sakramenti mbili ambazo ni Sakramenti ya Daraja na Sakramenti ya Ndoa

Sakramenti ya ndoa ni nini?
Sakramenti ya ndoa ndio yenye kuwaunganisha wakristo wawili mume namke waliopendana kwa hiari bila shuruti au vitisho au kizuizi kwa kuwapa neema ya kuishi pamoja kitakatifu wakiwalea watoto wao katika utakatifu

Je, ndoa halali yaweza kuvunjwa?
Sakramenti ya ndoa iliyofungwa kihalali hudumu milele kwani Yesu anafundisha kuwa "Alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe" (Mt 19:6)

Ndoa imewekwa na nani?
Ndoa imewekwa na Mungu mwenyewe na Yesu Kristo ameeinua na kuifanya Sakramenti. (Mwz 2:18; Mt 19:1-12)

Kabla ya kupokea Sakramenti ya Ndoa hutakiwa nini?
Kabla ya kupokea Sakramenti ya Ndoa hutakiwa; 1. Uhuru wa kila mmoja 2. Matangazo ya ndoa 3. Wachumba wawe na nia ya kweli ya kuoana
4. Mafundisho na semina ya ndoa 5. Wasiwe na kizuizi chochote cha ndoa 6. Wasikae suria na wapokee Sakramenti ya Kitubio

Mtu aweza kupokea Sakramenti ya ndoa zaidi ya mara moja?
Ndiyo, mwenzi akifa yule aliyebaki yupo huru kufunga ndoa tena (1Kor 7:39)

Vizuizi vya ndoa ni kitu gani?
Vizuizi vya ndoa ni vile vinavyofanya ndoa isiwe halali tangu mwanzo

Vizuizi vya ndoa ni vipi?
Vizuizi vya ndoa ni; 1. Upungufu wa umri 2. Uhanithi 3. Ndoa awali halali 4. Tofauti za dini au upagani
5. Daraja Takatifu 6. Nadhiri 7. Utekaji au kutumia nguvu 8. Taksiri au Jinai au Mauaji ya mwenzi wa ndoa 9. Uhusiano wa damu 10. Uhusiano wa ndoa 11. Ugoni au uhawara 12. Kuasili mtoto au Uhusiano wa kisheria

Ndoa mchanganyiko maana yake ni nini?
Ndoa mchanganyiko ni ndoa kati ya Mkristo Mkatoliki na Mkristo asiye Mkatoliki

Ndoa ya utofauti wa Imani maana yake ni nini?
Ndoa ya utofauti wa Imani ni ndoa kati ya Mkristo Mkatoliki na mtu ambaye hajabatizwa kwa mfano Mpagani, Mwislamu, Yehova, Mlokole tangu kuzaliwa n.k

Mkristo Mkatoliki awezaje kufunga ndoa mchanganyiko au utofauti wa dini kwa uhalali?
Aweza kufunga ndoa hiyo kwa uhalali baada ya kupata ruhusa maalumu ya Askofu kwa Barua.

Ili Askofu atoe ruhusa ya kufungisha ndoa ya mchanganyiko au dini tofauti kuna Masharti gani?
Ndiyo, Askofu atatoa ruhusa baada ya Mkristo Mkatoliki kuahidi kwamba;
1. Atabaki Imani Katoliki mpaka kufa na isiwe amedanganya 2. Watoto wote watabatizwa na kulelewa katika Kanisa Katoliki 3. Huyo anayefunga naye ndoa akubali bila masharti yoyote

Je, Mchumba Mkatoliki aweza kuiacha Imani yake kwa sababu ya Ndoa?
Hapana, Kwa kuwa Kanisa Katoliki limeasisiwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo kama la lazima kwa kupata wokovu, wanaokataa kuingia au kuhudumu ndani yake hawawezi kuokolewa.

Kuna kosa gani kama mmoja wapo atakuwa amedanganya ili aruhusiwe kufunga ndoa mseto au mchanganyiko
Kama mmoja amedanganya basi ndoa hiyo ingawa imefungwa haitakuwa halali kabisa mpaka mwisho. Watadumu katika dhambi mpaka kufa au watubu.

Kanisa linatoa ushahuri gani kuhusu ndoa halali au ya mseto?
Kanisa linatambua hatari kubwa kwa Imani linashauri watoto wake wawe na busara kubwa wanapoamua kupendana kwa lengo la kufunga ndoa.

Je, ndoa halali inaweza kuvunjwa?
Hapana, Hakuna yeyote anayeweza kuvunja ndoa halali isipokuwa kifo. (Mt 19:4-6)

Anayevunja ndoa na kuoa au kuolewa anaweza kupokea Sakramenti?
Hapana, Anayevunja maagano ya ndoa na kuoa au kuolewa hawezi kupokea Sakramenti ya Ekaristi wala Kitubio hadi afanye toba na kurekebisha hali hiyo. (Mk 10:11-12)

Ni nani wahudumu wa Sakramenti ya ndoa?
Wahiudumu rasmi wa Sakramenti ya ndoa ni wachumba wenyewe, Padri kama shahidi rasmi wa kanisa. Tena ni lazima ifungwe mbele ya mashahidi wengine wawili.

Watu wa jinsia moja waweza kuoana?
Hapana, watu wa Jinsia moja hawawezi kuoana na wakifanya hinyo wanatenda dhambi kubwa inayomlilia Mungu. (Wal 18:22)
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 51

Please log in or register to comment or reply.
👥 Dorothy Majaliwa Guest Jun 21, 2024
Endelea kuwa na imani!
👥 Betty Akinyi Guest Mar 18, 2024
Mungu akubariki!
👥 Stephen Mushi Guest Jan 13, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Mary Kendi Guest Sep 18, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Christopher Oloo Guest Jul 10, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Moses Kipkemboi Guest Jul 2, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Miriam Mchome Guest Jun 29, 2023
Dumu katika Bwana.
👥 Victor Kimario Guest May 13, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Stephen Mushi Guest May 10, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Charles Wafula Guest Mar 27, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Philip Nyaga Guest Jun 4, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Patrick Kidata Guest Jun 3, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Mafundisho ya Msingi kuhusu Roho Mtakatifu - AckySHINE Guest Apr 18, 2022
[…] nyingine muhimu zinatuwezesha kuishi kwa useja kama Yesu na Paulo, au kwa ndoa: “Nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake […]
👥 John Kamande Guest Mar 29, 2022
Mwamini katika mpango wake.
👥 Grace Majaliwa Guest Jan 8, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Rose Amukowa Guest Sep 12, 2021
Neema na amani iwe nawe.
👥 Betty Kimaro Guest Aug 25, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Ruth Wanjiku Guest Jul 5, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Alice Mwikali Guest Jun 24, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Anna Mahiga Guest Jun 18, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Joseph Njoroge Guest Apr 24, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 David Musyoka Guest Apr 4, 2021
Rehema zake hudumu milele
👥 Jacob Kiplangat Guest Dec 3, 2020
Rehema hushinda hukumu
👥 John Mushi Guest Jul 29, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Frank Sokoine Guest Jul 16, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Lucy Mahiga Guest Jul 13, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Grace Wairimu Guest Jun 4, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Alice Mrema Guest Apr 4, 2020
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Monica Lissu Guest Feb 26, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Patrick Kidata Guest Jan 20, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Anna Malela Guest Dec 31, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Nora Lowassa Guest Dec 21, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Victor Malima Guest Nov 16, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Rose Waithera Guest Jun 23, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Victor Kimario Guest May 30, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Rose Lowassa Guest Nov 4, 2018
Nakuombea 🙏
👥 Peter Mwambui Guest Jun 17, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Linda Karimi Guest Nov 21, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Peter Mwambui Guest Nov 14, 2017
Baraka kwako na familia yako.
👥 Wilson Ombati Guest May 17, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Anna Malela Guest Mar 30, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Monica Nyalandu Guest Mar 24, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Monica Lissu Guest Mar 11, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Grace Mushi Guest Oct 2, 2016
Sifa kwa Bwana!
👥 Irene Akoth Guest Jul 3, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Fredrick Mutiso Guest Oct 29, 2015
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Lucy Mahiga Guest Oct 28, 2015
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Anna Mahiga Guest Sep 27, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Samson Mahiga Guest Sep 20, 2015
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Diana Mallya Guest Jul 13, 2015
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Peter Mwambui Guest Jun 14, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About