Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Maswali na majibu kuhusu Mpako wa wagonjwa au Mpako wa Mwisho

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu gani?
Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu alijua udhaifu wa binadamu hauishi mara anapopokea uzima wa Mungu kwa sakramenti tatu za kuingizwa katika Ukristo. Hivyo alipanga kusaidia mpaka mwisho wa dunia waamini wake watakaopatwa na dhambi na ugonjwa, kama alivyowasaidia wengi aliokutana nao katika maisha yake.
“Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, ‘Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako’… ‘Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi’ – amwambia yule mwenye kupooza – ‘Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako’. Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake. Makutano walipomwona, walishikwa na hofu, wakamtukuza Mungu, aliyewapa watu amri ya namna hii” (Math 9:2,6-8).

Mpako wa Wagonjwa ulianzishwa na nani?
Mpako wa Wagonjwa ulianzishwa na Yesu, kama sakramenti zote. Maandiko yanasimulia huruma yake iliyomfanya awaponye wengi kwa namna mbalimbali na kuwapa Mitume uwezo wa kufanya vilevile kwa “kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina” (Math 10:1). Nao
“wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza” (Mk 6:13).
“Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa, nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa” (Yak 5:14-15).

Mafuta ya mpako wa wagonjwa yanamaanisha nini?
Mafuta ya wagonjwa yanamaanisha lengo la kuwaponya na kuwarudishia nguvu na uzuri.
Kama kawaida, maneno yanaweka wazi zaidi kuwa lengo si kuponya mwili tu, bali hasa roho kwa kuitia msamaha na faraja katika mateso ambayo huenda yakaendelea. Kwa kuwa Mungu haponyi mwili kila mara, isipokuwa kwa faida na wokovu wa mgonjwa na wa wengine. Kama ndiyo mapenzi yake, kila mmoja ajifunze kufaidika vilevile na ugonjwa:
“Makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, ‘Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu’. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu” (2Kor 12:7-9).
“Sasa nayafurahia mateso niliyo nayo kwa ajili yenu, tena nayatimiliza katika mwili wangu yale yaliyopungua ya mateso ya Kristo, kwa ajili ya mwili wake, yaani, kanisa lake” (Kol 1:24).

Sakramenti ya Mpako wa wagonjwa ni nini?
Ni Sakramenti ambayo Padri humuombea neema ya Mungu na kumpaka Mafuta Matakatifu mgonjwa aliye katika hatari ya kifo kwa ajili ya neema ya roho na mwili. (Yak 5:14-15, Mk 6:13)
Sakramenti ya Mpako wa wagonjwa ilianza lini? Je, wakati wa Yesu kulikuwa na sakramenti hii?
Sakramenti ya mpako wa wagonjwa ilikuwepo tangu wakati Yesu akiwa hai. Tunaweza kuiona Kwenye Biblia tunaposoma Yesu alivyowatuma wanafunzi wake waliwapaka watu mafuta. "Waliwatoa pepo wengi Wabaya, wakawapaka wagonjwa wengi mafuta wakawaponya. (Marko 6:13)

Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa inaadhimishwaje?
Inaadhimishwa kwa Padre kumuombea mgonjwa, kumuwekea mikono na kumpaka mafuta katika panda la uso na viganja vya mikono; kwa kutumia mafuta aliyobariki Askofu siku ya Alhamisi kuu.

Sakramenti ya Mpako Wa Wagonjwa inamanufaa gani rohoni mwa mtu?
Manufaa ya Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa ni
1. Nguvu ya kuvumilia mateso na kuyaunganisha na mateso ya Yesu Kristo 2. Maondoleo ya dhambi zote asizoweza kuziungama 3. Nafuu ya mwili, hata uzima ikifaa kwa wokovu wa roho yake 4. Neema ya kujiandaa kuaga dunia na kuingia katika uzima wa milele

Ni nani anayetoa Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa?
Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa hutolewa na kuhani tuu yaani Askofu au Padri

Padri aitwe kwa mgonjwa lini?
Padri aitwe kwa mgonjwa mara inapoonekana Hatari ya Kifo na kamwe isisubiriwe mpaka mgonjwa apoteze fahamu.

Ni nani aweza kupokea Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa?
Ni kila Mkatoliki aliyefikia umri wa kufikiri na aliye katika hatari ya kufa kwa ugonjwa au uzee aweza kupokea Sakramenti hii.

Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa yaweza kupokelewa mara ngapi?
Sakramenti hii yaweza kupokelewa mara nyingi ugonjwa ukizidi au akipatwa na ugonjwa mwingine mkubwa

Alama wazi ya Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa ni nini?
Alama wazi ya Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa ni tendo la kupaka Mafuta Matakatifu wagonjwa na kutamka maneno
"Kwa mpako huu Mtakatifu na kwa pendo lake kuu, Bwana Akujaze na nguvu ya Roho Mtakatifu. Amina Akuondoe katika enzi ya dhambi, akuweke huru. Kwa wema wake akupe nafuu katika mateso yako na kukujalia neema. Amina"

Kama padri hatapatika na mgonjwa afanye nini?
Kama padri hatapatikana mgonjwa aweke nia ya kuungama na afanye majuto kamili

Komunyo pamba ndio nini?
Komunyo pamba ndio Ekaristi inayopokelewa na wale wanaokaribia kuaga maisha ya duniani na wanaojiandaa kuvukia uzima wa milele
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Paul Ndomba Guest Jul 1, 2024
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Jane Muthoni Guest May 3, 2024
Rehema zake hudumu milele
👥 Stephen Amollo Guest Feb 28, 2024
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Agnes Lowassa Guest Aug 16, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Stephen Malecela Guest Jul 2, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
👥 George Tenga Guest May 18, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Edward Lowassa Guest Oct 17, 2022
Mungu akubariki!
👥 Paul Kamau Guest Jul 23, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Ruth Mtangi Guest Jun 18, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Nora Lowassa Guest Apr 11, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Monica Lissu Guest Mar 19, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Grace Mushi Guest Mar 12, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Peter Mbise Guest Nov 10, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Catherine Naliaka Guest Nov 3, 2021
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Nancy Akumu Guest Aug 29, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Lydia Mutheu Guest Aug 24, 2021
Nakuombea 🙏
👥 Rose Amukowa Guest Apr 28, 2021
Rehema hushinda hukumu
👥 John Lissu Guest Dec 14, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Janet Wambura Guest Dec 9, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Charles Mboje Guest Sep 13, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Emily Chepngeno Guest Apr 8, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Peter Tibaijuka Guest Mar 6, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Paul Kamau Guest Jan 4, 2020
Endelea kuwa na imani!
👥 Victor Kamau Guest Dec 1, 2019
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Anna Malela Guest Sep 28, 2019
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Benjamin Masanja Guest Sep 27, 2019
Mwamini katika mpango wake.
👥 Joyce Mussa Guest Jun 9, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Patrick Akech Guest Dec 31, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Frank Macha Guest Nov 20, 2018
Sifa kwa Bwana!
👥 Nora Lowassa Guest Nov 2, 2018
Baraka kwako na familia yako.
👥 Esther Cheruiyot Guest Sep 25, 2018
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Henry Sokoine Guest Sep 25, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Joyce Mussa Guest Aug 26, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 George Ndungu Guest Feb 7, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Grace Wairimu Guest Dec 31, 2017
Dumu katika Bwana.
👥 Samson Mahiga Guest Dec 5, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Joyce Nkya Guest Sep 9, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Nancy Kabura Guest Apr 17, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Ruth Kibona Guest Feb 23, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Peter Tibaijuka Guest Jan 28, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
👥 John Mushi Guest Jan 23, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Paul Kamau Guest Oct 4, 2016
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Lydia Mzindakaya Guest Sep 30, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Rose Kiwanga Guest Sep 6, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Frank Macha Guest Jul 30, 2016
Neema na amani iwe nawe.
👥 Victor Malima Guest Apr 9, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Joseph Kitine Guest Mar 1, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Isaac Kiptoo Guest Jan 25, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Hellen Nduta Guest Nov 23, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Thomas Mtaki Guest Sep 28, 2015
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About