Amri za Kanisa: Mambo ya Muhimu kujua na Kuzingatia

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2016-12-19 17:34:00πŸ’¬ 50 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF

Amri za Kanisa ni zipi?

Amri za kanisa ni;
1. Hudhuria Misa Takatifu Dominika na sikukuu zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya Majivu; usile nyama siku ya Ijumaa Kuu
3.Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Pasaka
5. Saidia Kanisa Katoliki kwa zaka
6. Shika sheria Katoliki za ndoa.


Katika Amri ya kwanza ya Kanisa tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tusikilize Misa kila siku ya Mungu na Sikukuu zilizoamriwa.


Sikukuu zilizoamriwa ni zipi?

Ndizo:

1. Kuzaliwa kwa YesuΒ - Noeli tarehe 25/12
2. Pasaka -Β Ufufuko wa Bwana Yesu
3. Kupaa Yesu β€”- Siku 40 baada ya Pasaka.
4. Kupalizwa Mbinguni Bikira Maria 15/8
5. Sikukuu ya Watakatifu Wote 1/11


Katika Amri ya Kwanza ya kanisa tumekatazwa nini?

Tumekatazwa;
1. Kukosa Misa
2. Kufanya kazi nzito siku hizo


Kujinyima ni nini?

Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.


Nani ana lazima ya kufunga?

Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula. (Jumatano ya Majivu)


Siku za kufunga ni zipi? Na siku gani tumekatazwa kula nyama?

Siku za kufunga ni Jumatano ya majivu, siku za Kwaresima isipokuwa Dominika zake, na siku iliyokatazwa kula nyama ni siku ya Ijumaa kuu.


Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa kuungama mara kwa mara walau mara moja kila mwaka


Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa tupokee Ekaristi Takatifu walau mara moja kwa mwaka wakati wa pasaka.


Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa kufahamu kuwa gharama za dini na za mapadre zatupasa. Yaanai wakristo walitegemeze Kanisa na wahudumu wake na hasa katika kazi ya kueneza injili.


Zaka ni nini?

Zaka ni asilimia kumi (10%) ya pato la mtu kwa mwaka ambalo anapaswa kulitoa kwa Kanisa.


Asiyelipa Zaka na michango mingine ya Kanisa ya lazima atenda dhambi gani?

Atenda dhambi kubwa: Yampasa kulipa na kuungama.


Amri ya Sita ya Kanisa Inadai nini?

Inadai kushika Sheria Takatifu Za ndoa

πŸ’¬

Discussion

Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.

50 comment(s)
πŸ” Login required to comment or reply

You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.

Log in to participate
M
Monica Lissu2024-06-30 05:49:52
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
J
Janet Mbithe2024-05-02 19:45:29
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
E
Edith Cherotich2024-04-15 16:58:51
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
S
Sarah Karani2024-04-08 09:03:02
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
N
Nancy Kawawa2023-12-29 23:43:59
Nakuombea πŸ™
R
Robert Ndunguru2023-11-20 13:16:46
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
L
Lydia Mutheu2023-11-16 10:37:58
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
E
Esther Cheruiyot2023-11-03 06:17:44
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
B
Benjamin Masanja2023-05-22 00:55:22
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
A
Agnes Njeri2023-05-20 22:04:42
Katika imani, yote yanawezekana
J
Joseph Mallya2023-04-15 07:01:39
Neema ya Mungu inatosha kwako
G
George Tenga2022-11-27 00:20:26
Rehema hushinda hukumu
D
Dorothy Nkya2022-07-11 03:28:02
Tembea kwa imani, si kwa kuona
R
Robert Ndunguru2021-11-21 07:42:08
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
J
Janet Sumaye2021-11-07 01:04:32
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
R
Ruth Kibona2021-05-11 07:58:07
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
J
James Kimani2021-04-06 05:00:30
Dumu katika Bwana.
J
Josephine Nduta2021-03-17 10:27:02
Endelea kuwa na imani!
A
Anthony Kariuki2020-10-30 09:45:34
Tumaini ni nanga ya roho
N
Nicholas Wanjohi2020-10-19 11:20:27
Mwamini Bwana; anajua njia