Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Uzinzi na Uasherati ndio mtego wa kizazi hiki

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Uzinzi na uasherati wakati huu umekuwa ndio sumaku kuu ya kuwanasa watu ili waende jehanamu.

Sumaki hii imewanasa hata ambao hawakutegemewa wala kutarajiwa.

Uzinzi uzinzi uzinzi umekuwa kama perfume ya kujipulizia kila Mara mtu akipenda.

Uasherati umekuwa kama heshima ya kibinadamu kwa vijana wengi.

Mbingu zimenyamaza kwa sababu iko jehanamu inawangoja wazinzi na waasherati.

Dhambi hii imekuwa sumaku kubwa ya shetani ya kukamata wanadamu ili waende jehanamu.

Wanadamu wa Leo ukimwambia kwamba aache uzinifu maana wazinzi na waasherati hawataenda uzima wa milele, mtu huyo anakuambia unamhukumu.

Ni Neno la MUNGU ndile limesema katika maandiko mengi tu kwamba wazinzi na waasherati sehemu yako itakuwa katika ziwa la moto.

Hata makanisani baadhi ya watu wamenasa kwenye sumaku hii.

Dada mmoja ambaye kila wiki anasimama na kushika mic kanisani kwao siku moja aliniambia kwamba hawezi kumaliza wiki bila kufanya ngono, na hajaolewa. Niliumia sana rohoni nikamwambia aache kutumika madhabahuni, yeye akasema itakuaje maana yeye ndiye tegemeo.

Mama mmoja alisema yeye ana mume mema sana na mume wake ni mwaminifu sana katika ndoa yao lakini yeye huyo mama ndio hutoka nje ya ndoa Mara kwa Mara, ni hatari inayohitaji neema ya MUNGU tu ili kutubu na kuacha.

Mama mmoja yeye ana watoto zaidi ya wawili na yuko katika ndoa lakini hana uhakika kama watoto wale ni wa mume wake wa ndoa, ni hatari sana.

Baba mmoja akiwa ndani ya ndoa amezaa watoto zaidi ya watatu nje ya ndoa tena wanawake zaidi ya wanne(4) tofauti tofauti.

Mwanaume moja ambaye husimama madhabahuni yeye kila Mara humdanganya mkewe kwamba anaenda safari kumbe ana mahawara karibia kila mkoa, ni hatari sana.

Watu wengi sasa wanaona uzinzi na uasherati ndio fashion nzuri ya wakati kuu.

Kila kijana ana girlfriend kwa lengo la ngono tu na sio vinginevyo.

Kila binti ana boyfriend kwa ajili ya uasherati.

Ukitaka watu wakuchukie basi kemea uzinzi na uasherati.

Watu wengi wamekuwa vipofu wa kiroho kwa sababu ya uzinzi na uasherati.

Lakini upo mwisho mmoja kwa watenda dhambi wote ambayo ni jehanamu.

Ndugu unahitaji kutubu Leo na kuacha dhambi.

Ndugu mmoja akasema yeye anaishi maisha matakatifu ila dhambi moja tu yaani uzinifu ndio imemshinda, hiyo ni hatari.

Leo hata ndoa takatifu zimeadimika maana wahusika huanza kwanza uzinzi na uasherati ndio baadae ndoa, ndugu mnahitaji kutubu.

Ndugu yangu unayenisikiliza kwa njia ya ujumbe huu nakuomba tubu na acha dhambi hiyo.

Amua kuiacha.

Mwisho wa uzinzi na uasherati ni kifo(Mauti) na baada ya kifo ni hukumu(Waebrania 10:27)

Nimekuonya wewe Leo ili ukishupasa shingo usije ukalaumu siku ile ukiwa katikati ya bahari ya moto huku kifo kimezuiliwa ili uteseke milele.

Mimi naamini utatengeneza ndugu baada ya kuusoma ujumbe huu.

Mimi naamini utaachana na mahawara na kuanza kuiheshimu ndoa yako.

Mimi naamini hutamsaliti tena mkeo/Mumeo.

Mimi naamini utaachana na huyo girlfriend/Boyfriend, wengine wanao zaidi ya mmoja, nakuomba ndugu achana nao.

Kijana au binti kaa tulia hadi wakati wako wa ndoa.

Uliyenisikia na utatubu na kuacha dhambi hiyo, MUNGU akubariki sana.```

ALIYE NA AKILI AWEKE MOYONI MANENO HAYA. AMINA

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ James Mduma Guest Jun 9, 2024
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Mar 17, 2024
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Dec 30, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Aug 31, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Aug 21, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Francis Njeru Guest Jul 7, 2023
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest May 17, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Stephen Mushi Guest Apr 17, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Mar 20, 2023
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Mary Mrope Guest Jan 4, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Dec 31, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Jul 22, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest May 31, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Mar 14, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Jan 28, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Dec 17, 2021
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Oct 14, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Oct 14, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Oct 11, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ David Sokoine Guest May 28, 2020
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Nov 27, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Nov 12, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Sep 4, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Apr 13, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Feb 8, 2019
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Jan 6, 2019
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Jan 1, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Dec 15, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Nov 26, 2018
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Jane Malecela Guest Jun 10, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest Jun 5, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest Jan 31, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Jul 8, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Grace Wairimu Guest Jul 3, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Jun 28, 2017
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest Mar 29, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Feb 28, 2017
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Dec 22, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Dec 13, 2016
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ John Mushi Guest Nov 2, 2016
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Oct 10, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Sep 18, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest Sep 6, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Martin Otieno Guest Jul 18, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ John Kamande Guest Feb 3, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Francis Mtangi Guest Feb 1, 2016
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Dec 27, 2015
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ John Lissu Guest Sep 30, 2015
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Aug 31, 2015
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Jun 20, 2015
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About