Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makundi yote tisa ya Malaika. Kuendana na jinsi tunavyofunuliwa katika Maandiko Matakatifu, makundi haya tofauti tofauti ya Malaika hujipanga kuanzia karibu sana na Kiti cha Enzi alipo Mwenyezi Mungu, kwenda chini tulipo sisi wanadamu. Makundi hayo kuanzia juu kwenda chini ni Maserafi, Makerubi, Wenye Enzi, Watawala, Wenye Nguvu, Wenye Mamlaka, Wakuu, Malaika Wakuu na Malaika.

Asili ya Rozari hii ni maono aliyopata Mtumishi wa Mungu Antonia d'Astonac, ambaye alitokewa na Malaika Mkuu Mikaeli aliyemfundisha sala za Rozari hii kwa kumwelekeza kuwa anataka aheshimiwe kwa salamu tisa kufuatana na makundi tisa ya Malaika.

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu aliahidi kuwa yeyote anayefanya ibada hii kwa heshima, akaribiapo Meza Takatifu, atasindikizwa na Malaika tisa, mmoja kutoka kila kundi la Malaika. Zaidi ya hayo, kwa kusali rozari hii, aliahidi msaada wa daima, na kwamba Malaika watamsaidia mwenye kuisali duniani na kumtoa toharani akifariki, yeye pamoja na jamaa zake.

ROZARI YA MALAIKA MKUU MIKAELI


Ee Mungu unielekezee msaada, Ee Bwana unisaidie hima!
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele. Amina.

Sali Baba Yetu (mara nne) kwa heshima ya Malaika Wakuu, Mtakatifu Mikaeli, Mtakatifu Gabriel, Mtakatifu Rafaeli na Malaika Mlinzi.

1. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Mikaeli; Baba Yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike, utakalo lifanyike duniani kama mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina
2. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Gabrieli; Baba Yetu, …..
3. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Rafaeli; Baba Yetu, …..
4. Kwa heshima ya Malaika Wangu Mlinzi; Baba Yetu, ……

Sali Baba Yetu moja na Salamu Maria tatu baada ya kila salamu katika tisa zifuatazo kwa heshima ya Makundi Tisa ya Malaika

Baba Yetu (mara moja, - tazama hapo juu)

Salamu Maria
Salamu Maria umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu, Amina.

1. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya kundi la Serafin, Bwana awashe mioyoni mwetu moto wa mapendo kamili. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

2. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Kerubin, Bwana atuwezeshe kuacha njia mbaya na kuenenda katika njia ya ukamilifu wa kiKristo. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

3. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Enzi, Bwana atujalie roho ya unyofu na unyenyekevu wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

4. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Watawala, Bwana atujalie neema ya kushinda maasi yetu na tamaa mbaya. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

5. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Nguvu, Bwana atukinge na vishawishi na mitego ya shetani. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

6. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Mamlaka, Bwana atukinge na mwovu wala tusianguke vishawishini. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

7. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wakuu, Bwana atujalie kuwa na roho ya utii wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

8. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika Wakuu, Bwana atudumishe katika imani na katika kazi zote njema ili tujaliwe utukufu wa Milele. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

9. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika, Bwana atujalie ulinzi wao duniani hapa na baadaye watuongoze kwenye furaha za Mbinguni. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kutujaza mapaji saba ya Roho Mtakatifu.

TUOMBE
Ee Mungu Mwenyezi wa milele, kwa wema na huruma yako ya ajabu, umetaka watu wako waokoke, ukamweka Malaika Mkuu Mikaeli kuwa Mkuu wa Kanisa lako, Utukinge na adui zetu, wasitusmbue saa ya kufa kwetu, bali tuongozwe naye kwenye utukufu wako Mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana Wetu Yesu Kristo. Amina.

Utuombee Ee Mtukufu Mtakatifu Mikaeli Mkuu wa Kanisa la Yesu Kristo, tujaliwe ahadi za Kristo. Amina.

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya shetani, Mungu amtiishe, tunaomba sana, nawe Mkuu wa Majeshi ya Mbinguni kwa nguvu ya Mungu uwaangushe motoni shetani na pepo wabaya wengine wote, wanaozunguka duniani, ili kuzipoteza roho za watu.
Amina.

SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI

Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi,
Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa,
Uwe nami leo hii,
Kuniangaza na kunilinda,
Kunitawala na kuniongoza.
Amina.

SALA NYINGINE KWA MALAIKA WAKO MLINZI

Ee Malaika wangu Mlinzi, uliyewekwa na Mungu Mwema, naomba unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina

Sali mara kwa mara unapokumbuka, hasa asubuhi uamkapo na usiku kabla ya kulala, Atukuzwe mara saba, kwa heshima ya Malaika wako Mlinzi.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Jun 16, 2024
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Sharon Kibiru Guest Jun 2, 2024
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ David Ochieng Guest May 14, 2024
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Grace Mushi Guest May 5, 2024
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Mar 22, 2024
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Mar 19, 2024
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Feb 19, 2024
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Dec 5, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Oct 9, 2023
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Jul 30, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Jane Muthui Guest Jul 27, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Jul 16, 2023
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Jul 11, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Jun 13, 2023
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Jan 25, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Sharon Kibiru Guest Jan 7, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Nov 22, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Nov 22, 2022
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Nov 5, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Grace Mushi Guest Sep 3, 2022
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Jul 13, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Jul 2, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Jun 18, 2022
πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Apr 4, 2022
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ George Tenga Guest Mar 30, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest Mar 28, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Mar 27, 2022
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Peter Otieno Guest Mar 9, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Jan 21, 2022
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ John Malisa Guest Sep 12, 2021
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Aug 9, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest May 26, 2021
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ John Lissu Guest May 3, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Mar 8, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Janet Mbithe Guest Jan 21, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Dec 17, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Michael Onyango Guest Nov 20, 2020
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Aug 22, 2020
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Jul 29, 2020
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Jun 16, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest May 14, 2020
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Apr 12, 2020
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Feb 6, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Jan 18, 2020
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Jan 2, 2020
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Sep 2, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest May 15, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Apr 1, 2019
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Sharon Kibiru Guest Jan 5, 2019
πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Nov 20, 2018
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Sep 17, 2018
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Sep 6, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Jul 15, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Jul 11, 2018
πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest Jul 5, 2018
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Samuel Were Guest May 24, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Jan 11, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Dec 30, 2017
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ James Malima Guest Dec 3, 2017
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Oct 29, 2017
Mwamini katika mpango wake.

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About