Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, - Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,

Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jul 9, 2024
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Jun 16, 2024
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Janet Mbithe Guest Apr 6, 2024
Amina
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Nov 26, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Sep 18, 2023
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Sep 3, 2023
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Jul 1, 2023
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Apr 5, 2023
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Mar 24, 2023
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Jan 18, 2023
πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πŸ‘₯ Maida Guest Jan 7, 2023
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Nov 24, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Oct 28, 2022
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Sep 8, 2022
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Sep 1, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Aug 31, 2022
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Jun 9, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Jun 2, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest May 14, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Apr 21, 2022
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Apr 3, 2022
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Feb 21, 2022
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Oct 17, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest Aug 1, 2021
πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Jul 16, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ James Malima Guest Jun 1, 2021
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Janet Mbithe Guest Mar 10, 2021
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Jan 16, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Jan 4, 2021
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Nov 23, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Oct 8, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Oct 5, 2020
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ James Malima Guest Sep 8, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Aug 8, 2020
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Jun 9, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest May 16, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest May 6, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ James Mduma Guest Apr 22, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Apr 17, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest Mar 31, 2020
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Mar 10, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Feb 21, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ John Kamande Guest Jun 22, 2019
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Brian Karanja Guest Jun 9, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Feb 6, 2019
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest Dec 23, 2018
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Nov 12, 2018
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Josephine Nduta Guest Nov 3, 2018
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Oct 14, 2018
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Oct 8, 2018
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Aug 12, 2018
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Jun 4, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Apr 22, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Mar 23, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ George Wanjala Guest Mar 20, 2018
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Dec 24, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Nov 20, 2017
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Nov 10, 2017
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ John Mushi Guest Oct 27, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Oct 12, 2017
Mwamini katika mpango wake.

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About