Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.

TESO LA KWANZA

Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga.
Tuombe neema ya kuvumilia mateso.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA PILI

Maria na Yosefu walikimbilia Misri usiku ili kumficha Mtoto Yesu asiuawe na Herodi.
Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA TATU

Mama Maria aliona uchungu sana Mtoto Yesu alipopotea kwa siku tatu.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA NNE

Mama Maria aliona uchungu sana alipokutana na Mwanae Yesu katika njia ya Msalaba.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA TANO

Mama Maria aliona uchungu sana alipomwona Mwanae Yesu akisulibiwa Msalabani.
Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA SITA

Mama Maria aliona uchungu sana alipopakata maiti ya Mwanae Yesu baada ya kushushwa Msalabani.
Tuombe neema ya kutotenda dhambi.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA SABA

Mama Maria aliona uchungu sana aliporudi nyumbani baada ya kumzika Mwanae Yesu
Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

LITANIA YA MAMA WA MATESO

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, - Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,

Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubwa sana ulipotazama mateso na kifo cha Mwana wako mpenzi. Muda ule uliweza kutuliz kidogo kwa sababu ya kumwona angali hai. Lakini je, baada ya kufa na kumzika? Sasa wewe ni mkiwa mkubwa mno! Uh, ukiwa wa pekee, uniombee mimi ninayempoteza mara nyingi kwa dhambi zangu. Unijalie nisimpoteze tena Yesu wangu kwa ubaya wa uvivu wangu, bali nimtumikie kiaminifu duniani hapa ili nimwone na kumfurahia milele mbinguni. Amina.

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkingaji na mteteaji wangu. Naweka roho fukara katika moyo wako uliotobolewa na panga nyingi za mateso. Unipokee mimi niwe mtumishi wako wa pekee na mshiriki wa mateso yako. Nijalie nguvu niwe daima karibu na msalaba ule alikosulibiwa Yesu. Nakutolea nafsi yangu na mali yangu yote. Pokea kila tendo langu jema ukalisindikize kwa Mwanao, Mama, nifanye nistahili kuitwa mtumishi wa Maria, Simama karibu yangu katika matendo yangu yote ili yafanwe kwa sifa ya Mungu. Ulivyosimama karibu kabisa ya Mwanao alipokufa msalabani uwe karibu nami saa ya kufa kwangu. Nijalie niweze kutaja jina lako na la Mwana wako nikisema: β€œYesu, Maria na Yosef mnisaidie saa ya kufa kwangu. Yesu, maria na Yosef, naomba nife kwa amani kati yenu!” . Amina.

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na uliyemtazama Mwana wako akifa, unitazame kwa huruma ya kimama ninayekusikitikia. Kwa sababu ya upanga uliochoma moyo wako, kwa mateso ya maisha yako nakuomba uniangalie kwa wema ukasikilize maombi yangu. Nakuomba, ee Mama, uniombee daima kwa Mwana wako, najua hawezi kukuvyima wewe kitu chochote. Basi, ufanye, Moyo wa Mwanao ukubali kunijalia ombi langu hili …………………(taja ombi lako).
Maana nitamkimbilia nani katika mahitaji na misiba yangu isipokuwa kwako, ee Mama wa huruma? Wewe hasa unaweza kutusaidia sisi tulio bado katika bonde la machozi kwa sababu ulishiriki mateso ya Mwanao kutukomboa. Umtolee Yesu tone moja la Damu yake takatifu. Umkumbushe ya kuwa wewe ni matumaini, furaha na maisha yetu ukanipatie jambo ninalokuomba kwa Yesu Kristo, bwana wetu. Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Jul 15, 2024
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Jul 11, 2024
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest May 24, 2024
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest May 14, 2024
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Feb 16, 2024
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Francis Mtangi Guest Jan 18, 2024
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Sep 28, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Martin Otieno Guest Jul 23, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Jun 22, 2023
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest May 1, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Mar 13, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Nov 16, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Oct 31, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Oct 12, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Aug 25, 2022
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Aug 24, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Jul 21, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Jul 13, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Jul 8, 2022
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Jul 2, 2022
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Jun 23, 2022
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Jun 12, 2022
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Jun 2, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest May 27, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Apr 21, 2022
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Apr 11, 2022
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Apr 11, 2022
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Mar 29, 2022
Amina
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Mar 17, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Mar 3, 2022
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ David Chacha Guest Feb 13, 2022
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Jan 24, 2022
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Dec 30, 2021
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest Dec 18, 2021
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Oct 24, 2021
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Sep 2, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ George Mallya Guest Jul 7, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Jun 6, 2021
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Stephen Mushi Guest May 2, 2021
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Stephen Mushi Guest Apr 8, 2021
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Mar 18, 2021
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Josephine Nduta Guest Mar 12, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Dec 7, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Nov 14, 2020
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Oct 18, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Sep 29, 2020
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Sep 16, 2020
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ James Mduma Guest Jun 18, 2020
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Feb 1, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Dec 31, 2019
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest Dec 23, 2019
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Dec 3, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ James Mduma Guest Aug 11, 2019
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest Aug 2, 2019
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Mary Mrope Guest Jul 25, 2019
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest May 31, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Apr 23, 2019
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Jan 3, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Nov 26, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Nov 25, 2018
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About