Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Safisha samaki na kisha uwamarinate na kitunguu swaum, tangawizi, limao na chumvi kwa muda wa nusu saa. Baada ya hapo wakaange na usiwakaushe sana kisha waweke pembeni. Chukua fry-pan kisha tia mafuta kidogo sana (kama 1/2 kijiko cha chai) kisha tia vitunguu maji na uvikaange kwa muda wa dakika 2 (kwani havitakiwi kuiva kabisa) kisha waweke samaki na uwachanganye na hivyo vitunguu. Kisha baada ya hapo tia giligilani iliyokatwa, kamulia limao na tia chumvi kidogo kisha geuzageuza ili kuchanganya vitu vyote na kisha ipua. Baada ya hapo menya na ukate viazi katika vipande vya wastani, na kisha uvichemshe kidogo na visiive kabisa. Baada ya hapo weka sufuria jikoni kwenye moto wa wastani na utie mafuta kidogo (kama vijiko 2 vya chakula) na kisha tia viazi na uanze kuvipika kwa kuvigeuzageuza mpaka viive na kuwa rangi ya brown kisha tia chumvi kidogo, curry powder na giligilani iliyokatwa.Vipike kwa muda wa dakika mbili kisha viipue. Na baada ya hapo malizia kwa kupika asparagus. Kwanza zioshe kisha zikate kati. Baada ya hapo weka mafuta kidogo kama 1/2 kijiko katika fry-pan yakisha pata moto tia kitunguu swaum, asparagus na chumvi.Zipike kwa kuzigeuzageuza kwa muda wa dakika 5 na hapo zitakuwa zimeshaiva na tayari kwa kuliwa pamoja na samaki na viazi. Unaweza kuvisevu kwa ketchup.
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Majimbi (Eddoes) kiasi 6 au 7
Nyama ng’ombe ½ kilos
Tangawizi ilosagwa 1 kijiko cha kulia
Haldi (bizari manjano/turmeric) ½ kijiko cha chai
Tui zito la nazi vikombe 2
Chumvi kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Safisha nyama kisha weka chumvi, bizari ya manjano, tangawizi mbichi, ukaushe kwanza katika sufuria kwa kukaanga kaanga. Ikianza kukauka, weka maji funika uchemshe iwive. Menya majimbi ukate kate na uweke katika sufuria nyengine. Mimina supu na nyama katika majimbi uchemshe yawive majimbi. Mwisho weka tui zito la nazi uchanganye vizuri kisha weka katika moto kidogo tu bila kufunika yakiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:56 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
· Osha mikono yako kwa sabuni kabla na baada ya kutayarisha chakula · Tumia vyombo safi na sehemu safi kwa kutayarisha na kula chakula · Viporo vipashwe moto vizuri kabla ya kula · Chemsha maji ya kunywa na kuyaacha jikoni dakika kumi baada ya kuchemka
Updated at: 2024-05-25 10:37:56 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Ngogwe ½ kg Kitunguu 2 Bamia ¼ kg Karoti 2 Mafuta vijiko vikubwa 8 Maji vikombe 3 Mayai 2 Nyanya 2 Chumvi
Hatua
• Osha, menya na katakata nyanya na vitunguu. • Osha, menya na kata karoti virefu virefu. • Osha, kata ncha za bamia pande zote na kama ndefu sana kata vipande viwili. • Osha, kata vikonyo vya ngongwe, kama ni kubwa kata vipande viwili. • Kaanga vitunguu, ongeza nyanya, korogoa mpaka zilainike. • Ongeza ngogwe, karoti, bamia na chumvi, koroga mpaka zionekane kukolea rojo. • Ongeza maji vikombe 2 koroga na funikia kwa dakika 10-15 au mpaka ziive. Punguza moto. • Koroga mayai kwenye maji mpaka iwe kama maziwa, ongeza kwenye mboga na koroga polepole usiponde ngogwe wala bamia kwa dakika 5. • Onya chumvi, pakua za moto kama kitoweo.
Updated at: 2024-05-25 10:23:02 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama ya kusaga (minced beef 1/4 kilo) Vitunguu maji vilivyokatwakatwa(diced onion 2 vikubwa ) Kitunguu swaum/ tangawizi (garlic and ginger paste 1 kijiko cha chakula) Chumvi (salt) Pilipili iliyokatwakatwa (scotch bonnet 1) Limao (lemon 1/2) Curry powder 1/2 kijiko cha chai Cinnamon powder 1/4 kijiko cha chai Coriander powder 1/4 kijiko cha chai Cumin powder 1/4 kijiko cha chai Unga wa ngano (all purpose flour kidogo) Manda za kufungia (spring roll pastry) Giligilani (fresh coriander kiasi) Mafuta ya kukaangia
Matayarisho
Changanya nyama na limao, chumvi, pilipili,kitunguu swaum, tangawizi na spice zote, kisha pika katika moto wa kawaida mpaka nyama iive na maji yote yakauke. Baada ya hapo kabla hujaipua nyama tia vitunguu na giligilani na uvipike pamoja kwa muda wa dakika 2 na uipue weka pembeni na uache viipoe. Baada ya hapo tia unga kidogo katika bakuli nauchanganye na maji kidogo kupata uji mzito kwa ajili ya kugundishia manda. Baada ya hapo tia nyama katika manda na kisha zifunge kwa kugundishia na unga wa ngano.Ukisha maliza kuzifunga zote zikaange mpaka ziwe za brown na uzitoe. Na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:22:57 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ulezi (millet flour vijiko 3 vya chakula) Maziwa fresh (milk 1/2 kikombe) Sukari (sugar 1/4 ya kikombe cha chai) Siagi (butter kijiko 1 cha chakula) Maji (vikombe 4 vya chai) (serving ya watu wawili)
Matayarisho
Chemsha maji ya uji, Kisha koroga unga na maji ya baridi kiasi na uchanganye kwenye maji ya moto yanayochemka. Endelea kukoroga mpaka uchemke ili kuhakikisha uji haupatwi na madonge. Ukishachemka tia, maziwa, sukari na butter. Kisha acha uchemke kwa muda wa dakika 10 na hapo uji utakuwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:34:39 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ngano nzima (shayiri) - 3 Vikombe
Kuku - ½ (3 LB takriban)
Thomu na tangawizi iliyosagwa - 1 kijko cha supu
Pilipili manga ya unga - ½ kijiko cha chai
Jiyrah (cumin/bizari ya pilau) - ½ kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Kidonge cha supu - 1
Samli ya moto - ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Roweka ngano (shayiri) tokea usiku au muda wa masaa. Katakata kuku mtie katika sufuria, tia maji kiasi viungo vyote. Mchemeshe awive na ibakie supu yake. Toa kuku, toa mifupa na umchambue chambue vipande vidogo vidogo. Chemisha ngano (shayiri) kwa kufunika sufuria hadi iwive na kukauka maji. Tia supu ya kuku katika ngano (shayiri), na kuku uliyemechambua. Tia kidonge cha supu. Tia samli nusu (bakisha nusu) kisha songa mchanganyiko uchanganye hadi ivurugike kuku na ngano (shayiri) vizuri. Mimina katika sahani, mwagia samli imoto ilyobakia likiwa tayari.
Jinsi ya kupika Visheti Vya Kastadi Vya Shepu Ya Kombe
Updated at: 2024-05-25 10:34:51 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga wa ngano 1 Kilo
Siagi ¼ kilo
Mayai 2
Kastadi (custard) 3 vijiko vya supu
Baking powder 1 kijiko cha chai
Maziwa 1 ½ gilasi
Mafuta Ya kukaangia kiasi katika karai
Maandalizi na upikaji
Weka unga katika bakuli kubwa kisha changanya na unga wa kastadi na baking powder. Tia siagi uchanganye vizuri. Tia mayai, kisha maziwa ya baridi uchanganye vizuri usiukande sana. Fanya madonge kisha kata vipande vidogovidogo kisha ubonyeze kwa kidole uvikwaruze kwenye chujio lenye tundu itokee shepu (design) yake.
5- Tia mafuta katika karai yakipata moto, kaanga visheti hadi viive. Usiache hadi vikageuka rangi sana.
6- Eupua, weka katika sufuria au chombo kikubwa kusubiri shira.
Vipimo Vya Shira
Sukari ½ kilo
Hiliki ilosagwa 1 kijiko cha chai
‘arki (rose flavor) 5 matone
Maji 1 gilasi
Namna Ya Kutyarisha
Changanya sukari na maji uipike hadi iwe nzito. Ukiona mapovu yanatoka tia hilik na ‘arki . Mwagia katika visheti uchanganye vizuri hadi vishike na sukari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:42 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Samaki (Tilapia 2) Nyanya ya kopo (Tomato tin 1) Kitunguu (Onion 1) Tangawizi (ginger kiasi) Kitunguu swaum (garlic clove ) Mafuta (Vegetable oil) Pilipili (scotch bonnet pepper 1) Tui la nazi zito (coconut milk 2 vikombe vya chai) Curry powder 1/2 cha kijiko cha chai Binzari nyembamba ya unga (ground cumin 1/2 kijiko cha chai Binzari manjano (turmaric 1/2 kijiko cha chai Chumvi (salt) Limao (lemon 1) Giligilani (fresh coriander)
Matayarisho
Marinate samaki na chumvi, limao, kitunguu swaum, tangawizi kwa muda wa masaa 6 au zaidi. Baada ya hapo wakaange au waoke katika oven mpaka waive ila usiwakaushe sana. Baada ya hapo saga pamoja nyanya ya kopo, kitunguu maji, kitunguu swaum na tangawizi. Kisha bandika huo mchanganyiko jikoni na upike mpaka ukauke maji kisha tia mafuta, binzari zote, curry powder, chumvi na pilipili na upike kwa muda wa dakika 5. Baada ya hapo tia maji kidogo (kama 1/2 kikombe) pamoja na tui la nazi. Acha uchemke mpaka tui liive na mchuzi ubakie kiasi. Baada ya hapo waweke samaki kwenye sufuria ya kuokea na kisha umwagie huo mchuzi juu ya hao samaki na owaoke (bake) kwa muda wa dakika 20. Ukisha toa kwenye oven katakata giligilani na utie kwenye hao samaki na hapo watakuwa tayari kwa kuliwa. unaweza kuwala na wali, ugali au chapati