Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kuku Na Mboga Mchanganyiko

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Vipimo

Mchele wa basmati/pishori - 4 vikombe vikubwa (mugs)

Kuku - 2

Vitnguu vya kijani (sprin onions) katakata - 5 miche

Maharage machanga (spring beans) katakata - kiasi kujaza mug moja

Pilipili boga la (capsicum) katakata - 1

Karoti katakata vipande virefu - 1

Kitunguu thomu (garlic) kuna (grate) - 1 kubwa

Tangawizi mbichi kuna (grate) - 1 kubwa

Sosi ya soya (soy sauce) - 2 vijiko vya supu

Kidonge cha supu - 1

Mafuta ya kupikia - ΒΌ kikombe cha chai

Chumvi - kiasi

Pilipili manga - 1 kijiko cha supu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha kuku vizuri, katakata vipande, weka katika sufuria, tia chumvi, pilipili manga, mfunike, umkaushe motoni huku ukimgeuza geuza.

Roweka mchele kisha uchemshe uive nusu. Chuja maji, tia siagi kidogo ili usigandane.

Weka karai ya kupika mboga (wok) au sufuria kisha tia mafuta yashite moto.

Tia kitunguu thomu, tangawizi, kaanga kidogo.

Tia mboga zote, ulizokatakata.

kaanga kidogo, kisha tia sosi ya soya na kidonge cha supu. Usizipike sana mboga mpaka zikalainika mno. Sababu zitaiva katika mchele

Changanya kuku na mboga kisha changanya vyote katika mchele, urudishe katika moto.

Funika upike hadi uive kamilifu.

Pakua kwenye sahani.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 0

Please log in or register to comment or reply.
No comments yet. Be the first to share your thoughts! πŸ“

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About