Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Mapishi ya Wali Wa Karoti Na Kuku Wa Kukaanga

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Vipimo Vya Wali

Mchele wa Basmati/Pishori - 1 kilo moja

Vitunguu maji - 3

Karoti - 2

Siagi - 3 vijiko vya supu

Kidonge cha supu (stock) - 1 kimoja

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Γ“sha mchele uroweke kama saa moja au mbili
Katakata vitunguu vipande vidogodogo (chopped) weka kando.
Kwaruza karoti (grate) weka kando.
Tia siagi katika sufuria ya kupikia wali, weka katika moto iyayuke
Kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi kiasi tu.
Tia maji kiasi ya kupikia wali, changanya na kidonge cha supu.
Yakichemka tia mchele, koroga, funika uweke moto mdogo mdogo.
Kabla ya maji kukauka tia karoti changanya wali kisha funika uive kama unavyopika pilau.

Vipimo Vya Kuku Wa Kukaanga

Kuku alokatwakatwa - 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa - 2 vijiko vya supu

Bizari ya mchanganyiko/garam masala - kijiko cha supu

Mtindi/Yoghurt - 1 kijiko cha supu

Ndimu - 1

Chumvi - kiasi

Mafuta ya kukaangia - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Ukishamuosha kuku, mchuje atoke maji yote.
Changanya viungo vyote katika kibakuli kidogo.
Changanya pamoja na kuku kisha acha akolee viungo (marinate) kwa muda wa masaa mawili takriban.
Weka mafuta katika karai na kaanga kuku, akiwiva yu tayari kuliwa na wali.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 0

Please log in or register to comment or reply.
No comments yet. Be the first to share your thoughts! πŸ“

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About