Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Ufanyialo wengine ndilo utakalofanyiwa

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Siku niliposoma hili andiko kwa mara ya kwanza nakumbuka, kwanza nilipata mshtuko flani baada ya kulisoma, halafu nikajikuta nikitafakari vitu vingi sana.

Hebu kwanza tusome pamoja andiko hili

ZABURI 109

17 Naye alipenda kulaani, nako kukampata.Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye

▶Huu mstari wa 17 umenishangaza sana, halafu ukanifungua na kunifundisha vitu vya msingi sana katika haya maisha tunayoishi

Ngoja tuuchambue kidogo hapa ili tuelewane vizuri

_Alipenda kulaani?………………………….Nako (laana/kulaaniwa) kukampata_

_Hakupendezwa na kubariki……………………(Kubarikiwa) kukawa mbali nae_

NET BIBLE inasema hivii

“He loved to curse others, so those curses have come upon him, He had no desire to bless anyone, so he has experienced no blessings” Kumbe the more ninakuwa na shauku ya kuona wengine wakibarikiwa, the more baraka zinanijia mimi and vice versa

Hapa nikajifunza kwamba kumbe yale mabaya tunayowafanyia au kuwawazia watu kuna uwezekano mkubwa sana yakatupata sisi wenyewe

Na tunapotamani kubarikiwa na kuinuliwa wakati hatufurahii kuona wengine wakiinuliwa, kuinuliwa kutakuwa mbali nasi

Huu mstari unaniongezea maarifa na kunifundisha namna ya kuishi katika ulimwengu huu

Nimewaza pia inawezekana wakati mwingine kuna vitu hatupati ni kwasababu tuu hatufurahii wala hatuombi wengine wapate hivyo

Kumbe kubarikiwa kwangu kunategemea na namna ambavyo ninakuwa baraka kwa wengine na kutamani kuona wengine wakibarikiwa

Shauku yangu ya kutamani wengine wabarikiwe na kuinuliwa ndio nyenzo ya kuinuliwa kwangu na moyo mbovu wa kufurahi kuona wengine wakikwama ndio sababu ya kukwama kwangu?

_"Hii ni kanuni ya ajabu"
Ndugu yangu, unajua hapa najifunza kwamba kumbe kuna uwezekano mkubwa kwamba mikwamo mingine tumekuwa tukijikwamisha sisi wenyewe

Ni kweli ninataka kubarikiwa, lakini ni mara ngapi nimefurahi au kuombea wengine ili wabarikiwe?

Unatamani kupandishwa cheo sawa, lakini wengine wakipandishwa vyeo unanuna? Au ukiona ofisini ndio anapewa safari nyingi za nje unakasirika?

Unatamani kuoa/kuolewa halafu wengine wakioa na kuolewa unaona uchungu juu yao, unawanunia, unapunguza ukaribu?

Unatamani kupata gari zuri lakini wengine wakipata unakasirika?

Nikiwa mtoto mdogo nakumbuka mwalimu mmoja aliwahi fundisha kwamba nisipende sana kujiombea mwenyewe, na akasema kama unahitaji kitu, waombee wengine wasionacho wapate, nawe utajibiwa pia, andiko hili limenifanya nielewe kwanini mwalimu yule alifundisha vile

Na wakati mzaburi anaongea maneno haya hapa chini sikumuelewaga, nilijua ni kawaida tuu, nilisoma kikawaida tuu, lakini sasa ndio nimefunguka ufahamu zaidi

*ZABURI 35*

13 Bali mimi, walipougua wao, Nguo yangu ilikuwa gunia. Nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga; Maombi yangu yakarejea kifuani mwangu

Bila kujali watu walikuwa wakimuwazia na kumfanyia nini, alipowaombea tuu, maombi yale yalirejea, yalifanya kazi na katika maisha yake. Kumbe kuomba kwaajili ya wengine wafanikiwe, wainuliwe, wabarikiwe na wapandishwe kunarejesha matunda kwetu pia

Ubaya unaomfanyia mwingine si ajabu ukakupata

Kuanguka unakomuombea mwingine kutakujia wewe

Kanuni hii inanifundisha pia kuwa YESU aliposisitiza tupendane alikuwa na maana kuu

Alijua kwamba ukiwa na chuki kwa mwingine chuki ile itakuathiri wewe

Ukiwa na moyo wa kufurahi wengine wanaposhindwa, kushindwa kutakupata wewe

Kwanini sasa tusichague kubariki wengine ili baraka zile zitupate na sisi pia?

Kwanini tusiwaombee mema wengine ili maombi yale ya mema yatutendee mema sisi?
Ni vyema sasa tukachagua kuwa na moyo wa upendo, moyo utakaowawazia na kuwatendea mema wengine kwasababu mema yale tuwafanyiayo wengine yatatuletea mema maishani mwetu pia

Jipime, jiangalie, jichunguze

Waza mema kwaajili ya wengine, mema yaje kwaajili yako

MITHALI 17

13 Yeye arudishaye mabaya badala ya mema,Mabaya hayataondoka nyumbani mwake

If you love to curse others, those curses will come upon you

If you have NO desire to bless others, then you will experience NO blessings

CHOOSE TO BLESS OTHERS,BLESSING WILL FOLLOW YOU

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Joseph Kawawa Guest Mar 11, 2024
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Carol Nyakio Guest Sep 17, 2023
Mungu akubariki!
👥 Rose Kiwanga Guest Aug 18, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Emily Chepngeno Guest Jul 15, 2023
Nakuombea 🙏
👥 Diana Mallya Guest Jun 10, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Ruth Mtangi Guest Apr 25, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Betty Akinyi Guest Apr 4, 2023
Mwamini katika mpango wake.
👥 Dorothy Majaliwa Guest Mar 15, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Lucy Mushi Guest Dec 4, 2022
Dumu katika Bwana.
👥 Martin Otieno Guest Nov 23, 2022
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Ruth Wanjiku Guest Nov 12, 2022
Neema na amani iwe nawe.
👥 Samson Mahiga Guest Nov 8, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Joseph Njoroge Guest Oct 24, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Lydia Mahiga Guest Sep 20, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Rose Mwinuka Guest Aug 5, 2022
Endelea kuwa na imani!
👥 Rose Mwinuka Guest May 22, 2022
Tumaini ni nanga ya roho
👥 John Malisa Guest Feb 10, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Jackson Makori Guest Aug 24, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Ruth Mtangi Guest Jul 9, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Jacob Kiplangat Guest Jun 4, 2021
Rehema zake hudumu milele
👥 Lucy Wangui Guest Mar 18, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Alex Nakitare Guest Apr 22, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Betty Kimaro Guest Oct 19, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Peter Mbise Guest May 25, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Esther Nyambura Guest May 14, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Sarah Karani Guest Nov 22, 2018
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Wilson Ombati Guest Oct 7, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Catherine Mkumbo Guest Aug 16, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Elizabeth Malima Guest Apr 5, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Victor Malima Guest Apr 4, 2018
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Catherine Naliaka Guest Feb 28, 2018
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Monica Adhiambo Guest Jan 4, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Victor Mwalimu Guest Oct 12, 2017
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 David Kawawa Guest Oct 3, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Joseph Njoroge Guest Aug 6, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Stephen Kikwete Guest May 20, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Jacob Kiplangat Guest May 14, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Frank Macha Guest Apr 9, 2017
Rehema hushinda hukumu
👥 Margaret Mahiga Guest Apr 5, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Rose Kiwanga Guest Jan 23, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 David Sokoine Guest Jan 8, 2017
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Joyce Mussa Guest Dec 17, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Joseph Mallya Guest Dec 4, 2016
Sifa kwa Bwana!
👥 Jackson Makori Guest Jul 3, 2016
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 David Sokoine Guest Apr 19, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Stephen Malecela Guest Jan 7, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Lucy Mahiga Guest Oct 17, 2015
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 John Malisa Guest Oct 17, 2015
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Frank Sokoine Guest Aug 27, 2015
Baraka kwako na familia yako.
👥 Francis Mrope Guest Jun 20, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About