Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/mobile/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁
AckyShine

Kwa nini tarehe ya Pasaka hubadilika

Featured Image
KALENDA za mwanzo ziliutumia mwezi wa angani kama kipimo cha muda. Ziliitwa “Lunar calender” au Kalenda-Mwezi. Tarehe 1 ya Mwezi ilikuwa ni siku ulipoandama yaani Mwezi-Mdogo (Crescent Moon). Mwezi unapofika siku ya 15 unakuwa umefikia ukubwa wa juu na huitwa Mwezi- Mkubwa (Full Moon). Hivyo kwa kalenda ile tarehe 15 ilikuwa ni siku ya Mwezi-Mkubwa. Mwaka 45KK, Julius Caesar alitangaza kalenda mpya ikaitwa “Julian Calender” iwe na siku 365. Wakati huo ikijulikana kwamba jua huzunguka kwa siku 365.25. Hivyo pengo la kalenda na mzunguko likabaki robo siku. Robo hiyo ifidiwe kila baada ya miaka minne mwishoni mwa mwezi Februari ambayo sasa ulifanywa kuwa wa pili baada ya January. Inapofanyika hivyo, huo ukaitwa mwaka- mrefu (Leap year). Mwaka mrefu ukachaguliwa kuwa ni ule tu unaogawanywa kwa nne mfano miaka ifuatayo 1700, 1800, 1900, 2100, 2200, 2300. Baadaye iligundulika kuwa jua huzunguka kwa siku 365.24218967 ziitwazo “Tropical year”. Hizi ni chache kuliko siku 365.25 zilizokadiriwa mwanzoni. Uchache huu husababisha kuwe na pengo la dakika 11 na sekunde 14.812512 kwa mwaka. Pengo hili ni dogo, lakini hupanuka hadi kuwa siku nzima kila baada ya miaka 128.0355. Mwaka 1545 lilivuka siku 9.25. Kuondoa tatizo hili, Papa Gregory XIII aliamuru iundwe kalenda mpya na akachagua Oktoba 04, 1582 iwe siku ya mwisho kutumika “Julian Calender”. Kesho yake, kalenda mpya ikaanza kutumika. Ungetegemea hiyo kesho iwe ni Oktoba 05, 1582. Lakini ili uzibe pengo lile lililofikia siku kumi, ilibidi kalenda mpya kuziruka siku hizo siku kumi. Hivyo hii mpya iliyoitwa “Gregorean Calender” ikaanza kama Oktoba 15 badala ya Oktoba 05. Ndiyo sababu katika historia ya nchi nyingi Ulaya, hakuna tarehe za Oktoba 05, 1582 hadi Oktoba 14, 1582. Watu walilala Oktoba 04, 1582 kesho yake wakaamka ikiwa ni Oktoba 15, 1582. Teresa Alonso huandikwa kwamba alifariki Oktoba 1582, kwenye usiku wa tarehe NNE kuamkia tarehe KUMI NA TANO! Alipotangazwa kuwa Mtakatifu, Kanisa Katoliki likaifanya Oktoba 15 kuwa siku ya kumkumbuka, yaani siku ya Mtakatifu Teresa wa Avila. Usipofahamu kwamba Mtakatifu Teresa alifariki siku kalenda zinabadilishwa, utadhani aliyeandika vile tarehe za kifo chake amekosea! Waandishi, William Shakespeare wa Uingereza na Miguel de Cervantes wa Spain huandikwa kwamba wote walifariki Aprili 23, 1616. Lakini ukweli ni kwamba hawakufa siku moja bali walipishana siku kumi kwani England ilichelewa kwa karibu miaka 200 kuikubali “Gregorean Calender”! “Gregorean Calender” haikuundwa ili kuishia kuliziba lile pengo. Bali pia, kuhakikisha halitokei tena. Tumeshaona kuwa lile pengo ni dakika 11 na sekunde 14.812512. Hivyo, linapanuka na kuwa siku tatu ndani ya miaka 400. Hivyo kuliziba inatakiwa kupunguza siku tatu kila baada ya miaka 400.

Je, zipunguzweje?

Kipande cha miaka 400 kina miaka mitatu ya karne inayogawanyika kwa 4 lakini haigawanyiki kwa 400. Ikakubalika kwamba unaogawanyika kwa 4, lakini haugawanyaiki kwa 400, usiendelee kuwa mrefu. Humo siku moja ichomolewe na uwe mfupi. Ndipo miaka 1700, 1800, 1900 haikuwa tena mirefu. Ndivyo pia miaka 2100, 2200, 2300 nayo haitakuwa mirefu. Kwa sababu ni miaka ambayo “Gregorean Calender” inachomoa siku moja ili kutosababisha pengo tena. Kipande hiki cha miaka 400 kikaleta wastani mpya wa siku 365.2425 kwa mwaka. Sasa lile pengo lile la siku moja si rahisi kufikiwa. Kwenye “Julian Calender” tumeona lilikuwa miaka 128.0355 lakini sasa limekuwa miaka 3,222. Sasa tuijadili tarehe ya siku ya Pasaka tukiwa na ufahamu wa kalenda zile. +++ Je, tarehe ya Pasaka imetajwa ndani ya Biblia? Kuna kifungu kinasema hivi: “..Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA. Na siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni sikukuu ya BWANA, ndiyo siku ya mikate isiyotiwa chachu. (Walawi 23:5)..”. Hivyo Pasaka ni tarehe 15 ya mwezi wa Kwanza. Lakini Biblia pia inautaja mwezi wa kwanza kwa jina la Nisan (Esta 3:7, Nehemia 2:1). Yesu alisulubiwa mwaka ambao Ijumaa iliitangulia sikukuu ya Pasaka kwa siku moja (Yohana 18: 28, Marko 15:42-43). Hivyo tarehe ya Yesu kusulubiwa ni Ijumaa, Nisan 14. Siku moja kabla ya Nisan 15. Siku moja kabla ya Mwezi-Mkubwa. Baada ya Yesu, Wakristo wengi Pasaka waliiadhimisha Jumapili, lakini utata ulijitokeza kuhusu tarehe ya kuiweka hiyo Jumapili ya Pasaka. Ilifika wakati jimbo moja la Wakristo linaadhimisha siku tofauti na jingine na kwa njia wanayoijua wao. Utata huu uliondolewa kule Nicaea mwaka 325 ambapo Kanisa Katoliki lilipoamua kuwa, tarehe ya Pasaka iwe moja tu duniani kote, yaani iwe ni Jumapili inayokuja baada ya Mwezi-Mkubwa (Full Moon) unaotokea baada ya siku ya Ikweta, yaani baada ya Machi 21 (Equinox). Baada ya uamuzi huu, wataalamu walipania kuunda chati maalum zenye tarehe za Mwezi- Mkubwa zitazokasaidia kuitambua tarehe ya Pasaka kwa mwaka wowote. Mwezi huizunguka dunia kwa siku 29.5305891203704 (Synodic Month), wakati dunia hulizunguka jua kwa siku 365.24218967 (Tropical year). Mizunguko hii miwili ikianza safari siku moja, itapishana kila mwaka, lakini itakutana tena mwezi unapokamilisha mizunguko 235. Dunia nayo inakuwa imekamilisha mizunguko 19, yaani miaka 19. Wataalamu wakaitumia hii miaka 19 kutengeneza chati yenye tarehe za Mwezi- Mkubwa unaotokea March 22 hadi April 18. Tarehe zile zikaitwa tarehe za Mwezi- Mkubwa Wa Pasaka au Ecclesiastical Full Moon (EFM). Ndani ya ile miaka 19, kila mwaka ukapewa tarakimu iitwayo Golden Number inayosimama badala ya mwaka ikiwa na tarehe zile ziliorekodiwa za Mwezi Mkubwa wa Pasaka. Chati yenyewe ya Golden Number na tarehe zake (siku/Mwezi) ni hii ifuatayo: {1=5/4, 2=25/3, 3=13/4, 4=2/4, 5=22/3, 6=10/4, 7=30/3, 8=18/4, 9=7/4, 10=27/3, 11=15/4, 12=4/4, 13=24/3, 14=12/4, 15=1/4, 16=21/3, 17=9/4, 18=29/3, 19=17/4} Golden Number ya mwaka inapatikana kuanza kuugawa mwaka kwa 19. Tulifundishwa mashuleni kuwa namba inayosalia baada ya kugawa huitwa “Baki” . Hii “Baki” ukiijumlisha na 1 unapata Golden Number (GN). Mfano unatafuta GN ya 27. Hatua ya kwanza ni kutafuta “Baki” baada ya kugawa 27 kwa 19. Hizi ni hesabu za “modulo” , yaani zinahitaji tu namba inayobaki baada ya kugawa. Ikiandikwa hivi: (27 mod 19) inatakiwa namba inayobaki baada ya kuigawa 27 kwa 19. Jibu ni 8. Hivyo tulipaswa tuandike hivi: (27 mod 19=8). “Baki” 8 tuliyoipata, ndiyo tunaihitaji ili tuijumlishe na 1 ili tupate GN ambayo hapa ni 9 kwani (8+1=9). Tungeweza pia kuandika hivi : 27 mod 19 + 1=9. Hivyo kanuni ya kupata GN kwa mwaka wowote ni hii: (MWAKA mod 19 + 1). Yaani, ugawe huo mwaka kwa 19, kisha namba itakayobaki ijumlishe na moja. Ukishaipata GN, itafute kwenye ile chati ambapo utaiona ikiwa na mwezi na tarehe. Jumapili inayofuata baada ya tarehe hii ndiyo tarehe ya Pasaka ya mwaka huo. Tutumie chati ile na kanuni hii kujua tarehe ya Pasaka ya mwaka 1474. GN ni (1474 mod 19 + 1=12). Hivyo GN ni 12. Kwenye chati, 12 inaonyesha ni tarehe 4/4. Hivyo, mwaka 1474 Mwezi-Mkubwa wa Pasaka ulikuwa tarehe 4/4/1474. Hiyo ilikuwa ni Jumatatu. Hivyo Pasaka ilikuwa ni Jumapili iliyofuata yaani tarehe 10/4/1474. Lakini, Kanisa Katoliki liliikubali kanuni hii karne ya sita. Hii ndiyo sababu, tarehe za Pasaka zinazojulikana ni zile tu zinazoanza mwaka 533. Ndivyo Pasaka ilivyotafutwa miaka ile. Sasa tuone Pasaka ya kizazi chetu. Kizazi cha “Gregorean Calender” iliyoanza mwaka 1582. Tumelijadili lile pengo la siku lililofikia ambalo mwaka 1582 lilishafika siku 10. Ukweli ni kwamba kabla halijazibwa, Pasaka ilikuwa inawadia lakini uhalisi ni kwamba inakuwa tayari imepitwa siku 10. Kinyume kabisa na maamuzi ya Kanisa kule Nicaea! Ili kulizuia lisitokee tena, tumeona uchomoaji wa siku moja toka kwenye miaka inayofunga karne, isiyogawanyika kwa 400. Uchomoaji huu umewekwa kwenye kanuni (formula) iitwayo “Solar Equation”. Kama mwendo wa kuzunguka jua umezingatiwa na “Gregorean Calender”, vipi kuhusu mwendo wa mwezi? Tumeuona kwamba mizunguko ya mwezi na dunia hukutana kila baada ya miaka 19. Kadirio la dunia kuzunguka kwa siku 365.25 linafanya ikizunguka kwa miaka 19 zinakuwa siku 6,939.75. Mwezi utakuwa nao umezunguka mara 235, huku kila mzunguko ukitumia siku 29.5305891203704. Hivyo, kukutana kule ndani ya kila miaka 19, huleta pengo dogo la saa 1, dakika 28, sekunde 38.5. Mapengo madogo haya tunayoyapuuza mwanzoni, yameshatugharimu vya kutosha. Pengo hili kwa mwaka ni dogo lakini kwa miaka 2500 linakuwa hadi kufika siku nane. Kwenye hesabu za kutafuta Pasaka urekebishaji wa hili pengo hutokea kwenye kanuni iitwayo “Lunar Equation”. Lakini kwa sababu ya tofauti ya uelekeo wa mzunguko wa mwezi na dunia, “Lunar Equation” hujumlisha mara nane kila baada ya miaka 2500. Hivyo, mahesabu yoyote ya kuitafuta tarehe ya Pasaka hayakosi kanuni hizi mbili “Solar Equation” na “Lunar Equation” . Tumeona kwamba kalenda ilianza mwaka 1582. “Solar Equation” inaondoa siku moja toka kwenye miaka 1700, 1800, 1900. Hivyo, ni kujidanganya kusema kwamba miaka yote inayogawanyika kwa nne ni mirefu, jambo ambalo hata mimi nilifundishwa shuleni. Hapa tumeona kwamba “Solar Equation” imeondoa siku moja kwenye mwaka 1900 na hivyo haukuwa mwaka mrefu ingawa unagawanyika kwa nne. “Lunar Equation” huongeza siku moja kwenye miaka 1800, 2100, 2400. Mwaka 1800 unaguswa na vyote “Solar Equation” na “Lunar Equation”. Hivyo hauathiriki. Kanuni zote za kuitafuta Pasaka huzingatia zaidi ya niliyoyaeleza, lakini cha muhimu zaidi ni hizi mbili yaani “Solar Equation” na “Lunar Equation” ambazo sijawahi kuzisikia kwa kiswahili. Ni vigumu kuepuka hesabu za “modulo” au “mod” unapotafuta tarehe ya Pasaka. Lakini ukiwauliza wanafunzi wa darasa la nne kwamba machungwa 2011 yakipangwa kwenye mafungu 19, ni mangapi yatakosa fungu? Wapo watakaopata jibu sahihi kwamba ni machungwa 16. Kimahesabu swali hilo linaandikwa hivi: (2011 mod 19) na jibu lake ni 16, yaani (2011 mod 19=16). Ifuatayo ni moja ya kanuni zinazotumika kuipata tarehe za Pasaka ya mwaka wowote kuanzia 1700 hadi 2099: (1) : a=MWAKA mod 19; (2) : b=MWAKA \ 100; (3) : c=MWAKA mod 100; (4) : d=b \ 4; (5) : e=b mod 4; (6) : f=c \ 4; (7) : g=c mod 4; (8) : h=(b + 8)\25; (9) : i=(b – h + 1)\3; (10) : j=(19xa + b – d – i + 15) mod 30; (11) : k=(32 + 2xe + 2xf – j – g) mod 7; (12) : m=(a + 11xj + 22xk) \ 451; (13) : n=j + k – 7xm + 114; (14) : Tarehe=(n mod 31) + 1 (15) : Mwezi =n\31; Penye neno MWAKA, andika mwaka unaotafuta kujua tarehe yake ya Pasaka. Panapotokea alama (\) ni kugawanya ambako hata kama jibu litaleta desimali, basi hiyo desimali unatakiwa kuachana nayo ili jibu libaki namba nzima. Penye alama (x) hiyo ni ya kuzidisha. Yafuatayo ni majibu niliyopata kwa hatua zote baada ya kuuingiza mwaka 2015 ili kujua siku ya Pasaka ya mwaka huu: (1): 1, (2): 20, (3): 15, (4): 5, (5): 0, (6): 3, (7): 3, (8): 1, (9): 6, (10): 13, (11): 1, (12): 0, (13): 128, (14): 5, (15): 4. Tarehe imepatikana kwenye hatua ya 14 ambako jibu ni “5”. Mwezi umepatikana kwenye hatua ya 15 ambako jibu ni “4”. Hivyo Pasaka ya mwaka (2015) huu ni Tarehe 5, mwezi wa 4. Hivyo, kwa njia hii, unaweza kujua tarehe za Pasaka kwa miaka ijayo kama unavyoijua tarehe ya Krismas. Kama kuna tukio lilifanyika siku ya Pasaka miaka iliyopita na hukumbuki tarehe, basi tumia kanuni hii. Zifuatazo ni siku zinazoitangulia Pasaka kwa idadi ya siku zilizoandikwa kwenye mabano: Jumatano Ya Majivu (46), Jumapili ya Matawi (7), Ijumaa Kuu (2). Zinazotanguliwa na Pasaka ni hizi zifuatazo: Kupaa (42), Pentekoste (49), Utatu Mtakatifu (56), Ekaristi (63). Mwanzo tuliona kwamba Mwezi-Mkubwa wa Pasaka au “Ecclesiastical full Moon” ni ule wa March 22 hadi April 18. Ukitokea March 22 basi kuna uwezekano siku hiyohiyo ikawa Pasaka na ikawa imevunja rekodi ya kuwahi mapema. Ukitokea April 18, kuna uwezekano wa Pasaka kuwa siku saba zaidi ya hapa yaani April 25, na hiyo ikawa ni tarehe ya juu mno ya Pasaka. Hivyo, Pasaka yoyote haiwezi kuwa chini ya Machi 22, wala haiwezi kuwazaidi ya April 25. Pasaka tuliyoiona mwaka 2008 ndiyo ya mwisho kwa kizazi chetu kuiona ikiwahi mapema kiasi kile, kwani ilitokea Machi 23 na itairudia tena tarehe hiyo mwaka 2160! by JOSEPH MAGATA
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Thomas Mwakalindile (Guest) on June 8, 2024

Imani inaweza kusogeza milima

Michael Mboya (Guest) on May 26, 2024

Sifa kwa Bwana!

Edward Lowassa (Guest) on February 1, 2024

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

James Malima (Guest) on December 18, 2023

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Joseph Kawawa (Guest) on December 11, 2023

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Lydia Mahiga (Guest) on November 27, 2023

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

John Lissu (Guest) on October 1, 2023

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Irene Akoth (Guest) on July 2, 2023

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Ann Wambui (Guest) on March 11, 2023

Mungu ni mwema, wakati wote!

Vincent Mwangangi (Guest) on February 19, 2023

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Francis Mrope (Guest) on October 18, 2022

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

David Musyoka (Guest) on June 11, 2022

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Peter Mwambui (Guest) on April 6, 2022

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Michael Onyango (Guest) on January 24, 2022

Tumaini ni nanga ya roho

Simon Kiprono (Guest) on September 16, 2021

Endelea kuwa na imani!

Anna Mchome (Guest) on May 27, 2021

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Benjamin Kibicho (Guest) on April 30, 2021

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Agnes Lowassa (Guest) on April 6, 2021

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Lucy Kimotho (Guest) on February 8, 2021

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Richard Mulwa (Guest) on February 4, 2021

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Tabitha Okumu (Guest) on August 31, 2020

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Grace Njuguna (Guest) on August 27, 2020

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

James Malima (Guest) on May 11, 2020

Rehema hushinda hukumu

Anna Mchome (Guest) on April 11, 2020

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Fredrick Mutiso (Guest) on April 4, 2020

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Esther Nyambura (Guest) on March 11, 2020

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Peter Mugendi (Guest) on February 18, 2020

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Alex Nakitare (Guest) on January 29, 2020

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Alice Wanjiru (Guest) on June 25, 2019

Mwamini katika mpango wake.

Lydia Mahiga (Guest) on March 10, 2019

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Charles Mchome (Guest) on January 6, 2019

Katika imani, yote yanawezekana

David Nyerere (Guest) on December 16, 2018

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Mariam Kawawa (Guest) on August 29, 2018

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Samuel Were (Guest) on August 8, 2018

Dumu katika Bwana.

Anthony Kariuki (Guest) on March 18, 2018

Neema na amani iwe nawe.

Mary Mrope (Guest) on October 28, 2017

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Frank Sokoine (Guest) on September 4, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Sharon Kibiru (Guest) on August 11, 2017

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

John Mwangi (Guest) on August 1, 2017

Nguvu hutoka kwa Bwana

Elizabeth Mrema (Guest) on July 24, 2017

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Lydia Mutheu (Guest) on May 19, 2017

Mwamini Bwana; anajua njia

Samuel Omondi (Guest) on July 17, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Charles Mrope (Guest) on July 12, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Nora Lowassa (Guest) on June 8, 2016

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

David Chacha (Guest) on January 9, 2016

Nakuombea 🙏

Ann Wambui (Guest) on October 27, 2015

Mungu akubariki!

Anna Mahiga (Guest) on August 24, 2015

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Violet Mumo (Guest) on August 18, 2015

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Patrick Mutua (Guest) on April 25, 2015

Rehema zake hudumu milele

Grace Mligo (Guest) on April 19, 2015

Baraka kwako na familia yako.

Related Posts

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili? Ji... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu tofauti za kijamii na uadilifu wa kijamii?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu tofauti za kijamii na uadilifu wa kijamii?

Kanisa Katoliki limekuwa likitetea uadilifu wa kijamii na tofauti za kijamii kama sehemu ya imani... Read More

Usipite bila kusoma kisa hiki cha kusisimua

Usipite bila kusoma kisa hiki cha kusisimua

Siku moja jioni katika mji flani, kulikuwa na basi likisafiri kutoka mji huo kuelekea mji mwingin... Read More

JE, WAKATOLIKI WANABUDU SANAMU?

JE, WAKATOLIKI WANABUDU SANAMU?

Read More
Ufalme wa simu wa sasa

Ufalme wa simu wa sasa

➡ Asubuhi saa 12 : 00 mtu anaamka, kabla hata HAJAMUSHUKURU MUNGU, kabla hata hajatoka kitandan... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Ndoa?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Ndoa?

Sakramenti ya Ndoa ni muhimu sana katika Kanisa Katoliki. Kwa mujibu wa imani ya Kanisa, ndoa ni ... Read More

Huruma ya Mungu: Ulinzi na Uongozi katika Maisha

Huruma ya Mungu: Ulinzi na Uongozi katika Maisha

Huruma ya Mungu: Ulinzi na Uongozi katika Maisha

Katika maisha yetu, tunaenda kupitia chan... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Roho Mtakatifu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Roho Mtakatifu?

Katika Kanisa Katoliki, Roho Mtakatifu ni Mungu mmoja katika Utatu Mtakatifu (Baba, Mwana, na Roh... Read More

Njia Kuu 3 za Kuiishi Huruma ya Mungu

Njia Kuu 3 za Kuiishi Huruma ya Mungu

Read More
Kanuni ya Mungu kuhusu mema

Kanuni ya Mungu kuhusu mema

Read More
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya watoto wachanga?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya watoto wachanga?

Katika Kanisa Katoliki, watoto wachanga ni baraka kubwa kutoka kwa Mungu. Imani yetu inaamini kuw... Read More

Mafundisho (Dogma) ya Kanisa Katoliki kuhusu Bikira Maria

Mafundisho (Dogma) ya Kanisa Katoliki kuhusu Bikira Maria

Read More