Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Maana halisi ya kuolewa au ya kuwa mke

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

NDOA sio kichaka cha kujificha kukimbia matatizo. NDOA sio mahali pa kutolea mkosi. Wala sio mahali pa kupunguzia shida. Ndoa sio mbadala wa elimu na michakato ya kimaisha. Huolewi ili kupunguza adha za maisha. NDOA ni jukumu zito kuliko hata kusoma masters degree ya Neuro-surgeon. Wengi hamjaweza kumudu maisha yenu binafsi na bado mnalilia Mungu kuwaongezea jukumu la kumeneji maisha ya mtu mwingine.

Kama huwezi hata kujitafutia hela ya kusuka nywele zako utawezaje kuendesha maisha ya familia. Maana unaweza kuolewa na mwanaume mwenye pesa lakini akapitia mithihani pesa zikatoweka utafanyaje kama huna akili ya kujiongeza? Ndio maana wengi mnawakataa watu wenye Ndoto lakini hawanapesa kwa sasa kwa sababu ya akili ya utegemezi. Unataka mwanaume mwenye kila kitu, sababu kubwa ni uvivu na uzembe. Hutaki kujitafutia vya kwako.
Ukisoma MITHALI 31 inaeleza habari za MKE MWEMA.

Hapo ndio pa kujipima je unakidhi hivyo viwango? Mke mwema sio tegemezi ila ni mwanamke mwenye uhuru wa kifedha (Financial Freedom). JIULIZE TU KAMA IKITOKEA HUJAOLEWA MIAKA MITANO IJAYO UTAKUWAJE? MAISHA YAKO YATAKUWAJE? UTAKUWA NA HALI GANI? Maswali kama haya yatakusaidia kujiongeza. Tafuta kitu cha kufanya hata kama Ndoa isipotokea leo isiwe mwisho wa maisha, Ndoto na maono yako. Siku hizi wanaume hawaulizi ukoo wanauliza UNAFANYA NINI?

Mtu anapiga hesabu akikuoa mkaunganisha nguvu mtafanya nini kwenye maisha. Sasa wewe kalia kubandika kope na kuchora kucha kutwa nzima huna shughuli ya kufanya huku ukingoja kuombewa upate Mume. Watu hawaoi mapambo wanataka Wake watakao tengeneza nao hatma zao. Pambo ni kwaajili ya Starehe lakini MKE ni kwaajili ya maisha. Sikupondi wala sio nia yangu kukuvunja moyo, nataka utoke hapo ulipo ujiongeze ili hata ukiingia kwenye Ndoa isijae visa na kuonewa. Pesa itakupa heshima, pesa inakupa sauti, hata Wakwe zako hawawezi kukunyanyasa ukiwa na pesa kwani wanajua watakosa vitenge.

Nataka nikwambie kweli, ukiwa na hela utachagua mwanaume wa kukuoa kwani wapo wengi ila kama umefulia, tegemezi kweli utaona wanaume ni wachache. Pata kitu cha kufanya, tengeneza milango ya kipato. Badala ya kukesha unaomba Mungu akupe Mume anza kuomba Mungu akupe uhuru wa kifedha, kama itakubidi kurudi shule rudi tu. Jiongeze usibaki hapo ulipo. Ni Yesu peke yake asiyebadilika (Hebrania 13) Lakini wanadamu wote lazima tubadilike kila kukicha tukihama hatua moja kwenda nyingine.

Mungu akufungue macho kuona kiini cha ujumbe huu na lengoF lake na wala usichukuliwe na upepo wa adui upindishao maana katika jumbe zenye kubadilisha maisha kama hii.

Kuolewa sio mwisho wa maisha, Mungu kwanza achukue nafasi kwenye maisha yako na akupe utoshelevu katika moyo wako kiasi kwamba uone hata bila Mume unaweza kuishi.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest May 19, 2024
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Mar 6, 2024
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Mar 5, 2024
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Feb 18, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Oct 20, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Oct 9, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Sep 3, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Aug 26, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Aug 14, 2023
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Jun 10, 2023
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest May 8, 2023
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ David Chacha Guest Feb 11, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ John Lissu Guest Feb 1, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Nov 18, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Oct 3, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Jun 9, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest May 4, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Mar 12, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Jan 20, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Nov 15, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ James Malima Guest Sep 9, 2021
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Sep 3, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Aug 10, 2021
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Jul 26, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Apr 14, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Mar 10, 2021
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Jan 8, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Sep 27, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Sep 7, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest May 20, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Mar 13, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Dec 29, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Dec 1, 2019
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest May 16, 2019
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Dec 16, 2018
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Sep 9, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Apr 9, 2018
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ George Mallya Guest Oct 5, 2017
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Jun 11, 2017
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Mar 10, 2017
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Sep 8, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Sep 2, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Aug 16, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Jun 21, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest May 23, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Apr 4, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest Feb 29, 2016
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ James Mduma Guest Feb 18, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ George Wanjala Guest Jan 5, 2016
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Aug 12, 2015
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About