Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Kwa nini Wakatoliki wanaungama dhambi kwa Padri?

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
KWANINI NYIE WAKATOLIKI MNAUNGAMA DHAMBI KWA PADRE AMBAYE NI MWANADAMU NA MDHAMBI BADALA YA KUUNGAMA MOJA KWA MOJA KWA MUNGU?
Pengine umewahi kuulizwa swali hili au umewahi kujiuliza: hapa ni maelezo yatayokusaidia kuelewa sababu (japo sio zote) na uhalali wa jambo hilo.
Hapa tunaongozwa na maneno ya Bwana Yesu mwenyewe alipotoa amri hiyo kwa mitume wake akisema;
"Pokeeni Roho Mtakatifu.wowote mtakaowaondolea dhambi wameondolewa na wowote mtakaowafungiwa dhambi wamefungiwa"(Yohane 20:22-23).
Na huo ndio utaratibu wetu tangu mwanzo wa kanisa wa mitume.
"Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana mpate kuponywa"(Yakobo 5:16a)
Ni miongoni mwa maagizo msingi kabisa ambayo hatuna mamlaka kuyabadili labda Yesu mwenyewe aliyeagiza hivyo aje mwenyewe kuyabadilisha.
Mungu anayesamehe dhambi ndiye aliyechagua njia ya kutoa msamaha huo,sisi tu nani tumpangie njia ya kutoa msamaha huo na kujipangia njia zetu?je tunamfundisha Mungu kazi?
Inashangaza siku hizi kusikia kwamba hata baadhi ya wakatoliki wameanguka katika mtego huu wa kutaka kubadilisha agizo hili la Yesu na inashangaza ni kwanini wanataka kurahisisha mambo kiasi hicho.
Mungu hafanyi kazi zake hewani bali huzifanya kupitia kwa watu wake.
Tunapoomba msamaha tunategemea kusikia maneno kama vile "nimekusamehe",hutaka kuamini kwamba mtu akinyamaza au akiongea kimoyomoyo basi amekusamehe.
Yesu kwa kujua umuhimu na kazi ya neno hilo,alilitumia yeye mwenyewe akiwa binadamu(Luka 7:48).
Luka 7:48
"Naye Yesu akamwambia yule mwanamke,umesamehewa dhambi zako"
na alitaka aendelee kulitumia hata utimilifu wa dahari katika hali ya kibinadamu,ndio maana aliwaachia binadamu baada ya kifo chake ili waendeleze kazi hiyo.
Kuondolea watu dhambi ni moja ya utume wa Yesu(Marko 2:10),ni pamoja na kazi hiyo aliwaachia mitume wake(Yohane 20:23).
Tukilinganisha na mfano wa mtume Petro baada ya kumkana Bwana,tunaweza kujifunza kwamba tunapoongea na Mungu peke yetu ni katika hali ya toba na majuto(Luka 22:61-62).
Luka 22:61-62
"Bwana akageuka na kumtazama Petro,naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana 'leo kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu' hapo akatoka nje,akalia sana."
Hivyo bado tunadaiwa kuungama iki kuondolewa dhambi zetu(Yohane 21:15-17)
Chakushangaza ni kwamba,Wakristo wote tunaamini kwamba Sakramenti ya ubatizo inatuondolea kabisa dhambi ya asili na dhambi zote zikizowahi kutendwa na yule anayebatizwa na kwa kawaida huwa hatujibatizi wenyewe wala hatubatizwi moja kwa moja na Mungu moja bali hubatizwa na wanadamu wenzetu.
Sasa kama huyu mwanadamu mwenzetu anatubatiza na anatuondolea dhambi ya asili na wote tunasadiki hivyo iweje tukija kwenye kitubio tunapinga ushiriki wa binadamu mwenzetu na wakati matokeo yanayotarajiwa katika sakramenti hizo ni yaleyale kama ya ubatizo.
Iweje aliyekubatiza na kukuondolea dhambi ya asili na ukaamini kwamba amekuondolea ashindwe au ushindwe kusadiki ushiriki wake katika kitubio?
Iweje akisema "Nakubatiza kwa JINA LA BABA NA LA MWANA NA LA ROHO MTAKATIFU" hiyo iwe sahihi lakini akisema "Nakuondolea dhambi zako KWA JINA LA BABA NA LA MWANA NA LA ROHO MTAKATIFU" iwe sio sahihi?
Sasa huoni kama unajipinga na kujichanganya mwenyewe hapo?
Wapendwa,tuache kutafuta visingizio visivyo na ukweli kwaajili ya kutaka kupindisha ukweli.
Anayekuondolea dhambi ni Mungu mwenyewe kupitia kwa wapakwa mafuta wake yaani mapadre ambao amewaweka mwenyewe kwaajili ya huduma ya kanisa lake.
Wengine hudai pia kwamba ni watu wote waliopewa jukumu hilo na sio mapadre pekee,lakini ni vizuri kwanza kabla hujajitetea kwa msimamo huo dhaifu uchunguze tofauti iliyopo kati ya "Wanafunzi" na "wafuasi" kisha usome Biblia yako na kuona je jukumu hilo Yesu aliwatamkia wanafunzi wake au aliwatamkia wafuasi wake.
Wanafunzi wa Yesu ni wale kumi na wawili walioandamana naye.
Wafuasi ni wale makutano wengi waliokuwa wakimfuata kwaajili ya kusikiliza mafundisho yake.
Ikumbukwe kwamba Yesu hakusema mambo yote hadharani mbele ya makutano,baadhi ya maagizo msingi kama haya aliwachagua watu maalum kwaajili ya kuwapa kazi hizo na Biblia inasema aliwaita faragha peke yao na kuwapa maagizo hayo.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 George Mallya Guest Mar 10, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 John Mwangi Guest Feb 14, 2024
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Joseph Njoroge Guest Feb 3, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Samuel Were Guest Aug 21, 2023
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Alex Nakitare Guest Aug 8, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Grace Minja Guest May 13, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Philip Nyaga Guest Mar 26, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Patrick Kidata Guest Feb 16, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Peter Mwambui Guest Dec 29, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Nora Lowassa Guest Dec 4, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 George Mallya Guest Dec 1, 2022
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Raphael Okoth Guest Nov 23, 2022
Endelea kuwa na imani!
👥 Frank Macha Guest Oct 29, 2022
Baraka kwako na familia yako.
👥 Edward Lowassa Guest Aug 28, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Janet Mwikali Guest Jun 17, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Grace Mligo Guest Nov 9, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Lucy Mahiga Guest Oct 11, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 David Chacha Guest Oct 10, 2021
Dumu katika Bwana.
👥 Edwin Ndambuki Guest Jun 7, 2021
Neema na amani iwe nawe.
👥 Nicholas Wanjohi Guest Mar 16, 2021
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Agnes Lowassa Guest Feb 20, 2021
Nakuombea 🙏
👥 David Kawawa Guest Nov 2, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Samson Tibaijuka Guest Sep 22, 2020
Mungu akubariki!
👥 John Lissu Guest Sep 9, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Moses Kipkemboi Guest Aug 28, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Nancy Kabura Guest Aug 8, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Nancy Kabura Guest Jun 27, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Rose Lowassa Guest Jun 27, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Michael Onyango Guest Dec 7, 2019
Sifa kwa Bwana!
👥 Mary Sokoine Guest Oct 20, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Isaac Kiptoo Guest May 19, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 John Mushi Guest Apr 17, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Benjamin Masanja Guest Mar 27, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Margaret Mahiga Guest Sep 10, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Victor Malima Guest May 7, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Fredrick Mutiso Guest Apr 1, 2018
Rehema zake hudumu milele
👥 Alice Wanjiru Guest Oct 16, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Sarah Mbise Guest Sep 15, 2017
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Lucy Mahiga Guest Aug 23, 2017
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Isaac Kiptoo Guest Aug 21, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Michael Mboya Guest Jun 14, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 John Malisa Guest Feb 28, 2017
Mwamini katika mpango wake.
👥 John Mwangi Guest Jan 12, 2017
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Charles Mrope Guest Jan 2, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Grace Mushi Guest Sep 3, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Michael Onyango Guest May 30, 2016
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Peter Mbise Guest Mar 18, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Kenneth Murithi Guest Nov 19, 2015
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Nora Lowassa Guest Aug 17, 2015
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Thomas Mwakalindile Guest Jul 14, 2015
Rehema hushinda hukumu

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About