BADILIKA: Anza kupiga hatua ya maendeleo sasa

โœ๏ธ SW - Melkisedeck Shine๐Ÿ“… 2016-09-10 11:12:00๐Ÿ’ฌ 0 commentsโฑ๏ธ ~1 min read
๐Ÿ“„ PDF

Ili kutoka hapo ULIPO uweze kwenda HATUA inayofuata kuna SWALI muhimu sana unahitaji kujiuliza.
Watu ambao huwa wanashindwa kupiga hatua katika maisha yao ni kwa sababu huwa wanajiuliza kinyume cha swali hili.
Swali hili ndilo wanalojiuliza watu wote waliofanikiwa:

Swali: "Hivi kwa sasa nina nini ambacho naweza kuanza kukitumia kama mtaji wa kwanza kuanza kufanya ninachotaka"?

Siku moja wakati nasoma biblia niliona Mungu alipotaka kumtumia Mussa kuokoa wana wa Israel akamuuliza-

โ€œUna nini mkononi mwakoโ€-

Mussa akajibu
kwa kudharau alichonacho kuwa โ€œNina fimbo kavu tu ya kuchungia mifugoโ€.

Ndipo Mungu alianza kumuonyesha miujiza kutumia fimbo ambayo siku zote
alikuwa nayo na kujidharau ndiyo ambayo ikatumika kwenda kuokoa wana wa Israel.

Watu wengi sana wanashindwa kuanza kwa sababu huwa wanajiuliza-

"Hivi ninakosa nini ili niweze kuanza"
badala ya 'Hivi nina nini cha kuanzia'.

Cha kuanzia sio lazima iwe pesa-Inawezekana ni uwezo wa kufanya jambo fulani la kipekee,inawezekana ni
mahusiano mazuri uliyonayo na watu fulani(mtandao wako),inawezekana ni uzoefu ulionao,inawezekana ni kipaji n.k
Leo unapoanza siku yako naomba ijiulize-

โ€œNina nini mkononi mwangu ambacho naweza kutumia katika
hatua ya kwanzaโ€?.

Kumbuka hakuna mtu ambaye hana
kitu kabisa-KITAFUTE HADI UKIPATE NA ANZA KUKITUMIA KUCHUKUA HATUA.

Share ili wengine wajifunzeโ€ฆ..uwe na Jumatatu njemaโ€ฆโ€ฆ..

๐Ÿ’ฌ

Discussion

Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.

0 comment(s)
๐Ÿ” Login required to comment or reply

You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.

Log in to participate
No comments yet.