Jinsi ya kutengeneza Labania Za Maziwa

✍️ SW - Melkisedeck ShineπŸ“… 2022-07-26 22:28:54πŸ’¬ 0 comments⏱️ ~1 min read
πŸ“„ PDF

MAHITAJI

Maziwa ya unga - 2 vikombe

Sukari - 3 vikombe

Maji - 3 vikombe

Unga wa ngano - Β½ kikombe

Mafuta - Β½ kikombe

Iliki - kiasi

MAPISHI

Paka sinia mafuta kabla ya kupika labania
Katika sufuria chemsha maji na sukari pamoja na iliki mpaka inate vizuri
Kisha mimina mafuta koroga
Halafu mimina unga wa ngano na ukoroge haraka haraka
Kisha tia unga wa maziwa, endelea kukoroga usiwe na madonge mpaka uwe rangi ya browni isiokoleza.
Kisha mimina mchanganyiko kweye sinia uliyoipaka mafuta, iwache ipoe na kata kata upendavo na itakuwa tayari.

πŸ’¬

Discussion

Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.

0 comment(s)
πŸ” Login required to comment or reply

You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.

Log in to participate
No comments yet.