VIAMBAUPISHI
Unga - 3 mug za chai
Samli - Β½ mug ya chai
Maziwa - 1ΒΌ mug ya chai
Baking powder - 2 vijiko vya chai
VIAMBAUPISHI VYA MJAZO
Njugu zilizomenywa vipande vipande - 2 vikombe cha chai
Sukari - Β½ kikombe cha chai
Iliki - 1 kijiko cha chai
Nazi iliyokunwa - 2 vikombe vya chai
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari - 2 vikombe vya chai
Maji - 1 kikombe cha chai
Ndimu - 1
JINSI YA KUVIANDAA
1-Changanya unga na samli kisha tia baking powder na maziwa. Ukande ulainike kisha
uwache kama dakika 5 uumuke.
2-Kwenye bakuli nyingine changanya njugu, sukari na iliki.
3-Kata madonge madogo dogo sukuma kila donge duara jembamba, kisha tia kijiko cha mchanganyiko wa njugu juu yake ifunikie juu yake na ibane pembeni.
4-Panga kwenye treya isiyoganda (non stick) kisha choma kwenye oven kwa moto wa chini
(bake) 350Β° C kwa dakika kama 15-20.
5-Chemsha maji na sukari katika sufuria ndogo kisha tia ndimu acha ichemke mpaka inatenate unapoigusa.
6-Kwenye sahani ya chali mimina nazi iliyokunwa.
7-Vibiskuti vikiwa tayari vya motomoto chovea kwenye shira kisha zungushia katika nazi iliyokunwa,
panga kwenye sahani tayari kwa kuliwa.






Discussion
Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.
You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.
Log in to participate