VIAMBAUPISHI
Unga - 3 mug za chai
Samli - ยฝ mug ya chai
Maziwa - 1ยผ mug ya chai
Baking powder - 2 vijiko vya chai
VIAMBAUPISHI VYA MJAZO
Njugu zilizomenywa vipande vipande - 2 vikombe cha chai
Sukari - ยฝ kikombe cha chai
Iliki - 1 kijiko cha chai
Nazi iliyokunwa - 2 vikombe vya chai
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari - 2 vikombe vya chai
Maji - 1 kikombe cha chai
Ndimu - 1
JINSI YA KUVIANDAA
1-Changanya unga na samli kisha tia baking powder na maziwa. Ukande ulainike kisha
uwache kama dakika 5 uumuke.
2-Kwenye bakuli nyingine changanya njugu, sukari na iliki.
3-Kata madonge madogo dogo sukuma kila donge duara jembamba, kisha tia kijiko cha mchanganyiko wa njugu juu yake ifunikie juu yake na ibane pembeni.
4-Panga kwenye treya isiyoganda (non stick) kisha choma kwenye oven kwa moto wa chini
(bake) 350ยฐ C kwa dakika kama 15-20.
5-Chemsha maji na sukari katika sufuria ndogo kisha tia ndimu acha ichemke mpaka inatenate unapoigusa.
6-Kwenye sahani ya chali mimina nazi iliyokunwa.
7-Vibiskuti vikiwa tayari vya motomoto chovea kwenye shira kisha zungushia katika nazi iliyokunwa,
panga kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
No comments yet. Be the first to share your thoughts!