Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

Jinsi ya kupika Keki Ya Maboga

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Viamba upishi

Unga wa ngano vikombe vikubwa 3
Boga lililopondwa kikombe 1
Baking powder vijiko vidogo
Sukari kikombe kikubwa 1
Blue band kikombe ยฝ
Vanilla kijiko kidogo 1
Mayai 2
Maji kiasi/ maziwa
(kama nilazima)

Hatua

โ€ข Osha boga, Kata, ondoa mbegu, kisha kata vipande vikubwa, chemsha na maji mpaka vilainike.
โ€ข Kwangua boga la ndani ukiacha maganda na ponda sawasawa.
โ€ข Chekecha unga (kila kikombe 1, vijiko vidogo 2 vya baking powder) kwenye bakuli kubwa.
โ€ข Ongeza blue band na changanya sawasawa na vidole.
โ€ข Ongeza sukari na changanya.
โ€ข Ongeza mayai na koroga na mwiko.
โ€ข Ongeza boga lililopondwa na koroga njia moja mpaka ilainike.
โ€ข (Kama haikulainika ongeza yai /mayai au maziwa/ maji kidogo).
โ€ข Ongeza vanilla na koroga.
โ€ข Paka mafuta chombo cha kuokea au sufuria kisha chekecha unga kidogo wa ngano.
โ€ข Mimina rojo la keki kwenye sufuria au chombo cha kuokea.
โ€ข Oka kwenye oven au tumia sufuria na weka mkaa wa moto juu na chini moto kidogo mpaka iive.
โ€ข Jaribu kuchoma kisu katikati, kama ni kavu keki imeiva, epua, pozesha kata tayari kwa kula, kama kitafunio.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 0

Please log in or register to comment or reply.
No comments yet. Be the first to share your thoughts! ๐Ÿ“

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About