Viambaupishi
Siagi 100gm
Unga wa kaukau (cocoa powder) 2 Vijiko vya supu
Maziwa mazito (condensed milk) Moja kikopo (397gm)
Bisikuti za Mary 2 Pakiti
Njugu Β½ Kikombe
Karatasi la plastiki
Jinsi ya kuandaa na kupika
1. Vunjavunja bisikuti zote packet mbili ziwe vipande vidogo vidogo.
2. Pasha moto siagi mpaka ipate.
3. Tia kwenya siagi imoto maziwa mazito na cocoa koroga vizuri.
4. Kisha tia kwenye mchanganyiko bisikuti zilizovunjwa na njugu na uchanganye kisha epua motoni.
5. Paka karatasi la plastiki mafuta kidogo halafu tia mchanganyiko kisha kunja (roll).
6. Tia kwenye freeza muda wa saa.
7. Halafu toa karatasi na ukate kate na panga kwenye sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa.







Discussion
Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.
You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.
Log in to participate