Vipimo
Wali:
Mchele - 3 Vikombe
Kitunguu kiichokatwa - 1
Pilipili boga nyekundu iliyokatwa vipande - 1
Mafuta - ยผ Kikombe
Zaafarani - 1 kijiko cha chai tia kwenye kikombe na maji robo roweka
Chumvi - 1 kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katika sufuria, tia mafuta, kaanga kitunguu mpaka kiwe kidogo rangu ya udongo (brown)
Tia pili pili boga.
Tia mchele, kaanga kwa muda wa dakika 3, tia zaafarani na chumvi.
Tia supu uliyochemshia kuku iwe imoto.
Pika wali katika moto mdogo hadi uwive.
Kuku
Kuku Mzima -1
Mayai ya kuchemsha - 6
Namna Ya Kupika Kuku
Mchemshe kuku mzima na chumvi mpaka uhakikishe ameiva vizuri.
Mtowe na muweke pembeni. Supu yake tumia katika wali kama ilivyo hapo juuu.
Chemsha mayai, menya na kata vipande viwili kila yai moja weka kando
Vipimo Vya Sosi Ya Kuku Ya Nazi
Kitunguu - 1
Nyanya iliyokatwa vipande - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi - 1 kijiko cha supu
Garam Masala - ยฝ kijiko cha supu
Bizari ya manjano - ยฝ kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Pilipili masala ya unga - ยฝ kijiko cha chai
Nyanya ya kopo - 1 kijiko cha supu
Nazi ya unga - 1 kikombe
Maji ya ukwaju - ยผ kikombe cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Tia Mafuta vijiko 2 vya supu katika sufuria
Kaanga kitunguu maji mpaka kiwe rangi ya udongo (brown).
Tia thomu na tangawizi.
Tia nyanya nzima iliyokatwa katwa.
Tia garam masala, manjano, pilipili ya unga, nyanya ya kopo, kaanga vizuri.
Changanya kwenye sufuria na ukwaju. Iache ichemke vizuri.
Changanya nazi ya unga na maji vikombe viwili.
Mtie kuku mpike vizuri na hilo tui.
Mtie kwenye oveni kidogo.
Kupakuwa katika Sinia
Pakuwa wali kwanza katika sinia
Muweke kuku juu ya wali.
Pambia mayai
No comments yet. Be the first to share your thoughts!