Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/mobile/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakushukuru, ee Mungu, kwa mapaji uliyotujalia leo. Amina.

Baba yetu …

Salamu Maria …

SALA YA IMANI

Mungu wangu, nasadiki maneno yote. Linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma. Kwani ndiwe uliyetufumbulia hayo. Wala hudanganyiki, wala hudanganyi. Amina.

SALA YA MATUMAINI

Mungu wangu, natumaini kwako, nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo. Neema zako hapa duniani, na utukufu mbinguni. Kwani ndiwe uliye agana hayo nasi, nawe mwamini. Amina.

SALA YA MAPENDO

Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote. Kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu, kama nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.

KUTUBU DHAMBI

Tuwaze katika moyo wetu makosa ya leo tuliyomkosea Mungu kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo na kwa kutotimiza wajibu. (Husubiri kidogo ).

Nakuungamia Mungu Mwenyezi, nanyi ndugu zangu, kwani nimekosa mno, kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa kutotimiza wajibu.
Nimekosa mimi, nimekosa mimi, nimekosa sana. Ndiyo maana nakuomba Maria mwenye heri, Bikira daima, Malaika na Watakatifu wote, nanyi ndugu zangu, niombeeni kwa Bwana Mungu wetu.
Mungu Mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu, atufikishe kwenye uzima wa milele. Amina.

SALA YA KUWAOMBEA WATU

Ee Mungu, nawaombea watu wa nchi hii, wapate kusikia maneno yako na kukupenda wewe Bwana Mungu wetu.

SALA KWA MALAIKA MLINZI

Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina.

MALAIKA WA BWANA

(kipindi kisicho cha Pasaka)
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria.
Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Salamu, Maria,…..
Ndimi mtumishi wa Bwana.
Nitendewe ulivyonena.
Salamu, Maria….
Neno la Mungu akatwaa mwili.
Akakaa kwetu.
Salamu, Maria….
Utuombee, Mzazi mtakatifu wa Mungu.
Tujaliwe ahadi za Kristu.
Tuombe:
Tunakuomba, Ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika kwamba Mwanao amejifanya Mtu kwa mateso na msalaba wake tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. AMINA.

AU;

MALKIA WA MBINGU (kipindi cha Pasaka)

Malkia wa mbingu, furahi, aleluya.
Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya.
Amefufuka alivyosema, Aleluya.
Utuombee kwa Mungu, Aleluya.
Furahi shangilia, ee Bikira Maria, Alaluya.
Kwani hakika Bwana amefufuka Aleluya.
Tuombe.
Ee Mungu, uliyependa kuifurahisha dunia kwa kufufuka kwake Bwana wetu Yesu Kristu, Mwanao, fanyiza, twakuomba, kwa ajili ya Bikira Maria, tupate nasi furaha za uzima wa milele. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina.

ATUKUZWE (mara tatu)
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.

KUJIKABIDHI

Enyi Yesu, Maria na Yosefu nawatolea moyo na roho na uzima wangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijilie saa ya kufa kwangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijalie nife mikononi mwenu!

(Rehema ya siku 300).

WIMBO:

Kwa heri Yesu mpenzi mwema,
Naenda usiudhike mno.
Nakushukuru, nakupenda,
Kwa hizo nyimbo za mwisho.
Asubuhi nitarudi.
Yesu kwa heri.

Kwa heri Mama mtakatifu,
Sasa napita pumzika.
Asante kwa moyo na nguvu,
Leo umeniombea.
Asubuhi nitarudi.
Mama kwa heri.

Kwa heri Yosefu mnyenyekevu,
Kazi zatimilizika.
Kama mchana, leo usiku,
Nisimamie salama.
Asubuhi nitarudi.
Yosefu kwa heri.

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

KUOMBA ULINZI WA USIKU

Mungu wangu naenda kulala naomba malaika 14, waende nami, wawili juu, wawili chini, wawili upande wa kuume, wawili upande wa kushoto, wawili wanifunike, wawili waniamshe, wawili wanipeleke juu mbinguni. Mimi mtoto mdogo, roho yangu ni ndogo, haina nafasi kwa mtu yoyote ila kwa Yesu pekee. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Ruth Wanjiku (Guest) on February 16, 2018

Mwamini katika mpango wake.

Stephen Kikwete (Guest) on February 9, 2018

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Raphael Okoth (Guest) on January 24, 2018

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Joseph Njoroge (Guest) on November 12, 2017

Tumaini ni nanga ya roho

Bernard Oduor (Guest) on July 1, 2017

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Dorothy Majaliwa (Guest) on April 24, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Nora Kidata (Guest) on January 8, 2017

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Margaret Mahiga (Guest) on December 29, 2016

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Benjamin Masanja (Guest) on December 19, 2016

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Grace Minja (Guest) on November 8, 2016

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Kenneth Murithi (Guest) on November 4, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Rose Waithera (Guest) on August 23, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Henry Sokoine (Guest) on April 7, 2016

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

John Mushi (Guest) on January 6, 2016

Wakati wa Mungu ni kamilifu

John Mushi (Guest) on December 15, 2015

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Jane Muthui (Guest) on November 13, 2015

Amina

Peter Mugendi (Guest) on November 7, 2015

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Elijah Mutua (Guest) on October 15, 2015

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Anna Mchome (Guest) on August 9, 2015

Rehema zake hudumu milele

Joyce Aoko (Guest) on June 28, 2015

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Francis Njeru (Guest) on June 26, 2015

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Grace Wairimu (Guest) on April 5, 2015

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

James Mduma (Guest) on April 2, 2015

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Related Posts

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wa... Read More

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie B... Read More

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na M... Read More

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

Kwa njia ya Maji haya ya Baraka,

na kwa njia ya Damu yako azizi,

na kwa maombezi ya M... Read More

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

(Sala hii inafaa sana kwa ajili ya kutetea uhai wa watoto wachanga wakiwa tumboni mwa mama za... Read More

SALA YA KUTUBU

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukiz... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

Ee uliye Mkuu, Mt. Yosefu, uliyatii kabisa maongozi ya Roho Mt. Unijalie neema ya kufahamu aina y... Read More

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie ... Read More

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo ... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Mar... Read More

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)