Log in to access your menu with tools for managing ๐ tasks, ๐ฅ clients, ๐ฐ finances, ๐ learning, ๐ personal growth, and ๐ spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-23 16:11:39 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Abebwaye hujikaza: huwakumbusha watu wajibu wa kufanya juhudi za kujisaidia wenyewe pale wanapopewa msaada wa awali. Ikiwa utasaidiwa basi abgalau onesha juhudi za kujiweza pindi msaada utakapofika mwisho
Updated at: 2024-05-23 16:11:40 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Asiyesikia la mkuu, huvunjka guu: methali hii ina lengo la kuwatahadharisha watoto au vijana wadogo kuheshimu yale wanayoambiwa na wakubwa zao. Sababu kuu ya kufanya hivyo ni kwa sababu watu wazima wanatajiriba ya maisha na hivyo maelekezo yao huwa ni msaada kwa vijana wadogo na endapo wakiipuuza wanaweza kujikuta katika matatizo.
Updated at: 2024-05-23 16:11:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Akili ni nywele kila mtu ana zake: hutukumbusha kuwa kila binadamu ana mawazo na mtazamo wake wa kufanya au kuamini mambo hivyo uono hakutafanana na mwingine.
Updated at: 2024-05-23 16:11:37 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Asiefunzwa na mama, huvunzwa na ulimwengu: maonyo ya wazaz, walezi au watu wazima yana nafasi kubwa katika ustawi wa maisha ya vijana, hivyo ni muhimu kuwasikiliza lakini ikitokea maonyo hayo hayasikilizwi basi watajifunza mambo mabaya kutoka kwa watu wengine na yataleta madhara. Vilevile hutukumbusha kuwa wazazi wanaweza kukuadhibu kwa wema tena kwa upendo lakini watu wengine watakuadhibu bila huruma endapo utakosea.