Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Sala ya Asubuhi ya kila siku

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Kwa jina la Baba….. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,Mwana na Roho. Nilinde tena siku hii,niache dhambi nikutii.Naomba sana Baba wee, baraka yako nipokee. Bikira safi, Ee Maria nisipotee nisimamie. Mlinzi mkuu malaika wee kwa Mungu wetu niombee,nitake nitende mema tu na mwisho nije kwako juu.Amina.

NIA NJEMA.

Kumueshimu Mungu wangu,namtolea roho yangu. Nifanye kazi nipumzike ,amri zake tu nishike. Wazo,neno,tendo lote namtolea Mungu pote Roho,Mwili chote changu. Pendo na uzima wangu. Mungu wangu nitampenda wala dhambi sitatenda. Jina lako nasifia,utakalo hutimia kwa utii navumili. Teso na matata pia,nipe Bwana neema zako, niongeze sifa yako.Amina.

SALA YA MATOLEO.

Ee Yesu kwa mikono ya Bikira Maria,na kwa maungano na sadaka yako kuu. Ninakutolea sala,matendo,masumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu ufalme wako utufikie.Amina.

BABA YETU.

Baba yetu uliye mbinguni,jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike.Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni. Utupe leo mkate wetu wa kila siku.Utusamehe makosa yetu,kama tunavyo wasamehe na sisi waliyo tukosea. Usitutie katika kishawishi,lakini utuopoe maovuni.Amina.

SALAMU MARIA.

Salamu Maria,umejaa neema Bwana yu nawe,umebarikiwa kuliko wanawake wote,na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu,utuombee sisi wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu.Amina.

KANUNI YA IMANI.

Nasadiki kwa Mungu,Baba Mwenyezi,muumba mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu Mwanaye wa pekee,Bwana wetu aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,akazaliwa na Bikira Maria,akateswa kwa mamlaka ya ponsyo Pilato,akasulibiwa, akafa,akazikwa,akashukia kuzimu siku ya tatu akafufuka katika wafu, akapaa mbinguni amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi,toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,kanisa takatifu katoliki ushirika wa Watakatifu,maondoleo ya dhambi,ufufuko wa miili na uzima wa milele.Amina.

AMRI ZA MUNGU.

1.Ndimi Bwana Mungu wako,usiabudu miungu wengine. 2.Usilitaje bure jina la Mungu wako. 3.Shika kitakatifu siku ya Mungu. 4.Waheshimu Baba na Mama upate miaka mingi na heri duniani. 5.Usiue. 6.Usizini. 7.Usiibe. 8.Usiseme uwongo. 9.Usitamani mwanamke asiye mke wako. 10.Usitamani mali ya mtu mwingine.

AMRI ZA KANISA.

1.Hudhuria misa takatifu domonica na sikukuu zilizo amuliwa. 2.Funga siku ya jumatano ya majivu,usile nyama siku ya Ijumaa kuuu. 3.Ungama dhambi zako walau mara moja kwa mwaka. 4.Pokea Ekarist takatifu hasa wakati wa Pasaka 5.Saidia kanisa katoliki kwa zaka. 6.Shika sheria katoliki za ndoa.

SALA YA IMANI.

Mungu wangu,nasadiki maneno yote linayo sadiki na kufundisha kanisa katoliki la Roma kwani ndiwe uliye fumbuliwa hayo,wala hudanganyiki na wala hudanganyi.Amina.

SALA YA MATUMAINI.

Mungu wangu,natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu,neema zako duniani na utukufu mbinguni.Kwani ndiwe uliyeagana hayo nasi nawe mwamini.Amina.

SALA YA MAPENDO.

Mungu wangu,nakupenda zaidi ya chochote, kwani ndiwe mwema ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu kama nafisi yangu kwa ajiri yako.Amina.

SALA YA KUTUBU.

Mungu wangu,nimetubu sana dhambi zangu kwani ndiwe mwema,ndiwe mwenye kupendeza wachukizwa na dhambi. Basi sitaki kukosa tena nitafanya kitubio,naomba neema yako nipate kurudi.Amina.

SALA KWA MALAIKA MLINZI.

Malaika mlinzi wangu,unilinde katika hatari zote za Roho na za Mwili.Amina.

MALAIKA WA BWANA.

K.Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria. W.Naye akapata mimba kwa Roho mtakatifu. Salamu Maria….. K.Ndimi mtumishi wa Bwana. W.Nitendewe ulivyo nena. Salamu Maria….. K. Neno la Mungu akatwaa Mwili. W. Akakaa kwetu. Salamu Maria…. K. Utuombee Mzazi Mtakatifu wa Mungu. W. Tujaliwe ahadi za Kristu. Tuombe. Tunakuomba Ee Bwana utie neema yako mioyoni mwetu ili sisi tuliyojuwa kwa maelezo ya malaika kwamba, Kristu mwanao amejifanya mtu kwa mateso na msalaba wake. Tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu.Amina.

ATUKUZWE BABA.

Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,kama mwanzo na sasa na siku zote na milele.Amina. K. Moyo Mtakatifu wa Yesu W.Utuhurumie. K. Moyo safi wa Bikira Maria. W. Utuombee. K. Mtakatifu Yosefu. W. Utuombee. K. Watakatifu somo wa majina yetu. W. Mtuombee. K.Watakatifu wote wa Mungu. W.Mtuombee. Kwa jina la Baba…..
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Jul 12, 2024
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest May 30, 2024
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Feb 9, 2024
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ James Kimani Guest Jan 26, 2024
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jan 10, 2024
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Dec 29, 2023
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Nov 20, 2023
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Oct 31, 2023
πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Sep 14, 2023
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Aug 6, 2023
Amina
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Aug 4, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Grace Mligo Guest May 26, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Apr 13, 2023
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Oct 13, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Jul 25, 2022
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Jul 16, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Jul 11, 2022
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Jun 25, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Jun 3, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Feb 18, 2022
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Feb 8, 2022
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Jan 26, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Dec 18, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Nov 23, 2021
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Oct 11, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Oct 10, 2021
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Aug 30, 2021
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest Apr 21, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jan 16, 2021
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Jan 13, 2021
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Dec 27, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Dec 21, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Oct 21, 2020
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ John Mushi Guest Aug 26, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Aug 11, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Samuel Were Guest May 4, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Apr 18, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jan 13, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Jan 13, 2020
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Jan 11, 2020
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Jan 2, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ James Kawawa Guest Dec 22, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Nov 24, 2019
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Nov 21, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Nov 18, 2019
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Peter Otieno Guest Oct 17, 2019
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Aug 25, 2019
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jun 30, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Jun 24, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Jun 1, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Feb 9, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Dec 11, 2018
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Aug 22, 2018
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Lydia Mzindakaya Guest Jul 2, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest May 4, 2018
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Jan 2, 2018
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Paul Ndomba Guest Dec 25, 2017
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Dec 19, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Oct 9, 2017
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Sep 14, 2017
Rehema zake hudumu milele

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About