Ukeketaji au tohara ya wanawake ni hatari sana kwa msichana
anayetahiriwa. Wasichana hufa kutokana na madhara yake
makubwa zaidi kwa vile:
Hutokwa na damu nyingi.
Uambukizo unatokea iwapo vifaa vilivyotumiwa
havikuwa safi. Uambukizo unaweza kuenea mpaka katika
viungo vya ndani vya uzazi na kusababisha ugumba na
hata vifo.
Hatari ya kuambukizwa Virusi vya UKIMWI wakati wa
ukeketaji.
Kuziba kwa mkojo na damu ya mwezi (hedhi) ndani ya
mwili wa mwanamke na kusababisha uambukizo.
Matatizo na maumivu makali wakati wa kujamiiana na
wakati wa kujifungua kutokana na kupungua ukubwa wa
uke. Ukeketaji wa wanawake mara nyingi una madhara
ya kisaikologia ambapo wasichana hupoteza tumaini
na imani kwa walezi au wazazi na wanaweza wakapata
mateso ya kujisikia waoga, kufadhaika, kutojiweza na
kutokuwa kamilifu kimwili.
Zaidi ya hayo, ukeketaji unampunguzia mwanamke hamu ya
kujamiiana. Kufanikisha hamu ya ngono inategemea kwa kiasi
kikubwa viungo vya uzazi vya nje. Ukeketaji hata hivyo unaharibu
umbile na kazi za viungo vya uzazi vya nje vya mwanamke.
Ina madhara kimwili na kisaikologia ambapo mara nyingi
huleta matatizo ya mahusiano ya kimwili kati ya mwanamume
na mwanamke. Kisimi ni sehemu ya mwili wa msichana chenye
ashiki na hisia kali ya viungo vya uzazi. Kinasisimua ashiki kwa
mwanamke anaposhikwa. Sehemu ya ndani ya mashavu na kisimi
kwa kiasi kikubwa vinahusika na hali kiwango cha raha ya na
kufikia mshindo wakati wa kujamiiana. Wakati kisimi na viungo
vingine vya uzazi vimeondolewa, ashiki na raha hupungua kwa
kiasi kikubwa. Endapo mwanamke amekatwa vibaya sana au uke
umeshonwa, kuna uwezekano wa kupata maumivu na matatizo
wakati wa kujamiiana na wa kujifungua.
Ukeketaji au tohara ya wanawake ni hatari sana kwa msichana anayetahiriwa. Wasichana hufa kutokana na madhara yake makubwa zaidi kwa vile: Hutokwa na damu nyingi. Uambukizo unatokea iwapo vifaa vilivyotumiwa havikuwa safi. Uambukizo unaweza kuenea mpaka katika viungo vya ndani vya uzazi na kusababisha ugumba na hata vifo. Hatari ya kuambukizwa Virusi vya UKIMWI wakati wa ukeketaji. Kuziba kwa mkojo na damu ya mwezi (hedhi) ndani ya mwili wa mwanamke na kusababisha uambukizo. Matatizo na maumivu makali wakati wa kujamiiana na wakati wa kujifungua kutokana na kupungua ukubwa wa uke. Ukeketaji wa wanawake mara nyingi una madhara ya kisaikologia ambapo wasichana hupoteza tumaini na imani kwa walezi au wazazi na wanaweza wakapata mateso ya kujisikia waoga, kufadhaika, kutojiweza na kutokuwa kamilifu kimwili. Zaidi ya hayo, ukeketaji unampunguzia mwanamke hamu ya kujamiiana. Kufanikisha hamu ya ngono inategemea kwa kiasi kikubwa viungo vya uzazi vya nje. Ukeketaji hata hivyo unaharibu umbile na kazi za viungo vya uzazi vya nje vya mwanamke. Ina madhara kimwili na kisaikologia ambapo mara nyingi huleta matatizo ya mahusiano ya kimwili kati ya mwanamume na mwanamke. Kisimi ni sehemu ya mwili wa msichana chenye ashiki na hisia kali ya viungo vya uzazi. Kinasisimua ashiki kwa mwanamke anaposhikwa. Sehemu ya ndani ya mashavu na kisimi kwa kiasi kikubwa vinahusika na hali kiwango cha raha ya na kufikia mshindo wakati wa kujamiiana. Wakati kisimi na viungo vingine vya uzazi vimeondolewa, ashiki na raha hupungua kwa kiasi kikubwa. Endapo mwanamke amekatwa vibaya sana au uke umeshonwa, kuna uwezekano wa kupata maumivu na matatizo wakati wa kujamiiana na wa kujifungua.
π¬
Discussion
Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.
0 comment(s)
π Login required to comment or reply
You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.
Je, Ni Vipi naweza kuacha Kufanya Ngono Baada ya Kuanza? Jambo la kwanza kabisa, napenda kukupa pongezi kwa kuanza kufikiria juu ya uamuzi muhimu katiβ¦
Hapana, mbu na wadudu wengine hawawezi i kukuambukiza virusi vya UKIMWI kutokana na mfumo wa mii li yao. Virusi vya UKIMWI haviwezi kuishi kwenye mii β¦
Athari za pombe kwa mtu anayeishi na ualbino ni sawa na zilezinazowapata watu wengine.Mtu akiwa katika hali ya ulevi anaweza kuzembea katikakufanya uaβ¦
Hapana. Ualbino ni haliinayoweza kutokea kwawanadamu na wanyama wakundi la mamalia. Temboweupe wa India hujulikanasana na walithaminiwasana katika mahβ¦
Kila mtu anataka kuwa na uhuru katika uhusiano wao na msichana wao. Lakini wakati mwingine inaweza kuwa ngumu kufikia uhuru huo. Kwa hiyo, katika makaβ¦
Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kimyakimya au ngono/kufanya mapenzi ya kelele? Hii ni swali ambalo linaweza kuwa na majibu tofauti kutoβ¦
Discussion
Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.
You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.
Log in to participate