Vipimo Vya Koshari
Mchele - 2 vikombe
Makaroni - 1 kikombe
Dengu za brown - 1 kikombe
Vitunguu vilokatwakatwa (chopped) - 2
Nyanya ziilokatwakatwa (chopped) - 4
Nyanya ya kopo - 1 kijiko cha supu
Kitunguu saumu(thomu/galic) ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi ilosagwa - 1 kijiko cha chai
Pilipili manga ya unga - 1 kijiko cha chai
Mdalisini kijiti - 1
Bizari ya pilau (cumin seeds) - 1 kijiko cha supu
Hiliki - 2 chembe
Mafuta - 3 vijiko vya supu
Chumvi - kiasi
Vipimo Vya Kuku
Kuku - 3 LB
Kitunguu saumu(thomugalic) na tangawizi - 1 kijiko cha supu
Mtindi (yoghurt) - 1 kijiko cha supu
Pilipili ya masala nyekundu - 1 kijiko cha chai
Bizari upendazo - 1 kijiko cha chai
Ndimu - 1
Vitunguu slesi vilokaangwa - 3
Namna Kutayarisha Kuku
Kata kuku vipande vikubwa kiasi, osha, weka kando achuje maji.
Changanya vipimo vya kuku pamoja katika kibakuli.
Changanya pamoja na kuku, roweka muda wa kiasi nusu saa au zaidi.
Mchome (grill) kuku hadi aive weka kando.
Namna ya Kutayarisha Koshari
Tia mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu hadi viive kuwa rangi hudhurungi.
Tia thomu ,mdalisini, bizari ya pilau na hiliki kaanga tena kidogo.
Tia nyanya, pilipili zote, nyanya kopo, chumvi changanya vizuri ukaange kidogo.
Epua sosi acha kando.
Chemsha dengu pamoja na kidonge cha supu ziive nusu kiini na ibakie supu yake. Muda wa kuchemsha dengu inategemea aina yake.
Tia mchele uchanganyike, funika, pika hadi uive vizuri pamoja na dengu
Chemsha makaroni hadi yaive , epua chuja maji.
Changanya pamoja wali wa dengu na macaroni.
Pakua katika sahani, kisha weka juu yake kuku aliyechomwa, mwagia vitunguu vilokaangwa, kisha mwagia sosi.
No comments yet. Be the first to share your thoughts!