Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya Kiti cha Enzi cha Mungu, ninakukabidhi nia na haja zangu zote. Ee Mt. Yosefu, unisaidie kwa maombezi yako yenye nguvu, na unipatie kutoka kwa Mwanao Mungu, baraka zote za kiroho, kwa njia ya Kristu Bwana wetu, ili nikishapata msaada wako wa mbinguni ningali bado hapa duniani, niweze nami kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu aliye Baba mwema kabisa kushinda wote. Ee Mt. Yosefu, sichoki kamwe kufikiri moyoni kwa upendo, jinsi Mtoto Yesu alivyokuwa amesinzia mikononi mwako. Akiwa amepumzika hivyo karibu na moyo wako, sithubutu kujongea, nisije nikamsumbua, bali nakuomba wewe umkumbatie na kumbusu kwa niaba yangu na kumwambia anipe busu lake nitakapovuta pumzi yangu ya mwisho.
Mtakatifu Yosefu Msimamizi wa wanaozimia roho; Utuombee.
Amina.

Sala hii ilipatikana katika mwaka wa hamsini wa Bwana na Mwokozi Wetu Yesu Kristu. Mnamo mwaka 1505 Baba Mtakatifu alimtumia sala hii Mfalme Charles wakati alipokuwa anaenda vitani. Yeyote atakayeisoma sala hii, au kuisikia ikisomwa, au kuibeba, hatakufa kifo cha ghafla,hatazama majini, hatadhurika kwa sumu, wala hataanguka katika mikono ya adui zake, au kuunguzwa katika moto wowote ule, au kushindwa katika vita.

Sali sala hii kwa siku tisa mfululizo, kwa kuomba jambo lolote unalolihitaji. Haijawahi kusikika kuwa sala hii imeshindwa jambo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 85

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Dec 27, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Dec 27, 2017
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Dec 19, 2017
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Oct 11, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Aug 10, 2017
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Jun 15, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest May 7, 2017
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Chris Okello Guest May 2, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Dec 10, 2016
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Nov 14, 2016
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Oct 15, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ James Kimani Guest Sep 26, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Aug 20, 2016
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Jun 29, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest May 20, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Chris Okello Guest May 20, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Violet Mumo Guest May 6, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Nov 22, 2015
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Lydia Mzindakaya Guest Oct 28, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Oct 13, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Aug 18, 2015
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Aug 14, 2015
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Jul 11, 2015
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ John Lissu Guest Jun 18, 2015
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Jun 13, 2015
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About