Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili yangu,/ nashindwa kuelewa./ Unaficha Ukuu wako usiofahamika/ na kujidhihirisha kwa ajili yangu mimi mnyonge./ Ee Mfalme wa utukufu,/ unaficha uzuri wako,/ lakini jicho la moyo wangu/ linapenya pazia na kuona Majeshi ya Malaika/ wakikuimbia kwa heshima bila kukoma/ na nguvu zote mbinguni zikikusifu bila mwisho zikisema:/ β€œMtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu..”/

Ni nani awezaye kufahamu Upendo wako/ na huruma yako isiyo na kipimo kwa ajili yetu!/ Ee Mfungwa wa Upendo,/ nafungia moyo wangu masikini/ kwenye Tabarnakulo hii/ ili niweze kukuabudu usiku na mchana bila mwisho./ Najua hakuna kizuizi/ na hata kama naonekana kukaa mbali,/ lakini moyo wangu u pamoja nawe/ katika ibada hii./ Hakuna kinachoweza kuzuia upendo wangu kwako./ Kwangu hakuna kizuizi chochote./

Ee Utatu Mtakatifu,/ Mungu Mmoja usiyegawanyika,/ utukuzwe kwa zawadi yako hii kuu/ na agano hili la huruma!/

Nakuabudu,/ Bwana na Muumba uliyefichika katika Sakramenti Takatifu!/ Ee Bwana,/ nakuabudu kwa kazi zote za mikono yako/ zinazonifunulia Hekima yako kuu,/ Wema wako na Huruma yako kuu./ Uzuri uliousambaza hapa/ Uzuri ulio nao Wewe mwenyewe/ ambaye U Uzuri usioelezeka;/ na ingawaje umejificha na kusitiri uzuri wako,/ jicho langu,/ kwa mwanga wa imani linafika kwako,/ na roho yangu inapata kumtambua Muumba wake/ aliye Uzuri usiopimika,/ ulio juu ya kila uzuri,/ na moyo wangu unazama kabisa katika sala ya kukuabudu./

Bwana wangu na Muumba wangu,/ wema wako wanitia moyo wa kuongea nawe,/ Huruma yako huondoa kiambaza/ kitenganishacho Muumba na kiumbe./ Furaha ya moyo wangu,/ ee Mungu, ni kuongea na Wewe./ Yote ambayo moyo wangu unayatamni nayapata kwako./ Hapa ndipo mwanga wako unaponiangaza akili yangu/ na kuiwezesha kukujua Wewe zaidi na zaidi/ – ndipo mikondo ya neema inapoutiririkia moyo wangu,/ ndipo roho yangu inapochota uzima wa milele./ Ee Bwana na Muumba wangu,/ licha ya mapaji yote haya,/ unajitoa mwenyewe kwangu,/ ili uweze kujiunganisha na kiumbe dhaifu na maskini./

Ee Kristu,/ nafurahi sana nionapo kwamba unapendwa/ na kwamba sifa na utukufu wako vinaongezwa/ hasa ya Huruma yako./ Ee Kristu,/ sitaacha kamwe kuutukuza wema wako na huruma yako,/ hadi dakika ya mwisho ya maisha yangu./ Kwa kila tone la damu yangu/ na kwa kila pigo la moyo wangu/ naitukuza Huruma yako./ Natamani kugeuzwa kabisa/ na kuwa utenzi wa utukufu wako./ Naomba siku ya kufa kwangu/ popote nitakapokuwa nimelala,/ pigo la mwisho la moyo wangu/ liwe utenzi mpendevu/ usifuo Huruma yako isiyo na kipimo./ Amina

(Na Mt. Faustina Kowalska).

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Sep 3, 2018
πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Aug 29, 2018
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Aug 13, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest May 3, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Feb 27, 2018
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Dec 10, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ George Mallya Guest Nov 16, 2017
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Jul 16, 2017
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Jun 7, 2017
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Mar 20, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Feb 4, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Jan 2, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Nov 15, 2016
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Oct 15, 2016
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Jul 23, 2016
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest May 11, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest May 9, 2016
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Apr 26, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Feb 9, 2016
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Dec 15, 2015
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Nov 1, 2015
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Diana Mumbua Guest Jul 8, 2015
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest May 1, 2015
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About