Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Inaweza kusemwa wakati wowote katika mwaka. Kwa ajili ya kujiandaa kwa Sikukuu ya Moyo Mtakatifu wa Yesu,; anza Novena kwa Moyo Mtk wa Yesu katika Alhamisi ya Sikukuu ya Ekaristi Takatifu (Corpus Christi), yaani Alhamisi ya wiki moja kabla ya Sikukuu ya Moyo Mtk (au Alhamisi baada ya Sikukuu ya Utatu Mtk). Endapo Sikukuu hii itaadhimishwa siku ya Dominika inayofuata Sikukuu yenyewe kama inavyofanyika mahali pengi, basi novena inatakiwa ianze Ijumaa ya baada ya Sikukuu ya Utatu Mtk ili imalizike Jumamosi kabla ya Dominika ya sikukuu hii ya Moyo Mtk kwa Yesu.

WIMBO:

YESU KRISTU TWASIFU MOYO WAKO
Yesu Kristu, twasifu Moyo wako, sisi sote, milele mali yako
Tunakupa, nyoyo zote zetu, Mukombozi, Mfalme Mungu wetu;
Tunakupa, nyoyo zote zetu, Mukombozi, Mfalme Mungu wetu!

Watu wengi, wanakaa ugenini, wazunguka, wenye ukiwa chini,
Uwatie huruma yako kuu, roho zao, uziinue juu;
Uwatie huruma yako kuu, roho zao, uziinue juu!

Uwe Mfalme, wa wale washikwao, na ushenzi, na ukaidi wao
Wapelekee ufalme wa Mungu, ni Mchunga mmoja Zizi moja tu;
Wapelekee ufalme wa Mungu, ni Mchunga mmoja Zizi moja tu!

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi wkako. Amina.

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.
Kwenye Msalaba Sali:

“Ee Yesu tupe moyo wako kama amana ya upendo wako na kimbilio letu, ili tupate pumziko salama wakati wa maisha yetu na faraja tamu saa ya kufa kwetu”.
Baba Yetu ……..
Salamu Maria ……. (mara tatu)
Nasadiki ………..

Kwenye chembe kubwa Sali (Badala ya ‘Baba Yetu’):
“Ninakuabudu, ninakutukuza na ninakupenda, Ee Moyo wa Yesu wangu mpenzi, uliopenywa na huzuni nyingi kwa ajili ya dhambi, ambazo zimekuwa zikitendwa hata leo, dhidi ya Sakramenti Takatifu sana ya Altare. Ninakutolea hapo kwa kuridhika, moyo wa Mama yako mpendevu, na mastahili ya watakatifu. Amina”.

Kwenye chembe ndogo sali (Badala ya ‘Salamu Maria’):
“Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, uwakao mapendo kwetu, washa nyoyo zetu kwa mapendo yako"

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie Kristo utusikilize
Baba wa mbinguni Mungu Utuhurumie
Mwana, Mkombozi wa dunia Mungu Utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu mmoja Utuhurumie
Moyo wa Yesu Mwana wa Baba wa Milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu uliotungwa na Roho Mtakatifu mwilini mwa Mama Bikira Maria Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulioungana na Neno wa Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulio na utukufu pasipo mfano Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hekalu takatifu la Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hema la Yule aliye juu Utuhurumie
Moyo wa Yesu tanuru lenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, nyumba ya Mungu na mlango wa Mbingu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tanuru yenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chombo cha haki na upendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaojaa upendo na wema Utuhurumie
Moyo wa Yesu, kilindi cha fadhila zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaostahili sifa zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaotawala mioyo yote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, zinamokaa hazina za hekima na elimu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliopendelewa na Mungu Baba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotuenezea maziada yake Utuhurumie
Moyo wa Yesu, mtamaniwa wa vilima vya milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu, wenye uvumilivu na huruma nyingi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tajiri kwa wote wenye kukuomba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya uzima na utakatifu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, malipo kwa dhambi zetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, ulioshibishwa matusi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliovunjika kwa sababu ya ubaya wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotii mpaka kufa Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliochomwa kwa mkuki Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya faraja zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uzima na ufufuo wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, amani na upatanisho wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sadaka ya wakosefu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unamokaa wokovu wao wenye kukutumaini Utuhurumie
Moyo wa Yesu, matumaini yao wenye kuzimia kwako Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sababu ya furaha ya watakatifu wote Utuhurumie
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusamehe Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusikilize Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utuhurumie

Kiongozi: Yesu mwenye Moyo mpole na mnyenyekevu,
Wote: Ufanye mioyo yetu ifanane na Moyo wako

TUOMBE: (W) Ee Mungu Mwenyezi milele, uuangalie Moyo wa mwanao mpendelevu, pia na heshima na malipo aliyokutolea kwa ajili ya wenye dhambi, uridhike, uwaondolee wenye kuomba toba kwako kwa njia ya huyo Mwanao Yesu Kristo anayeishi na kutawala nawe pamoja na Roho Mtakatifu, Mungu milele. Amina.

P.S. Mwezi wa sita ni wa kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu. Vitu vya kufanya ni pamoja na kushiriki Misa takatifu kila siku, kumtembelea Bwana Yesu katika Ekaristia, kusali Rozari ya Moyo Mtakatifu wa Yesu kila siku, kusali Litania za Moyo Mtakatifu wa Yesu, kuimba nyimbo za kuusifu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na kadhalika. Kwa kufanya hayo na mengineyo yanayofanana nayo, waumini hujichotea Baraka na neema nyingi za kimwili na kiroho.

SALA YA NOVENA

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwa”, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewa”, tazama kwa jina lako ninaomba ……. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe”, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.

Sali ‘Salamu Malkia’ na kuongezea, ‘Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombee’.

P.S. – Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.

SALA YA MAOMBI

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe tegemeo langu na tumaini langu dhabiti. Ndiwe mwenye dawa ya maovu yangu yote, malipizi ya makosa yangu yote. Waweza kunipatia haja zangu na neema ninazoziomba mimi na wengine. Wewe uko ili kutusaidia sote, ndiwe mwanga mkuu usiozimika, ndiwe chanzo cha nguvu, uvumilivu, amani na faraja. Nina hakika kuwa maombi yangu hayatakuchosha, nawe hutaacha kunisaidia, kunilinda, kunipenda, kwani, ee Moyo Mtakatifu , upendo wako hauna mwisho. Ee Moyo Mtakatifu, unihurumie, kwa ajili ya maombi yangu, kadiri ya huruma yako. Nawe katika sisi, na kwa ajili yetu, ufanye lolote unalolihitaji, kwani tunajitoa kwako kwa imani na uhakika thabiti kwamba kamwe hautatuacha, kwa milele. Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
👥 Anna Malela Guest Jun 14, 2024
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
👥 Edwin Ndambuki Guest Jan 1, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Christopher Oloo Guest Dec 22, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Anna Sumari Guest Nov 20, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Miriam Mchome Guest Nov 13, 2023
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
👥 Anna Sumari Guest Oct 14, 2023
🙏✨ Mungu atakuinua
👥 Stephen Kikwete Guest Aug 4, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 John Malisa Guest Jul 10, 2023
Rehema hushinda hukumu
👥 Lucy Mushi Guest Jun 23, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Edward Chepkoech Guest Jun 5, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Monica Adhiambo Guest Jun 3, 2023
🙏🙏🙏
👥 Rose Mwinuka Guest May 21, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Ruth Kibona Guest Mar 23, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Moses Mwita Guest Feb 16, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Martin Otieno Guest Dec 30, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Kenneth Murithi Guest Nov 15, 2022
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
👥 Sarah Mbise Guest Nov 13, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Stephen Amollo Guest Oct 22, 2022
Neema na amani iwe nawe.
👥 Elijah Mutua Guest Oct 20, 2022
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
👥 Jackson Makori Guest Aug 4, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Rose Waithera Guest Jul 1, 2022
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
👥 Raphael Okoth Guest Jun 26, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Charles Wafula Guest Jun 25, 2022
Nakuombea 🙏
👥 Brian Karanja Guest Jun 8, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Samuel Were Guest May 24, 2022
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
👥 Samuel Omondi Guest Feb 4, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Miriam Mchome Guest Jan 23, 2022
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
👥 Mariam Hassan Guest Oct 15, 2021
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
👥 Michael Onyango Guest Oct 4, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Alice Wanjiru Guest Aug 28, 2021
Amina
👥 Mary Kendi Guest Jun 21, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Kenneth Murithi Guest Dec 1, 2020
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
👥 Isaac Kiptoo Guest Nov 25, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Joyce Nkya Guest Oct 2, 2020
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
👥 Francis Mtangi Guest Oct 2, 2020
Sifa kwa Bwana!
👥 Rose Waithera Guest Jul 28, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Betty Akinyi Guest Jun 28, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Irene Makena Guest May 23, 2020
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
👥 Lucy Mahiga Guest Apr 3, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Edward Chepkoech Guest Feb 16, 2020
🙏🌟 Mbarikiwe sana
👥 Rose Kiwanga Guest Jan 14, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Mary Njeri Guest Jan 4, 2020
🙏❤️ Mungu akubariki
👥 Ruth Mtangi Guest Dec 23, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Kevin Maina Guest Dec 22, 2019
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
👥 Esther Nyambura Guest Dec 12, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Betty Kimaro Guest Aug 6, 2019
Dumu katika Bwana.
👥 Diana Mallya Guest Jul 11, 2019
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Stephen Mushi Guest May 25, 2019
Mungu akubariki!
👥 Lydia Mutheu Guest Feb 17, 2019
🙏🌟 Mungu akujalie amani
👥 Benjamin Masanja Guest Dec 21, 2018
🙏💖 Nakusihi Mungu
👥 Peter Mwambui Guest Dec 5, 2018
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
👥 Rose Kiwanga Guest Nov 7, 2018
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
👥 Grace Mushi Guest Oct 23, 2018
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
👥 Stephen Kangethe Guest Oct 4, 2018
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
👥 Chris Okello Guest Aug 30, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Grace Njuguna Guest Aug 13, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Lydia Mahiga Guest Jul 14, 2018
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
👥 Charles Mboje Guest Jun 23, 2018
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
👥 Peter Mugendi Guest May 4, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Nancy Akumu Guest Apr 26, 2018
Endelea kuwa na imani!

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About