Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Mambo ya Msingi kujua kuhusu Sakramenti ya Kitubio

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu gani?
Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu alijua udhaifu wa binadamu hauishi mara anapopokea uzima wa Mungu kwa sakramenti tatu za kuingizwa katika Ukristo. Hivyo alipanga kusaidia mpaka mwisho wa dunia waamini wake watakaopatwa na dhambi na ugonjwa, kama alivyowasaidia wengi aliokutana nao katika maisha yake.
“Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, ‘Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako’… ‘Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi’ – amwambia yule mwenye kupooza – ‘Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako’. Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake. Makutano walipomwona, walishikwa na hofu, wakamtukuza Mungu, aliyewapa watu amri ya namna hii” (Math 9:2,6-8).

Mungu aliwapa watu (mapadri) amri/uwezo ya kusamehe dhambi kwa njia ya nani? Ni halali kuungama kwa padre?
Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi kwa njia ya Mwanae. Yesu mfufuka aliwaonyesha Mitume alama ya mateso mwilini mwake, “akawavuvia, akawaambia, ‘Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wowote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa” (Yoh 20:22-23).
Katika Kanisa tunafurahi kupewa msamaha wa dhambi kila tunapohitaji, mradi tutubu. Kwa njia ya mwandamizi wa Mitume, Yesu anatuambia,
“Umesamehewa dhambi zako… Imani yako imekuokoa, enenda zako kwa amani” (Lk 7:48,50).
Si dhana wala hisia tu, bali ni neno la hakika tunalolipokea kwa masikio yetu.

Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi zipi?
Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi zote, kwa sababu upendo mtiifu wa Mwanae aliyejitoa kuwa sadaka ya wokovu wetu unampendeza kuliko dhambi zote zinavyomchukiza. Ila hatuwezi kusamehewa dhambi ya kukataa neema ambayo Roho Mtakatifu anatusukuma tuamini na kutubu, kwa sababu pasipo imani na toba hapana msamaha.
“Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa” (Math 12:31).
“Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure” (2Kor 6:1).

Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi kwa sababu gani?
Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi kwa sababu amependa washiriki katika kazi zake. Ametuumba kwa njia ya wazazi na kutulea na kutusaidia kwa njia ya wengine pia. Hasa ametuokoa kwa njia ya Yesu, ambaye yupo nasi sikuzote katika Mwili wake, yaani Kanisa, na katika wale walioshirikishwa mamlaka ya Mitume.
“Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho; yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho. Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo: mpatanishwe na Mungu” (2Kor 5:18-20).

Je, tumuendee padri ili kuondolewa dhambi?
Ndiyo, tumuendee padri ili kuondolewa dhambi tulizotenda baada ya ubatizo, kwa kuwa hatuwezi kupokea msamaha tukikataa masharti yake, na Mungu ametupangia watu ambao watuondolee kwa niaba yake.
“Watu wote na watoza ushuru waliposikia hayo, waliikiri haki ya Mungu, kwa kuwa wamebatizwa kwa ubatizo wa Yohane. Lakini, Mafarisayo na wanasheria walilipinga shauri la Mungu juu yao, kwa kuwa hawakubatizwa naye” (Lk 7:29-30).
Yesu mwenyewe alikubali kubatizwa na Yohane ili atimize mpango wa Baba.
“Yohane alitaka kumzuia, akisema, ‘Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?’ Yesu akajibu akamwambia, ‘Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote” (Math 3:14-15).
Je, sisi tukatae kumkimbilia padri wa Mungu ili kupokea huruma yake tunayoihitaji kuliko hewa?

Tumuungamie padri dhambi zetu kwa lengo gani? Kwa nini Wakatoliki wanaungama kwa padri?
Tumuungamie padri dhambi zetu ili aweze kutushauri na kuamua kama tuko tayari kuondolewa. Tumweleze kwa unyofu makosa yote tuliyoyafanya na nia tuliyonayo ya kuyafidia na kutoyarudia.
“Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo, wala neno lake halimo mwetu” (1Yoh 1:8-10).
Tukumbuke tulivyo viungo vya Mwili mmoja, hivi kwamba dhambi zetu zimewadhuru wenzetu. “Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana, mpate kuponywa” (Yak 5:16).
Kutokuwa tayari kufanya hivyo walau sirini kwa padri ni dalili ya kiburi na ya kutotubu.

Je, padri akiwa mkosefu, anaweza kutuondolea dhambi?
Ndiyo, padri akiwa mkosefu, anaweza kutuondolea dhambi kwa niaba ya Mungu aliyempa mamlaka hiyo. Hatusamehewi na utakatifu wa padri, bali na huruma ya Baba kwa njia yake.
Yeye anamtumia padri yeyote ili kuturahisishia kazi, tusihitaji kuchunguza kwanza ubora wa maisha yake, wala kwenda mbali tukampate mmoja asiye na dhambi. Tungefanyeje kuhakikisha ni mtakatifu, wakati hatuwezi kusoma moyo wake? Ingekuwa hivi, tusingepata kamwe hakika ya kusamehewa. Kumbe inatutosha kujua ni padri, kwamba Mungu amempa mamlaka ya kusamehe dhambi, kama Yesu alivyowapa Mitume siku tatu baada ya kumkimbia na hata kumkana. Kila padri anaweza kukiri,
“Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa: ya kwamba Kristo Yesu alikuja ulimwenguni awaokoe wenye dhambi, ambao wa kwanza wao ni mimi” (1Tim 1:15).
Amri ya kusamehe dhambi wamepewa watu, si malaika.
“Tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu” (2Kor 4:7).

Je, nje ya kitubio tunaweza kuondolewa dhambi tuliyotenda baada ya ubatizo?
Ndiyo, nje ya kitubio tunaweza kuondolewa dhambi tuliyotenda baada ya ubatizo, lakini ni vigumu zaidi, kwa sababu hatupati msaada wa sakramenti hiyo maalumu.
Pamoja na nia ya kumuungamia padri mapema tunahitaji neema ya kutubu kikamilifu, si kwa kuhofia adhabu, bali kwa kumpenda Mungu tuliyemchukiza.
“Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana” (Lk 7:47).

Sakramenti ya Kitubio ni nini?
Sakramenti ya Kitubio ndiyo Sakramenti ya kuwaondolea watu dhambi walizotenda baada ya Ubatizo (Yoh 20:22-23)

Lini na kwa maneno gani Yesu aliweka Sakramenti ya Kitubio?
Yesu aliweka Sakramenti ya Kitubio jioni ya ufufuko wake alipowapulizia mitume na kuwaambia maneno haya "Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi watakua wameondolewa, wowote mtakaowafungia dhambi watakua wamefungiwa" (Yoh 20:22-23)

Mwenye kuwaondolea watu dhambi ni nani?
Mwenyezi Mungu pekee yake aweza kuwaondolea watu dhambi. Ndiye aliyewapa Mitume, Maaskofu na Mapadri uwezo wa kuwaondolea watu dhambi (Yoh 20:21-23)

Nani yampasa kupokea Sakramenti ya Kitubio?
Kila mkristo aliyetenda dhambi yampasa kupokea Sakramenti ya Kitubio

Mkristo akitaka kupokea Sakramenti ya Kitubio yampasa nini?
Mkristo akitaka kupokea Sakramenti ya Kitubio yampasa haya
1. Kutafuta dhambi moyoni (Yoh 3:20-21) 2. Kujuta dhambi 3. Kukusudia kuacha dhambi 4. Kuungama kwa padre 5. Kutimiza malipizi 6. Kumshukuru Mungu aliyemwondolea dhambi

Wakati wa Sakramenti ya Kitubio Utamwomba Roho Mtakatifu kwa sala gani?
Utamuomba Roho Mtakatifu kwa sala hii:
Uje Roho Mtakatifu unisaidie nitambue dhambi zangu, nijute sana, niungame vema, nipate kutubu kweli. Amina

Kutafuta dhambi maana yake ni nini?
Kutafuta dhambi maana yake ni kujiuliza moyoni dhambi nilizotenda Tangu ungamo la mwisho (Ef 4:17-32)

Utafuteje dhambi wakati wa kujiandaa kuungama?
Tafuta dhambi kwa njia hizi
1. Kwa kukumbuka uliyokosa kwa mawazo, kwa maneno na kwa vitendo 2. Katika Amri za Mungu na za Kanisa 3. Katika vichwa vya dhambi 4. Katika kutimiza wajibu

Kutubu dhambi maana yake ni nini?
Kutubu dhambi maana yake ni kuona uchungu na chuki moyoni juu ya dhambi tulizotenda na kukusudia kutotenda dhambi tena (Yoh 8:11)

Kwa nini tujute dhambi zetu?
Tunajuta dhambi zetu kwa sababu tumeukosea Utatu Mtakatifu na tunastahili adhabu yake, na pia bila majuto hatuwezi kupata maondoleo ya dhambi.

Kuna majuto ya namna ngapi?
una majuto ya namna mbili, 1. Majuto kamili/Majuto ya mapendo 2. Majuto yasiyokamili/majuto pungufu/majuto ya hofu

Majuto kamili ni nini?
Majuto kamili ni kujuta kwa sababu tumemchukiza Mungu mwenyewe aliye mwema na mpendelevu kabisa

Majuto yasiyo kamili au majuto pungufu ni nini?
Majuto yasiyokamili ni kujuta kwa sababu tumepoteza furaha za Mbinguni na tunahofia adhabu ya Mungu

Asiyejuta aweza kuondolewa dhambi?
Asiyejuta hawezi kuondolewa dhambi kabisa, na anayeungama bila kujuta anatenda dhambi kubwa ya kufuru.

Kabla ya kuungama ni lazima kufanya nini?
Kabla ya kuungama ni lazima kukusudia kuacha dhambi na kuepuka nafasi kubwa ya dhambi bila kusahau kufuata hatua sita za kabla na baada ya kupokea kupokea Sakramenti ya Kutubio ambazo ni,
(1) kuwaza/kutafuta dhambi moyoni, (2)kutubu/ kujuta, (3)kukusudia kuacha dhambi, (4)kuungama kwa padri, (5)kutimiza kitubio, (6)kumshukuru Mungu

Anayetaka kweli kuacha dhambi afanye nini?
Anayetaka kuacha dhambi afanye nguvu kuvishinda vishawishi, asali/aombe na apokee Sakramenti Mara nyingi hasa Sakramenti ya Kitubio na Ekaristi Takatifu.

Kuungama ni kufanya nini?
Kuungama ni kumwambia Padri wazi wazi dhambi zako ulizotenda, zipi na ngapi ili upate maondoleo.

Anayeficha kusudi dhambi ya mauti katika ungamo anaondolewa?
Haondolewi, Bali anatenda dhambi kubwa ya kukufuru Sakramenti ya Kitubio. (Mt 7:21-23, Yoh 20:23, Gal 6:7)

Anayekufuru Sakramenti ya Kitubio yampasa nini?
Yampasa kuziungama tena dhambi zake zote alizotenda tangu ondoleo la mwisho

Padri anaondolea dhambi mahali pa nani?
Padri anaondolea dhambi mahali pa Mungu

Padri anaondolea dhambi kwa maneno gani?
Padre anaondolea dhambi kwa maneno haya: Nami "Nakuondolea dhambi zako zote kwa Jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu".

Kitubio tuwezacho kupewa na padre ni nini?
Kitubio tuwezacho kupewa na Padre ni kama sala, kufunga, kutoa sadaka kwa maskini, kusoma maandiko matakatifu, kuwatazama wagonjwa, n.k.

Kitubio tupewacho na padre chatosha?
Ni shida kutosha. Mara nyingi chataka malipizi ya hapa duniani kama kufunga, magonjwa, masumbuko, sala n.k mateso yasipotosha hapa duniani yatakamilishwa toharani

Kutimiza malipizi maana yake ni ni nini?
Kutimiza malipizi maana yake ni kutekeleza kiaminifu sala au matendo aliyotuagiza padre muungamishi ili kulipa adhabu za muda. (Rom 8:17)

Kwa Sakramenti ya Kitubio tunapata neema zipi?
Kwa Sakramenti ya Kitubio tunapata neema hizi;
1. Maondoleo ya dhambi zote kubwa na adhabu ya milele 2. Maondoleo ya dhambi ndogo na adhabu nyingine za muda (Isa 6:5-7, Yoh 8:11) 3. Twarudishiwa na kuongezewa neema ya utakaso 4. Twasaidiwa kuepa dhambi na twapata nguvu ya kutenda mema 5. Twarudishiwa tena mastahili tuliyopoteza kwa dhambi zetu
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 51

Please log in or register to comment or reply.
👥 Alice Wanjiru Guest Apr 14, 2024
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Josephine Nduta Guest Mar 26, 2024
Baraka kwako na familia yako.
👥 Andrew Mchome Guest Feb 28, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Marko marite Guest Dec 6, 2023
Very nice teaching lesson about spiritual issues
👥 David Kawawa Guest Dec 6, 2023
Rehema hushinda hukumu
👥 Mary Sokoine Guest Sep 23, 2023
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Ann Awino Guest Jul 19, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Grace Mushi Guest Jun 19, 2023
Dumu katika Bwana.
👥 Bernard Oduor Guest Apr 25, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Grace Mligo Guest Feb 28, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Janet Sumaye Guest Feb 24, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Nora Lowassa Guest Feb 7, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Miriam Mchome Guest Aug 6, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Esther Cheruiyot Guest May 12, 2022
Endelea kuwa na imani!
👥 Edwin Ndambuki Guest Apr 30, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Susan Wangari Guest Dec 12, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Henry Mollel Guest Oct 11, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Violet Mumo Guest Jul 22, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Nancy Kawawa Guest Apr 30, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Thomas Mwakalindile Guest Apr 23, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Moses Kipkemboi Guest Dec 17, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Ann Awino Guest Jul 1, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 George Ndungu Guest Mar 18, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 David Musyoka Guest Jan 27, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Robert Ndunguru Guest Jan 19, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 George Tenga Guest Dec 20, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Susan Wangari Guest Dec 2, 2019
Sifa kwa Bwana!
👥 Mary Mrope Guest Nov 18, 2018
Nakuombea 🙏
👥 James Malima Guest Nov 16, 2018
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Mary Sokoine Guest Jun 15, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Nora Lowassa Guest Jun 3, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Nora Lowassa Guest May 22, 2018
Mungu akubariki!
👥 Diana Mallya Guest May 11, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 David Sokoine Guest Apr 2, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Nancy Akumu Guest Feb 24, 2018
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Edith Cherotich Guest Feb 5, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Joseph Njoroge Guest Jan 14, 2018
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Carol Nyakio Guest Dec 25, 2017
Neema na amani iwe nawe.
👥 Margaret Mahiga Guest Oct 19, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Henry Sokoine Guest Oct 5, 2017
Rehema zake hudumu milele
👥 Lydia Wanyama Guest Sep 25, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Ruth Wanjiku Guest Apr 29, 2017
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Nora Kidata Guest Dec 21, 2016
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Lydia Wanyama Guest Nov 26, 2016
Mwamini katika mpango wake.
👥 Irene Akoth Guest Sep 9, 2016
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Anna Malela Guest Sep 8, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Samuel Omondi Guest Apr 4, 2016
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Nancy Komba Guest Mar 19, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 George Tenga Guest Feb 24, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Stephen Mushi Guest Sep 16, 2015
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Mary Kidata Guest May 28, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About