Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Unayopaswa kujua Kuhusu Kipindi cha Majilio

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Majilio (pia: Adventi ) ni kipindi cha liturujia ya
madhehebu mbalimbali ya Ukristo (kama vile
Kanisa Katoliki, ya Waorthodoksi , Waanglikana
na Walutheri ) kinatangulia sherehe ya Noeli na
kuanza mwaka wa liturujia. Kinaweza kudumu
kati ya siku 22 na 40.
Jina lake kwa Kilatini ni adventus maana yake
ujio (wa Yesu Kristo ), lakini jina la Kiswahili ni
sahihi zaidi kwa sababu linadokeza kuwa ujio
wa Yesu ni kwa ajili yetu na kuwa alikuja
zamani, anakuja kila siku na atakuja kwa
utukufu mwisho wa dunia.
Maana ya Majilio katika
maisha ya binadamu
Sisi binadamu hatuwezi kuishi daima katika
hali ileile bila ya matazamio. Hasa kijana
anatarajia mambo mapya tena mema. Hivyo
tunajitahidi kuyapata. Asiyetazamia chochote
amevunjika moyo, hana hamu ya kuishi. Lakini
matazamio ya kibinadamu yakimfikia mtu
hayamridhishi moja kwa moja. Kristo tu
anatimiza hamu zote kwa kumkomboa kutoka
unyonge. Majilio yanatukumbusha kila mwaka
matarajio ya kweli na hivyo yanaamsha hamu
ya kuishi kwa bidii ya kiroho.
MAJILIO: Katika Kanisa la Roma.
Katika mwaka wa liturujia ya Kanisa la Roma ,
sherehe ya Noeli inaandaliwa na kipindi cha
Majilio ambacho kina mambo mawili:
kinakumbusha Mwana wa Mungu alivyotujilia
mara ya kwanza, na papo hapo kinatuandaa
kumpokea atakapotujilia tena siku ya mwisho .
Kufuatana na hayo kina sehemu mbili: hadi
tarehe 16 Desemba kinahusu zaidi kurudi kwa
Bwana; siku nane za mwisho kinatuelekeza
moja kwa moja kuadhimisha kuzaliwa kwake.
Urefu wa Majilio unategemea siku
inayoangukia Noeli, kwa kuwa ni lazima yawe
na Jumapili nne. Hivyo basi yanaanza kwa
Masifu ya Jioni ya kwanza ya Jumapili
inayoangukia tarehe 30 Novemba au tarehe ya
jirani zaidi; yanakwisha kabla ya Masifu ya
Jioni ya kwanza ya Noeli.
Kwa jumla ni kipindi cha toba: rangi yenyewe
ni zambarau; haziruhusiwi sherehe za fahari;
ala za muziki na maua vinaweza kutumika
kwa kiasi tu. Masharti hayo yanalegezwa
katika Jumapili ya tatu kwa sababu ya furaha
ya kuona tunakaribia sherehe yenyewe.
Katika kipindi hicho tunaadhimisha tumaini la
Israeli lililotimizwa Yesu alipokuja katika
unyenyekevu wa umbile letu; pia tunangojea
arudi kwa utukufu. Kama alivyotekeleza ahadi
mara ya kwanza, atazitekeleza pia mara ya
pili, ingawa kwake miaka elfu ni kama siku
moja tu. Kati ya majilio hayo mawili, Bwana
anatujilia mfululizo kifumbo katika sakramenti
(hasa ekaristi ) na katika maisha ya kila siku
kwa njia ya matukio na watu (hasa maskini ).
Basi tunapaswa kuwa tayari daima kumpokea
ili siku ya mwisho tukamlaki, naye
atukaribishe kwenye uzima wa milele. Pia
tunapaswa kumuomba aje kutukomboa, yeye
aliye tumaini letu.
Katika safari ya Majilio watu watatu
wanatuongoza tukutane na Yesu:
1. Isaya
nabii wa tumaini, mwenye kipaji cha kutokeza
matazamio ya binadamu na kumhakikishia
atatimiziwa na Mwokozi
. 2. Yohane Mbatizaji ,
mwenye kuhimiza toba kwa kuwa tunapaswa
kupindua maisha yetu ili tukutane vema na
Kristo.
3. Maria , bikira aliyekuwa tayari
kumpokea Masiya kwa upendo na kushirikiana
naye katika kutimiza mpango wa wokovu .
Tukiwafuata hao watatu tunaweza kujipatia
maadili yale yanayotuandaa kumpokea
Mwokozi anapotujilia: ndiyo matunda maalumu
tunayotarajiwa kuyachuma wakati wa Majilio:
1. Kukesha katika imani, sala na kutambua
ishara za Bwana kutujilia katika nafasi yoyote
ya maisha na mwishoni mwa nyakati.
2.Kuongoka kwa kufuata njia nyofu.
3.Kushuhudia furaha inayoletwa na Yesu kwa
kuwa na upole na uvumilivu kwa wenzetu, kwa
tumaini la kuwa bidii zetu zinawahisha ufalme
wa Mungu wenye heri isiyo na mwisho.
4. Kutunza unyenyekevu kwa kufuata mifano ya
maskini wa Injili ambao ndio waliompokea
Mkombozi .
kwa mambo mengi mengine ya dini tembelea
https://ludovicktmedia.blogspot.com/
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Jul 2, 2024
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ George Mallya Guest May 31, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Mar 23, 2024
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Feb 3, 2024
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Oct 30, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest May 18, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Dec 2, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Oct 7, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Sep 28, 2022
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest May 6, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Mar 19, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jul 4, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Apr 17, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jan 26, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Dec 2, 2020
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Nov 22, 2020
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Sep 14, 2020
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest May 9, 2020
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest May 7, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Apr 30, 2020
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Jan 12, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Sep 17, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest May 11, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Peter Otieno Guest Mar 27, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Mar 20, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Jan 30, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Jul 28, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest May 25, 2018
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Mar 19, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ George Mallya Guest Mar 19, 2018
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Feb 28, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Paul Ndomba Guest Dec 23, 2017
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ James Mduma Guest Nov 15, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Sep 11, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Sep 2, 2017
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Robert Okello Guest May 6, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Mar 11, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Nov 26, 2016
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Nov 9, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Jun 29, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Jun 25, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Michael Onyango Guest Mar 25, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ David Chacha Guest Feb 27, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Feb 22, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Jan 22, 2016
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Oct 29, 2015
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Sep 5, 2015
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Aug 23, 2015
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Jul 28, 2015
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest May 16, 2015
Mungu akubariki!

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About