Nini kinatokea wakati Virusi vya UKIMWI (VVU) vinapoingia mwilini na vinakwenda wapi katika sehemu ya mwili?

✍️ SW - Melkisedeck ShineπŸ“… 2022-04-17 07:47:29πŸ’¬ 0 comments⏱️ ~1 min read
πŸ“„ PDF

Virusi hivi vinakaa katika chembechembe nyeupe zilizopo kwenye majimaji ya mwili i wa binadamu hasa kwenye damu, shahawa na maji maji ya ukeni na maziwa ya mama anayenyonyesha. Ndani ya chembechembe nyeupe ndiyo mahali virusi vinakaa na kuendelea kuzaliana. Vikiwa ndani ya chembechembe nyeupe hizi, virusi huendelea kuzaliana hadi kusababisha chembechembe nyeupe hizi kupasuka.

Virusi hivi hupata nafasi ya kuendelea kushambulia chembechembe nyingine nyeupe za damu. Kwa kadri chembechembe nyeupe zilizoshambuliwa zinavyoendelea kupasuka ni kwa kiwango hicho hicho chembechembe nyeupe zinaendelea kuharibiwa na kupungua. Matokeo yake ni kupungua kwa kinga mwilini na mtu kuendelea kudhoofika.

πŸ’¬

Discussion

Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.

0 comment(s)
πŸ” Login required to comment or reply

You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.

Log in to participate
No comments yet.